TUNAANDAA SHERIA YA BIASHA KUPUNGUZA MIGOGORO YA ARDHI ''MDAMINI ANAESEMA



NA FATMA HAMAD, PEMBA

 Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Zanziba imesema, imo kwenye mchakato wa  kuandaa Sheria ya Biashara ya Majengo na Ardhi kwa lengo la kuimarisha sekta ya uwekezaji wa majengo pamoja na usimamizi bora wa ardhi visiwani Zanzibar.

 Hayo yameelezwa na Afisa Mdhamini wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi Bakar Ali Bakar katika kikao cha uwasilishaji wa ripoti ya uandaaji wa sheria ya sekta  miliki Zanzibar kilichofanyika ukumbi wa Wizara ya Fedha Gombani kisiwani Pemba.

 Afisa huyo alisema kwamba Hatua hiyo inalenga kuweka mfumo rasmi wa kusimamia biashara ya nyumba, viwanja, upangishaji wa nyumba pamoja na mauzo ya mali zisizohamishika, ili kuhakikisha shughuli hizo zinafanyika kwa uwazi na kwa kufuata sheria.

 ‘’Tunandaa sharia ya biashara ya Majengo na Ardhi ili kuepo na usimamizi mzuri wakati watu wanapouziana Ardhi ama kukodishana Majengo, ambapo kutaimarisha sekta ya uwekezaji Nchini,’’alisema.

 Kwa upande wake Muezeshaji wa kikao hicho Ali Ali Hassan alisema sheria hiyo itasaidia kupunguza migogoro ya ardhi pamoja na kuongeza uwazi katika shughuli za ununuzi, uuzaji na ukodishaji wa majengo na viwanja.

 ‘’Naamini kuwepo kwa Sheria hiyo itapunguza madalali matapeli ambao wanachangia kwa kiasi kikubwa kuzuka kwa migogoro ya ardhi katika jamii zetu,’’alisema.

 Alisema kumekuepo na madalali wengi wanaofanya shughuli za udalali bila ya kua na elimu ya kazi hiyo na bila ya utambulisho wowote, hivyo serikali imeamua kuweka sheria hiyo ambayo itakua ni chachu ya kupunguza mifarakano isiyoyalazima.

 Nao washiriki wa kikao hicho walisema kuwa kuwepo kwa sheria hiyo kutasaidia kulinda haki za wanunuzi, wauzaji pamoja na mawakala wa majengo, sambamba na kuimarisha mazingira salama ya uwekezaji Zanzibar.

 Uandaaji wa Sheria ya Biashara ya Majengo na Ardhi Zanzibar unatarajiwa kuwa hatua muhimu katika kuimarisha sekta ya uwekezaji, kuongeza mapato ya serikali, pamoja na kuleta maendeleo endelevu katika matumizi bora ya ardhi na majengo.

 MWISHO





 

 

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’