‘’KIMBILIENI HOSPITALI NA SIO KWA WAGANGA MNAPOONA DALILI ZA TB’’


NA FATMA HAMAD, PEMBA

WANANCHI wamehimizwa kujitokeza Hospitali   kupima afya zao wakati wanapojihisi na dalili za ugonwa wa Kifua kiku,ili waweze kugundulika na kupatiwa tiba mapema, na sio kukimbilia kwa waganga wa jadi.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Habari Tehama na Mawasiliano kutoka Kitengo shirikishi Ukimwi, Homa ya Ini, Kifua kikuu, na Ukoma Khalifan Khamis Khalifan wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Ofisini kwake Chak chake mkoa wa Kusini Pemba.

Alisema kwa mujibu wa utafiti wa Shirika la Afya Duniani (WHO)  unaonesha kwamba ugonjwa wa kifua kikuu upo, ingawa bado wagonjwa kugundulika ni shida.

Alisema  takribani asilimia 80 ya wagonjwa kuwagundua inapotea, na hubakia katika jamii  na kutumia dawa za waganga wa jadi.

‘’Licha ya jitihada mbalimbali zinazofanyika kuondosha ugonjwa huo, bado watu hawaji Hospitali, wanaendelea kwenda kwa waganga wa jadi kwani wanaimani kwamba wamerogwa,’’alisema.

Alisema wananchi waliowengi wanaamini kwamba Kifua kikuu ni maradhi yatokanayo na ushirikina, hivyo hukimbilia kwa waganga jambo linalopelekea kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa huo.

‘’Mtu anapoona dalili za kifua kikuu haji Hospitali na hata anaekuja na tukamgudua hatumii dawa zetu bali anatumia mitishamba, na kupelekea wengi kupoteza maisha,’’alieleza.

Alisema ugonjwa wa kifua kikuu unatibika, hivyo ni vyema wanajamii kufika Vituo vya afya kupima afya zao kuweza kugundulika na kupatiwa tiba mapema, ili kuepusha kuenea kwa mambukizi ya maradhi hayo.

Alifahamisha kuwa ugnjwa wa Kifua kikuu unaambukizwa kwa njia ya hewa,  hivyo mgonjwa anaeugua maradhi hayo na kama hajanza kutumia dawa inakua ni rahisi zaidi kuambukiza.

‘’Mtu ambae anaugua ugonjwa huo kama hajaanza matibabu ni rahisi zaidi kuambukiza, hivyo anapokohoa anatakiwa ajizibe mdomoni kwa mikono yake ama kwa kitambaa, ili kuwanusuru na wengine,’’anaeleza.   

Akitaja dalili za ugonjwa huo ni kukohoa kwa muda wa wikimbili mfululizo au zaidi, kupungua uzito ama kukonda bila sababu yoyote, kupata Homa  mara kwa  mara hasa inapofika wakati wa  jioni.

Aidha dalili nyengine ni kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku licha ya kua ni wakati wa baridi, pia kukohoa makohozi ambayo huwa yamechanganyika na damu.

Alisema matibabu ya maradhi hayo ni miezi sita mfululizo, ambapo dawa ni  bure na zinapatikana masaa 24, bila ya gharama yoyote.

Alisema maranyingi wagonjwa wanaowapata na kuwaanzishia matibabu ni wale ambao walishashindikana kwa waganga, na kuamua kuenda Hospitali.

Fatma Khamis Ali (sio jina lake halisi) mkaazi wa kisiwa cha Pemba alisema baada ya kuumwa na kifua alikwenda kwa mganga na kutumia dawa, ingawa hakupata nafuu hadi alipokuja Hospitali na kuanza dawa  za kufua kikuu alipata ahueni.

‘’Nilishahangaika kwa muda wa miaka miwili sijafanikiwa, ila nilipokuja Hospitali nikagundulika nina TB, nilianzishiwa dawa na sasa nashukuru niko vizuri,’’alisema.

Mkurugenzi mkuu kutoka Shirika la afya Duniani WHO Dokta  Tedros Adhanom  Ghebreyesus alisema ingawa juhudi za kimataifa za kutokomeza Kifua Kiku  zimeshaepusha vifo Milioni 750 tangu mwaka 2000, bado ugonjwa huo unasababisha vifo vya watu Milioni 1.3 kila mwaka, na kuathiri mamilioni wengine huku madhara yakisalia kwa Jamii na familia.

Dokta  huyo alizungumza katika taarifa  ya Shirika la Umoja wa Mataifa la afya Duniani huko Geneva,  Machi 18 2024.

Pia kwa mujibu wa WHO  mwaka  2022, iliripoti kukwamua vizuri katika kufanikisha upatikanaji wa huduma ya uchunguzi, dhidi ya kifua kikuu na matibabu.



 

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO