Jamii yatakiwa kuwacha tabia ya kuwaficha wadhalilishaji
NA FATMA HAMAD,PEMBA Mkuu wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya ameitaka Jamii kuwa mstari wa mbele kutoa mashirikiano kwa vyombo vya Sheria wakati kunapotokea vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia Vijijini mwao. Mkuu huyo ameyasema hayo wakati akifungua kongamano maalumu la kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili dhidi ya Wanawake na watoto, ambalo limeandaliwa na Jumuiya ya Sauti ya Vijana [Youth Voice Oganization] lililofanyika Tumbe Mashariki wilaya ya Micheweni Pemba. Amesema suala la udhalilishaji bado ni tatizo ambalo linaendelea kuiathiri Jamii, hivyo ni wakati kwa jamii kuacha muhali na kuvunja ukimwa kusimama kidete kutoa ushahidi ili kuona wahalifu wanaotenda makosa hayo wanatiwa hatiani jambo ambalo litao...