VIONGOZI WANAWAKE NA TISHIO LA UDHALILISHAJI

 



                                NA FATMA HAMAD, PEMBA

 Wakati taifa likijivunia ongezeko la wanawake katika nafasi za maamuzi, changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia inaendelea kuwa kikwazo kinachowakatisha tamaa wanawake wengi kuingia katika siasa na uongozi.

 Matusi ya mitandaoni, kejeli zinazolenga mwonekano, vitisho, lugha ya kudhalilisha na propaganda zinazolenga jinsia badala ya uwezo wa kiongozi zinaendelea kushamiri.

 Licha ya kwamba hata Raisi wa Tanzania ni mwanamke bado wapo baadhi ya wanajamii wamekua na  mitazamo tofauti dhidi ya viongozi wanawake kwa kutokana na jinsia zao.

 Wadau wa haki za binadamu wanaonya kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi kwa sababu matukio mengi hayaripotiwi kutokana na hofu, aibu au mila zinazowazuia waathirika kuzungumza.

 WENYEWE VIONGOZI WANAWAKE WANASEMAJE JUU YA HILI

 Mkufu Faki Ali ni Katibu tawala wilaya ya Wete Kaskazini Pemba anasema maranyingi vikwazo vinavyomkwaza katika uongozi wake ni nidharau nakuitwa maneno mabaya.

 Anasema wapo baadhi ya wanajamii wanaona hawawezi kuongozwa na mwanamke, na maranyingi hata inapotokea jambo ukalikemea ama ukawaelekeza jambo lenye maslahi nao, lakini huonekana kama msumbufu tu.

 ‘‘Wapo baadhi ya watu hunidharau na hunipa maneno yanye kukatisha tama, nambiwa hasa huyu bibi kashazeeka kwanini hakai nyumbani kwake akalea wakuu zake anatusumbua tu,’’anasema.

 Anasema muda mwengine hufanyiwa udhalilishaji katika mitandao ya kijamii, mfano Rais wa mungano Samia Suluhu Hassan amekua akichorwa vikatuni, jambo ambalo linawadhalilisha na kuwatia hofu viongozi wote wanawake, kuzungumza na wananchi wao baadhi ya mambo.

 Sheha wa Njuguni Wingwi wilaya ya Micheweni, Hadia Omar Dadi anasema kikwazo kikubwa  anachokipitia ni kupewa matusi na maneno ya dharau, kutoka kwa baadha ya wananchi wake.

 ‘’Tunaambiwa toka lini mwanamke kuwa kiongozi, na kuna baadhi ya mambo wanaume hukaa kikao msikitini na kuamua jambo mfano watoto wasiende tv usiku basi mimi , kama sheha si shirikishwi, hiyo ni dharau.

 Anasema kikwazo chengine kinacho mkwaza ni kukosa usafiri wa kufika katika baaadhi ya maeneo hususani wakati wa usiku.

 ‘’inaweza kukatokea tatizo usiku unapigiwa simu ufike, igawa inakua ni shida, Napata hofu kufika kwenye tukio hasa mida hiyo ya usik,’’anasema.

 Nasra Ali Salim ambae alikua Diwani zaidi ya awamu 10 anasema kikwazo kikubwa ambacho  huwakumba viongozi wanawake ni dhana mbaya kwamba ukiwa kiongozi unakua muhuni.

 ‘’Mwanamke yule yule anakwenda shamba, anakwenda mwani peke yake wala hatiliwi shaka, ila ukipata nafasi ya uongozi tu utaambiwa unakwenda kuvuja maadili yako,’’ anasema.

 WANANCHI

 Zeyana Seif Nassor kutoka Pandani Wete Kaskazini Pemba anasema watu huwadharau viongozi wanawake kwa kutokana nan a jinsia zao, wanahisi hawezi kuongoza.

 ‘’Ni baadhi tu ya watu hususani wanaume wanahisi mwanamke si kiongozi, na wala hawamini kuongozwa na wanawake,’’ anasema.

 Anasema suala la uongozi lianze kufundishwa kuanzia ngazi ya familia, ili kuondosha mitazamo potofu juu ya uongzi kwa mwanamke.

 Omar Khamis mkaazi wa Wingwi wilaya ya Micheweni Kaskazini Pemba anasema suala la uongozi lifundishwe kuanzia ngazi ya familia, watu wafahamu na waondokane na mifumo dume na kua na imani juu ya kiongozi mwanamke.

 WANAHARAKATI

 Mkitu Hassan Mwalim mwanaharakati wa masuala ya wanawake na watoto kutoka Wingwi anasem katika Jamii bado wapo watu huwadharau  na kushambulia kwa matusi viongozi wanawake, kwani wanahisi anaefaa kuongoza ni mwanamme tu.

 ‘’bado viongozi wanawake wanadharauliwa ni hilo ni kutokana na hali zao na jinsiq y,’’anasema.

 Asya Hakim Makame Afisa kutoka Chama cha Wandishi Habari Wanawake Tanzania TAMWA  Zanzibar  anasema kwa sasa wanatekeleza  mradi wa "Tunaweza Pamoja" kwa ushirikiano wa UN Women. 

Mradi huo unafadhiliwa na serikali ya Norway chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa unaolenga kujenga jamii salama dhidi ya vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na wasichana.

 Ikiwa  Mradi huo wa Tunaweza pamoja unatekelezwa katika Mikoa ya Kaskazini mwa Pemba na Unguja, ambao lengo lake ni kuondosha vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na wasichana

 VIONGOZI WA SERIKALI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, maranyingi  anasisitiza kuwa wanawake wanapaswa kuthaminiwa kwa uwezo wao wa kuongoza badala ya kuhukumiwa kwa jinsia yao. 

 Mara kadhaa amekemea lugha za matusi na udhalilishaji dhidi ya wanawake katika siasa.

 Spika wa zamani wa Bunge, Anne Makinda, aliwahi kueleza kuwa wanawake wanaoingia kwenye uongozi hukutana na vikwazo vikubwa kuliko wanaume, ikiwemo matusi, kejeli na mashambulizi ya maneno yanayolenga kuwakatisha tamaa.

 Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dkt. Asha-Rose Migiro, amesisitiza mara kwa mara umuhimu wa kuwawezesha wanawake kushiriki katika maamuzi bila hofu ya ubaguzi au udhalilishaji.

 VIONGOZI WA DINI

 Sheikh Said Ahmed Mohamed, kutoka Ofisi ya Mufti Pemba, anasema dini imempa nafasi mwanamke ya kushika nafasi yoyote ya uongozi, ilimradi asivunje miiko na maadili ya Taifa lake.

 Yohana Ali Mfundo ambae ni Mchungaji kutoka Kanisa la Mkusanyiko wa Mungu Tanzania (TAG) lililopo Ngerengere Chake Chake anasema, dini yao haijambagua mwanamke asiwe kiongozi, ispokua aendeshe kwa kufuata taratibu na sheria zinavyoelekeza.

 ZAECA

 Kamanda wa kudhibiti na kupambana na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) mkoa wa Kusini Pemba Mustafa Hassan Issa anasema wao hawapokei malalamiko ya udhalilishaji, isipokua ni kwa kesi za rushwa.

 MIKATABA

 Kwa mujibu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na tafiti za afya na maendeleo ya jamii, wanawake wengi nchini bado hukumbana na aina mbalimbali za ukatili wa kijinsia, ikiwemo ukatili wa kimwili, kingono na kisaikolojia wa mwaka 2022

 Takwimu hizi zinaonesha kuwa ukatili dhidi ya wanawake bado ni changamoto ya maendeleo.

 Tanzania inaendelea kupiga hatua katika kuongeza ushiriki wa wanawake katika nafasi za maamuzi, Hata hivyo, ongezeko la uwakilishi halijaondoa changamoto ya udhalilishaji wa kijinsia. 

 Mara nyingi viongozi wanawake hukumbana na mashambulizi yanayolenga utu wao badala ya hoja zao.

 Kwa mujibu wa Serikali ya Tanzania, wanawake wanawakilisha zaidi ya asilimia 36 ya wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na takribani asilimia 40 ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, hatua inayoonyesha maendeleo katika ushiriki wa kisiasa kuanzia 2020-2025. 

 Kwa upande wa takwimu za ukatili wa kijinsia, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar imekuwa ikitoa taarifa za kila mwezi.

 Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakwimu wa Serikali kwa mwaka 2024 jumla ya matukio 1,809 ya ukatili wa kijinsia yameripotiwa, visiwani Zanzibar.

 kwa mujibu wa Utafiti wa Viashiria vya Demografia na Afya nchini Tanzania (Tanzania Demographic and Health Survey - TDHS) Aidha, wanawake takribani asilimia 14 Zanzibar wamewahi kupitia ukatili wa kimwili, huku karibu mwanamke mmoja kati ya kumi akiripoti kufanyiwa ukatili wa kingono.

 Alisema Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakuimu mkuu wa serikali ya Zanziba Machi 2026 kuliripotiwa matukio 103 ya ukatili na udhalilishaji, ambapo watoto ilikua ni 84 sawa na asilimia 81.6 wanawake wakiwa ni 17 sawa na asilimia 16.5.

 Utafiti uliofanywa na Taasisi ya Women at Web kwa kushirikiana na Tamwa Tanzania hivi karibuni asilimia 79 wanawake wanasiasa na wanaharakati wa kisiasa, walifanyiwa ukatili wa kijinsia walifanyiwa ukatili wa kijinsia kwa njia ya mtandao katika uchaguzi mkuu wa 2020.

 CHANZO MWANANCHI.

 Hotuba ya Waziri wa nchi - 0fisi ya Rais - Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala bora Mheshimiwa DKT Haroun Ali Suleiman imeweza kushirikiana na taasisi mbali mbali katika kupambana na kupunguza kesi za udhalilishaji kutoka kesi 348 kwa mwaka 2023/2024 hadi kesi 292 kwa mwaka 2024/2025.

 Katika miaka ya hivi karibuni, China imekuwa ikihimiza maendeleo ya sifa bora ya mambo ya wanawake nchini humu, siku zote inafanya juhudi za kujenga mazingira ya kimataifa yanayosaidia maendeleo ya wanawake, na kutoa mchango muhimu kwa ajili ya mambo ya wanawake duniani.

 


MWISHO.

 

Comments

Popular posts from this blog

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

HOFU YA UDHALILISHAJI MTANDAONI INAVYOWANYAMAZISHA WANAWAKE

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI