Wajasiriamali walia na uhaba wa malighafi za kusarifia bidhaa.



 

 

NA FATMA HAMAD,PEMBA

WANAWAKE WAJAsiriamali kisiwani Pemba wamelalamikia juu ya kukosa sehemu maalumu ya kununulia malighafi kwa ajili ya kutengenezea bidhaa  kama vile, Crab pamoja na sabuni.

Wajasiriamali hao wametoa kauli hiyo wakati wakizungumza na mwandishi wa habari hizi mara baada ya kumaliza mafunzo maalumu ya utengenezaji wa bidhaa za vyakula kama vile Makwaru na Achari, huko Ofisi za Jumuiya ya Uhifadhi wa Misitu CFP, Minyenyeni Wete Kaskazini Pemba.

 Maryam Mbarouk Khamis mjasiriamali kutoka Kambini Mchangamdogo na Aisha Ali Hamad wa kiuyu minungwini walisema wamekua wakipata mafunzo kadhaa,  lakini wanashindwa kuzalisha kutokana na kukosa mali ghafi kwa ajili ya kutengenezea bidhaa hizo.

‘’Tunataka vitu tutengeneze lakini sehemu ya kununua ivo vifaa vya kutenezea bidhaa kama vile Ckirabu, shampuu, sabuni hapana, mpaka tuagizishie nje ya Pemba, hilo sisi wajasiriamali wachanga linatukwaza,’’walisema.

Walisema  kwa vile serikali ya awamu ya nane imedhamiria kuwanyanyua wajasiriamali wadogo wadogo, ni vyema kuboresha miundombinu ya upatikanaji wa mali ghafi kwa kuweka kituo maalumu, ili wajasiriamali hao iwe rahisi kuzipata na wazalishe bidhaa kwa wingi na zenye ubora.

Mapema Mkufunzi wa mafunzo hayo ambae pia ni mjasiriamali  Meiye Mbarouk Mussa alisema suala la upatikanaji wa malighafi  pamoja na vifungashio bado ni tatizo, jambo linalopelekea kutokuendele kwa wajasiriamali wadogo wadogo.

‘’Nikweli suala la upatikanaji vifaa kama vyakutengenezea Ckrabu, havipatikani hadi uagizie, hali inayowafanya wajasiriamali wengi watengeneze bidhaa kimazoea,’’alisema.

Aidha aliwasisitiza wajasiriamali hao kuhakikisha wanavisajili vikundi vyao katika mamlaka husika, viweze kuwa rasmi na viweze kutambulika kisheria.

Pia aliwataka  wazisajili bidhaa zao katika mamlaka za ZBS, ZFDA NA BRA, kutasaidia kua zenye ubora na zenye viwango ziweze kuuzwa ndani ya nchi, na hata katika soko la Dunia.


Mapema mwanaharakati na mtetezi wa masuala ya wanawake kutoka Jumuia ya Uhifadhi wa Misitu Pemba CFP Sada Juma Segeja alisema katika jumuia yao, wamekuwa wakiwawezesha wanawake kwa kuwapa mafunzo watengeneze bidhaa, wauze  wajipatie kipato na  wajiinue kiuchumu.

‘’Takribani wanawake 180 tumewapatia mafunzo ya ujasiriamali,watengeneze bidhaa waondokane na changamoto ya umaskini,’’alisema. 


Mafunzo hayo ya siku tatu yaliowakutanisha wajasiriamali wadogo wadogo pamoja na wakulima wa kilimo msitu kutoka shehia za Mchangamdogo, Kambini, Kiuyu minungwini na Chwale, yameandaliwa na Jumuiya ya uhifadhi wa misitu Pemba CFP, ambapo lengo hasa ni kuwafundisha kutengeneza bidhaa mbali mbali, ili wajiingizie kipato chao wenyewe.

Afisa Habari wa Uwakala wa Uwezeshaji Wananchi kiuchumi ZEEA Pemba Abdi Juma Suleiman, alikiri kuepo kwa changamoto hiyo ya upatikanaji wa malighafi pamoja na vifungashio kwa wajasiriamali wa Pemba.

Alisema kwa sasa wako kwenye mchakato wa kuweka sehemu maalumu katika eneo la wajasiriamali Michakaini Chakechake, bidahaa na vifungashio viweze kupatikana hapo, ili kuondosha changamoto hizo.

‘’Tunatarajia kuweka duka maalu litakalokua na vifaavyote ambavyo wajasiriamali wanasafirisha kutoka nje ya Pemba viweze kupatikana hapo,’’alisema.

Alisema pia kutakuepo na Mshine ambayo itatoa vifungashio pamoja na Brendi za biashara zao.

Sera ya Zanzibar ya Wajasiriamali Wadogo na wa Kati ya mwaka  2006  lengo lake ni  kukuza sekta ya wajasiriamali wadogo na wa kati, kuendeleza biashara ndogo ndogo na ujuzi wa kiufundi miongoni mwa Watendaji.




 


Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO