MGOMBEA URAIS ADC AAHIDI FUPA KWA WALIMU WA MADRASA AKIPATA URAIS

                                 NA FATMA HAMAD,PEMBA

MGOMBEA Urais Zanziba kwa tiketi ya Chama cha Allance for Democratic Change ADC Hamad Rashid Muhamed amesema endapo atapata ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi na kuwa Rais, atahakikisha walimu wa Madrasa za Qur an  wanalipwa mishaha kama walimu wengine.

Mgombea huyo ameyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi pamoja na wanachama wa chama hicho, katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni uliofanyika Gombani ya kale Chakechake mkoa wa Kusini Pemba.

Alisema walimu wa Madrasa sikuzote wamekua wakiishi katika maisha ya unyonge, hivyo endapo atachaguliwa atahakikisha walimu wote wa madrasa  wanapokea mishahara kila mwezi.

‘’Tunaona walimu ambavyo  wanapoteza muda wao madrasani kwa kutusomeshea watoto wetu elimu ya akhera, lakini tukiangalia maisha yao bado ni ya kusikitisha,’’alisema

Alisema  kwa vile elimu wanayoifundisha ndio msingi wa maisha lakini  hakuna yoyote anaewaangalia, hivyo endapo atachaguliwa atahakikisha anawawekea mazingira rafiki, waendeleze kitabu kitakatifu cha Alla ( S,W).

Aidha kwa upande mwengine mgombea huyo alivitaka vyama vyengine vya  siasa kuhakikisha wanafanya kampeni za kistaarabu, ambazo hazitasababisha kutokea kwa uvunjifu wa Amani Nchini.

Akitoa salamu kutoka kwa Jumuia  ya akinamama mwenyekiti wa wanawake Taifa Nadhira Ali Haji amemtaka Rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania Samia Suluh Hassan kuweka usimamizi wa  hali ya juu katika suala la uchaguzi, ili kunusuru maafa na kuona umemalizika katika hali ya amani na utulivu.

‘’Jicho letu lote lipo kwako wewe mwanamke mwenzetu sisi ni watu wa Amani hatutaki kudhulumiwa, hatutaki kunyanyaswa, tunakuomba usimame imara, ili tubaki salama kabla na baada ya uchaguzi,’’alisema.

Aidha kwa upande mwengine liwataka watoto  kujiepusha na makundi ya kisiasa, ili kujinusuru na vitendo viovu vya uvunjifu wa amani.

Alisema watoto muda wao wa siasa haujafika bali waendelee na masomo yao, ili kuleta matokeo mazuri kwenye mitihani yao.

Kwa upende wake Mwenyekiti wa chama cha ADC Shaaban Ramadhan Itutu alisema Zanziba uchumi wake unategemea zaidi bahari, hivyo endapo wataingia madarakani  wataimarisha uchumi wa buluu na viwanda.

Alisema Zanziba imejaaliwa na rasilimali nyingi, hivyo  mara tu watakapoingia madarakani watapigania  suala la uchimbaji wa mafuta kuona yanachimbwa na  kupatikana, ili kuondosha umasikini kwa wanchi wa visiwa hivyo.

Nae Mgombea wa Urais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania kupitia chama hicho  Wilson Elias Malumbe alisema mara baada ya kuingia madarakani atahakikisha kunapatikana kwa Katiba mpya, ili kuondosha mpasuko na mvurugiko uliomo katika vyama vya siasa.

 

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’