ADAIWA KUMLAWITI MTOTO WA MIAKA MIWILI


NA FATMA HAMAD, PEMBA

KIJANA SHAAME Ali Hamad anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka (38) mkaazi wa Mchangamdogo wilaya ya Wete Pemba, ashikiliwa na adaiwa za kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka miwili na miezi mitatu.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko nyumbani kwake, mama wa mtoto huyo alisema mtoto wake alifanyiwa tukio hilo la kinyama akiwa nyumbani kwa jirani yake ambae ni mtuhumiwa.

Alisema, siku ya Ijumaa ya tarehe 26/06/2026 akiwa nyumbani kwake akifanya shughuli zake, mtoto wake alikuwa hajamuona muda mrefu, ndipo aliponza kumtafuta na kumuita kwa jina ingawa hakubahatika kumuona kwa wakati huo.

‘’Nilirudi nyumbani kuendelea kufua lakini nilifanya wasiwasi na nikaamua kwenda kumtafuta tena, ndipo nikamkuta amekaa nje ya mlango wa nyumba ya Shaame, akiwa na hali ya huzuni,’’ alisema.

Alisema, alimwambia asimame ili waondoke lakini mtoto huyo hakuweza kusimama na akambeba na kwenda nyumbani kwao na kumueka huku yeye akiendelea na shughuli zake.

Alisema, baada ya muda mfupi alimuona amelala kifudifudi huku suruali yake aliyokuwa amevaa ikiwa na uchafu.

 ‘’Hapo nilishtuka, nikaanza kumuangalia vizuri na nikaona sehemu zake za siri za nyuma haziko sawa, kwani zinatoka uchafu,’’alisema.

Mama huyo alieleza kuwa, baada ya kuona hali hiyo walikwenda kituo cha afya Kinyikani, na madaktari wakawapa barua ya kwenda kituo cha Polisi Mchangamdogo, na hapo wakapewa Pf 3 na kwenda hospitali ya wilaya Kinyasini Wete kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi.

‘’Tulipofika Kinyasini alifanyiwa uchughuzi na tukaambiwa   kwamba mtoto wetu alishafanyiwa kitendo cha udhalilishaji,’’ alifafanua mama huyo.

Baba mzazi wa mtoto alisema, tangu siku ya Ijumaa alipofanyiwa unyama huo, mtoto wake amekua akitokwa na uchafu, kinyesi bila kuzuilika, na kulazimika kuvalishwa pempasi muda wote.

‘’Kwakweli tokea alipopatwa na tukio hilo amekua choo chake hakizuiliki, ilibidi muda wote tuvalishe pempasi kutokana na athari aliyoipata,’’alisimulia.

Alisema, licha ya tukio hilo la kinyama bali kuna watu wamekua wakimuendea na kumtaka wafanye suluhu, ili kesi isiende kwenye vyombo vya Sheria.

 ‘’Wanakuja watu wasiopenda nguvu za wenzao na kunipa vitisho nikubali suluhu, ila kwa unyama aliofanyiwa mtoto wangu hilo silikubali, kama ni ujirani alishaupoteza yeye,’’alisema.

Hivyo aliiomba Serikali na wanaharakati kusimama imara kuhakikisha hatua kali za kisheria zinachukuliwa dhidi ya muhalifu huyo, na kuona haki inatendeka.

Sheha wa Mchangamdogo Assaa Makame Said alikiri kuepo kwa tukio hilo katika shehia yake na kusema, amelipokea kwa huzuni, huku akiwataka wazazi wa mtoto huyo kutosikiliza maneno ya jamii kwa ajili ya kuifanyia suluhu kesi hiyo.

Mratibu wa wanawake na watoto shehia ya Mchangamdogo Mbeu Makame Bakar alisema, amefurahishwa na kitendo cha wazazi wa mtoto huyo kuwa na mwamko wa kulipeleka katika mamlaka husika kwa ajili ya kuchukuliwa hatua.

Suleiman Hamoud Salim ambae daktari kutoka Spitali ya Kinyasini Wete alisema, siku ya ijumaa aliletewa mtoto huyo aliedaiwa kulawitiwa, na baada ya kumfanyia uchunguzi aligundua kwamba tupu yake ya nyuma haikua katika hali ya kawaida kwani alikuta michubuko na alikua akitoka kinyesi na uchafu.

‘’Baada ya kumfanyia uchunguzi nilikuta michubuko katika tupu yake ya nyuma na huku akiwa anatoka kinyesi,’’alisema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) William Mwampagale alisema kuwa, hajapokea taarifa za tukio hilo ingawa wanapopokea taarifa za matukio kama hayo wanafanya uchunguzi na kuyachukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuyafikisha mahakamni kwa ajili ya kuendelea na taratibu.

 "Baada ya kupokea taarifa ya tukio, huwa tunaliangalia ikiwa ni muhimu kujulikana kwenye jamii kwa faida yao, basi tunaita vyombo vya habari na kulitolea ufafanuzi lakini ikiwa kwenye umma hakuna umuhimu wa kulitoa kwa maslahi ya jamii, basi tunachukua tu hatua za kisheria tu na sio kutoa kwenye vyombo vya habari," alisema Kamanda huyo.

 

                                         MWISHO.

 

 

 

Comments

Popular posts from this blog

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’