Mgombea Urais ADC Aahidi kupunguza kodi wakati akiingia madarakani.
NA FATMA HAMAD,PEMBA
MGOMBEA
Urais Zanziba kwa tiketi ya Chama cha Allance for Democratic Change ADC Hamad
Rashid Muhamed amesema endapo atapata ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi na kuwa
Rais, atahakikisha anapunguza mtiririko wa kodi, ili kupunguza bei za bidhaa na
kila mwananchi amudu kununua.
Mgombea huyo ameyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi
pamoja na wafuasi wa chama hicho katika mkutano wa kampeni uliofanyika
Micheweni Kaskazini Pemba.
Alisema ushuru wa bidha umekua mkubwa, na kupelekea bidhaa
kupanda bei, hali inayowakosesha baadhi ya wananchi wenye kipato cha chini
kushindwa kupata chakula cha uhakika.
‘’Nitakapo kua Rais nitahakikisha napunguza asilimia 10 ya
kodi, na kila mfanyabiashara atakua na tin namba yake ya kulipa, ili kupunuza mtiririko
na ubadhilifu, na mapato yaingie serikali moja kwa moja,’’alieleza.
Aidha kwa upande mwengine Mgombea huyo alisema atahakikisha analiboresha
Mwani kwa kuweka Viwanda vya kisasa vya
kuchakatia mwani, ili kuona makampuni ya nchi za nje yanafika Zanziba kununua
zao hilo.
‘’Kisiwa cha Pemba tu kunazalishwa tani zaidi ya tani elfu
11 za mwani, hivyo ndani ya siku 100 tukiingia madarakani, tutaweka viwanda vya
kisasa, na tutakua tunauza mwani, unga wa mwani pamoja na bidhaa zinazotokana
na mwani alisema.
Alisema atalifanya zao la mwani linalozalishwa Zanzibar kua
zao kuu la Taifa, na liweze kuuzwa Duniani kote, ili wakulima wafaidike na
kilimo hicho.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama hicho Mwalim Mohamed alisema endapo watachaguliwa na
kuingia madarakani watatoa vifaa vya kisasa kama Maboti kwa ajili ya uvuvi, kwa
wananchi wanafanya shughuli za uvuvi.
‘’Ndugu zangu wa Micheweni tunafahamu nyinyi uchumi wenu
mmeuwelekeza zaidi baharini, hivyo endapo mtatuchagua, tutawapatia Boti za
kisasa pamoja na elimu ya uvuvi wa kisasa, ili kupatikana kitoweyo cha
kutosha.’’alisema.
Alisema ni vyema kwa mwaka huu wananchi wa Micheweni kura
zao wakaziweka kwenye Chama hicho, ili kiweze kubadilisha maisha yao.
Mapema Mgombea Ubunge jimbo la Micheweni wa chama hicho
Hamad Abdala Chande aliwataka wananchi wa Micheweni kuchagua viongozi ambao
wanaumwa na wananchi na wenye sifa ya kua viongozi, na sio kuchagua kwa ajili
ya chama Fulani.
Nao baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo walisema
ADC ni chama ambacho kimeonesha muelekeo mzuri, hivyo haja kwa jamii kukipigia
kura cjhama hicho ili kuleta mabadiliko ya kimaendeleo.
Comments
Post a Comment