WAVUVI WATAKIWA KUTUMIA ZANA MBADALA KULINDA RASILIMALI BAHARI
NA FATMA HAMAD, PEMBA
AFISA MRADI wa Kuimarisha Uvuvi endelevu na usimamizi wa Mazao ya Bahari
TASFAM Salma Sururu Juma amewataka wananchi wanaofanya shughuli za Uvuvi
kuhakikisha wanafanya shughuli hizo wanatumia zana za kisasa ambazo zinaruhusiwa
kisheria, ili kulindavrasilimali za Bahari na kuona zinakua endelevu.
Wito huo meutoa wakati akizungumza na Maafis Uvuvi na wadau wanaosimamia shughuli za
Uvuvi, katika mkutano wa kuutanbulisha Mardi huo wa kuimarisha Uvuvi endelevu na
usimamizi wa Mazao ya Baharini TASFAM huko ukumbi wa wizara ya Fedh Gombani
Chakechake Kusini Pemba.
Alisema bila kutumia zana za kisasa na zinazokubalika kisheria, sio rahisi rasilimali Bahari
zikaweza kuhifadhika na kua endelevu.
Alisema lengo la Mardi huo ni kuhivadhi Mazao ya Bahari, hivyo ipo haja kwa maafisa Uvuvi
kusimamia ipasavyo kuona wavuvi na wanaofanya shughuli za abaharini kuwa na zana
zinazokubalika, ili lengo liweze kulengo lifikiwe na kuona serikali inaingiza kipato kupitia
Mazao ya Baharini.
“Kama hatutotumia zana zilizombadala hatutopata kitu na hatutoweza kujiingizia
kipato,”alisema.
Shafii Khamis Sudi kutoka Uchumi wa Buluu na Uvuvi Idara ya Maedeleo na Uvuvi alisema
Mradi wa TASFAM utawaezesha wavuvi pamoja wakulima wa Mwani wanaotumia kina kidogo
cha Maji, na wafikie kina kikubwa, ili wazalishe Mazao kwa Wingi,''alisema
''Tunaimani kwamba MRadi huu utakua chanzo Cha mabadiliko na kujiinua kiuchumi kwa
wavuvi pamoja na wale wote wanaofanya shughuli za uhifadhi wa Mazao ya Bahari,’alisema
.
Shaaban Ngwabila kutoka Shirika linaloshughulikia Mazao ya Baharini, alisema watahakikisha
wanashirikiana na Mradi huo na kuondosha baadhi ya changamoto zinazowakaza wavuvi
ikiwemo kuwapata Maboti ya kisasa kwa ajili ya Uvuvi.
‘’Mradi huu utasaidia wavuvi kupata zana za kisasa pamoja na Boti za uokozi pindi
itakapotokezea dharura wakati wakiwa katika shughuli zao za uvuvi,’’alisema.
Nao Maafisa hao walisema watahakikisha wanasimamia ipasavyo, ili kuona rasilimali Bahari
zinatunzwa na zinabakia katika uhalisia wake.
Nae Afisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi DK Salim Mohamed Hamza
aliwataka aliwataka Maafisa hao kuhakikisha wanatoa ushirikiano bega kwa bega na Mradi huo,
kuona unatekelezeka ipavyo na rasilimali bahari zinabakia salama.
Mradi huo ambayo unatekelezwa na Wizara ya Uchumi wa buluu Zanzibar, wizara yaMifugo
na Uvuvi MLF Tanzania, na Dee Sea Fishing, Authority DSFA Tanzani.
Ambapo atatekeleswa kuanzia 2025 hadi 2030 kwa ufadhili wa benk ya dunia.
Unaolenga kuongeza uzalishaji wa thamani ya mazao ya baharini pamoja na kuimarisha
upatikanaji wa masoko na uhifadhi wa rasilimali hizokwa manufaa wa kizazi cha sasa na
kijacho.
MWISHO..


Comments
Post a Comment