WANAFUNZI DARASA LA SABA LEO KUANZA MITIHANI YAO

                       FATMA HAMAD, PEMBA

Jumla ya wanafunzi 18236,  wa darasa la Saba  waleo hii waanza mitihani yao ya Taifa kisiwani Pemba, ambapo  wanawake ni  9235 ikiwa wanaume ni 9001.

Akitoa tarifa hiyo Afisa Mdhamini wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kwa mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Chakechake mkoa wa Kusini Pemba

 Alisema maandilizi yote ya Mitihani yameshakamilika, hivyo jumla ya wanafunzi  18236 watafanya mitihani yao katika vituo 139 kwenye Skuli mbalimbali kisiwani humo.

Alisema kwa mwaka huu kutakua na jumla ya walimu wakuu 189, huku walimu watakaosimamia mitihani ni 608, huku walinzi kutoka Jeshi la Polisi ni 278.

Aidha Afisa huyo aliwataka walimu kuhakikisha wanasimamia mitihani hiyo kwa uwadili na uwaminifu wa hali ya juu, ili kuepusha udanganyifu na wanafunzi kufutiwa  kwa mitihani yao.

‘’Walimu simamieni kwa uadilifu, kama Wizara ya Elimu hatupendi mwisho wa siku kusikia kama kunawanafunzi wamefutiwa mitihani yao.’’alisema.

Alisema ni vyema kwa vyombo vya ulinzi na usalama  kushirikiana na walimu katika kusimamia mitihani, ili kuna imefanyika bila udanganyifu  na kupatikana kwa matokeo mazuri.

Aidha Mdhamini huyo aliwataka walimu kuhakikisha wanafunga kambi zote za wanafunzi, wapate kupumzika na kujianda vizuri kwenye mitihani yao.

Pia aliwataka wazazi kuwa karibu zaidi na wato wao katika kipindi hiki cha na kuapatia huduma muhimu, ikiwemo chakula, vifaa kwa ajili ya mitihani, ili kufanya vyema kwenye Mitihani yao.

Aidha alisema kwa upande wa darasa la tatu watahiniwa watakaofanya mitihani yao ya kupima maarifa ni 18427.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO