WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUANDIKA HABARI ZILIZOJIFICHA

 

Waandishi wa habari Pemba wametakia kuibua na kuandika habari zinazochangia kufanyika kwa vitendo vya udhalilishaji katika maeneo yasio maarufu (yasio tambulika).

 Agizo hilo  limetolewa na Mratibu wa Mradi wa Tunaweza pamoja kutoka Tamwa Zanzibar Asya Hakim Makame  katika mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari  wa vyombo mbalimbali,yaliyofanyika Ofisi za TAMWA Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba.

 Alisema yapomaeneo kadhaa ambayo wanawake na watoto wamekua wakidhalilishwa kama vile kwenye usafiri wa Umma, Bandarini, Masokoni na hata katika mitandao ya kijamii, na hata kwenye viwanja vya Skukuu za Iddi.

 Alisema licha ya udhalilishaji unaofanywa katika sehemu hizo, lakini bado wandishi wa habari hawaripoti, hivyo ipo haja kwa sasa kutupa jicho lao na kuibua kesi hizo, ili kuona usalama unatawala ndani ya maeneo hayo ambayo sio rasmi.

 ‘’Wandishi wa habari msiishie tu kuandika udhalilishaji unaofanywa  Madrsa, Mitaani,amma Maskulini, bali jikiteni  masokono, bandarini, kwenye daladala na hata katika mitandao ya kijamii ili nako huko kubaki salama,’’alisema. 

 Kwa upande wake Mkufunzi wa mafunzo hayo toa  Haji Nassor Moh’d alisema miongoni mwa vitendo hivyo vya udhalilishaji ambavyo vimekua vikifanyika ni pamoja na usafirishaji haramu wa binaadamu.

 Aidha alisema bado takwimu zinaonesha kuongezeka kwa  matukio ya udhalilishaji kwa wanawake na watoto visiwani Zanziba.

 Alisema Takwimu kutoka Ofisi ya Mtakuimu mkuu wa serikali ya Zanziba Machi 2026 kuliripotiwa matukio 103 ya ukatili na udhalilishaji, ambapo watoto ilikua ni 84 sawa na asilimia 81.6 wanawake wakiwa ni 17 sawa na asilimia 16.5.

 Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo walisema mafunzo  yatawasaidia katika majukumu yao kwani watatumia kalamu zao kuelimisha jamii juu ya vitendo vya udhalilishaji vinavyoendelea kutokea kwenye maeneo hayo ambayo sio rasmi.

 Mafunzo hayo kwa waandishi wa habari ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa "Tunaweza Pamoja" unaotekelezwa ma UN Women kwa kushirikiana na TAMWA Zanzibar kwa ufadhili wa Serikali ya Norway chini ya mpango wa Umoja wa Mataifa unaolenga kujenga jamii salama dhidi ya vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na wasichana.

 Mradi huo wa Tunaweza pamoja unatekelezwa katika Mikoa ya Kaskazini mwa Pemba na Unguja, ambao unalengo la kuondosha vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na wasichana.

 MWISHO.

 


Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’