MARADI WA MALEZI,MAKUZI YA AWALI YA MTOTO ULIVOBADILISHA MITAZAMO KWA WAZAZI PEMBA
NA FATMA
HAMAD, PEMBA
WAZAZI NA
WALEZI kisiwani Pemba wamesema uwepo wa Mradi wa Malezi,Mkuzi na Maendeleo
ya awali ya mtoto umewasaidia, kwani
wameelewa umuhumu wa kukaa karibu na watoto wao na kucheza nao.
Walisema
mradi umewazesha kujua kipindi cha siku
1000 ndicho kipindi pekee mtoto anachohitaji uangalizi zaidi na kuwandaliwa
kuwa mtoto bora wa baadae.
Akizungumza
katika kikao cha tathmini juu ya mradi huo mzazi Asha kutoka N’gambwa Chake,
alisema baada ya kupata elimu ya malezi na makuzi ya awali ya mtoto amejenga
ukaribu na watoto wake na wamekua na uthubutu wa kuiga baadhi ya mambo ambayo
wanamuona akiyafanya.
‘’Kwa
mfano wakati nikiwa jikoni nikipika nilikua mtoto namuweka mbali kwani nahisi
ananikera, ila kwa sasa napika nae na nikimenya mbatata yeye anamenya vitunguu,’’alisema.
Kwa
upande wake mzazi Kassim Masoud Hamad kutoka Piki Wete alisema zamani ilikua watoto
wake hawakua na ukaribu nawala
hawakisubutu kumueleza shida zao, bali wakimwambia mama yao.
‘’Nashkuru
elimu hii ya malezi ya makuzi na maendeleo ya mtoto yametubadilisha kwani kwa
sasa ninakawaida ya kuwaita watoto wangu na wameondokana na woga wananieleza kila
wanachokihitaji bila ya hofu,’’alisema.
Zulekha
Othman Omar muhudumu wa afya ngazi ya Jamii kutoka Shungi Chakechake alisema
mradi wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto umeleta mapinduzim makubwa
katika jamii, kwani wengi wameona ile thamani ya kuwa na ukaribu na watoto wao.
‘’Nilipokenda
kwa mzazi Amina Ali (sio jina lake halisi) kwa mara ya kwanza mwenye mtoto wa miezi sita aliniambia hana tabia ya kukaa na kuzungumza wala kucheza nae yule mtoto wake kwani
anahisi ni mchanga hafahamu chochote,’’alisema.
Alisema
mara baada ya kurudi tena kwa ajili ya kujua maendeleo yao, alisema baada ya kupata elimu amekua akicheza ,nae na amemgundua kwamba
anasikia, anafahamu na anafurahia kitendo hicho cha kucheza na mamayake.
Mapema
Mratibu wa Madrasa Early childhildhood Programme Zanzibar upande wa Pemba Haji
Ali Hamad alisema kwa mujibu wa Sayansi
ya ECD katika kipindi cha awali cha siku 1000 ndicho kipindi muhimu ambacho
mtoto anahitajika kupata huduma hizo, kwani ndipo akili ya mtoto inachukua
mambo kwa haraka.
‘’Wazazi niwambie kipindi hichi ndicho cha
kuwekeza zaid, kwani akili yake haija beba mambo mengine utakachomfundisha
anakishika, kuliko kupiga kelele na wa miaka 16,’’alisema.
Alisema
ili mtoto akue akiwa vizuri kiakili anahitaji uangalizi wa hali ya juu kutoka
kwa wazazi wake, hivyo ipo haja wazazi kuwakaribu na watoto wao, licha ya
pirika za maisha walizonazo.
Mtaalamu
kutoka wizara ya Afya Pemba Fadhila Abdulla Abdi alisema mtoto anahitaji kuzungumzishwa
kuanzia tokea akiwa tumboni kwa mama
yake.
Alisema
kiutaalamu mtoto alietumboni anasikia kila kitu kinachozungumzwa, hivyo ni
vyema mama anapokua na ujauzito kuepuka migogoro na kuwa na mawazo mabaya, ili
kuzaa mtoto mwenye akili timamu na mwenye afya bora.
‘’
Wazazi wenzangu tuzungumze na watoto wetu kuanzia wakiwa tumboni, na pia mama
anapokua na ujauzito anahitajika uangalifu wa hali ya juu (STIRES),’’alisema.
Mradi
huo wa Vroom unatekelezwa katika Visiwa vya Unguja na Pemba, ikiwa kwa Pemba ni
wilaya ya Wete na Chakechake, unafadhiliwa na Shirika la Bezos Familiy
Fondation, lengo lake ni kutoa uwelewa kwa wazazi na Wahudumu wa afya ngazi ya
Jamii, juu ya malezi na makuzi ya awali ya mtoto.
Mradi
huo ulianza mwakajana na unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwaka huu.
MWISHO.


Comments
Post a Comment