WANANCHI KISIWANI Pemba ambao walichukuliwa Ardhi zao
kwa ajili ya Ujenzi wa Miradi ya Maendeleo na Uwekezaji waliokua hawajalipwa
fidia zao wameiomba Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi kuwasikiliza kilio
chao na kuwafuatilia ili wapate haki zao serikalini.
Akizungumza katika kikao cha
Uwasilishaji wa Ripoti ya Uandaaji wa Sheria ya Sekta Miliki Zanzibar
kilichofanyika Gombani Chakechake Pemba, Suleiman Mansur mwananchi wa
Chakechake alisema tokea alipochukuliwa ardhi yake kwa ujenzi wa Skuli ya
Uwandani bado hajalipwa fidia yake.
Alisema kila siku amekua
akihangaika kwa ajili ya kutafuta haki yake, lakini ameshindwa, hivyo aliomba Wiazara ya Ardhi kuwafuatilia kero
lao na kuwaonesha njia ya kupita, ili kuona wanapata haki zao,
‘’Kila siku nahangaishwa mara
peleka barua kwa mkuu wa Wilaya mara Mkoa wala sjaona lolote, tunawaomba
wenzetu wa wizara ardhi mtusaidie tupate fidia zetu,alisema.
‘’’alisema,
Kwa upande wake wakili wa
kujitegemea kutoka Chake chake Zahran
Mohammed Yussuf ambae alishiriki kikao hicho, alisema ni vyema kuwepo na
Mamlaka moja tu ambayo inatoa hatimiliki kwa wananchi, jambo litalosaidia
kupunguza migogoro ya Ardhi katika Jamii.
‘’Utakuta kuna BPR, Wokfu,
Wizara ya Ardhi, zote zinatoa umiliki ardhi, hivyo kuepo kwa mlolongo wa
Taasisi kunachangia migogoro, ni vyema serikali kuweka mamlaka moja
tu,’’alisema.
Mapema Muezeshaji wa kikao
hicho Ali Ali Hassan alisema kwa mujibu wa kifungu cha 17 (C) cha Katiba ya
Zanzibar yam waka 1984 kinasema mwananchi
anatakiwa alipwe fidia yake kabla ya
ujenzi kuanza na inayolingana na mali yenyewe.
Hivyo aliwataka wananchi hao
ambao wanadai fidia zao kuenda Mahkamani na kudai haki zao.
Afisa Mdhamini wizara ya Ardhi
na Maendeleo ya Makaazi Bakar Ali Bakar, alisema kuepo kwa Sheria ya Sekta
Miliki Zanzibar
kutasaidia kuondokana na
migogoro ya ardhi Nchini.
MWISHO.
Comments
Post a Comment