“Uchumi, unavyofifiza Ndoto za Wanawake Wenye Ulemavu kufikia uongoz’’


NA FATMA HAMAD, PEMBA

Katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2025, Tanzania imeshuhudia wimbi jipya la wanawake wenye ulemavu wanaojitokeza kugombea nafasi za uongozi  kutoka udiwani, ubunge hadi uwakilishi wa majimbo.

Ingawa  nyuma ya safari hiyo ya kisiasa, kuna simulizi  ya kiuchumi, unavyosababisha  wanawake hao kufikia malengo yao ya kisiasa.

Makala hii inachambua jinsi uchumi wa wanawake wenye ulemavu unavyoathiri ushiriki wao katika maamuzi, nafasi zao za uongozi, na sauti yao katika jamii ya Tanzania, hususan Zanzibar, kwa kuzingatia takwimu, sheria, na mikataba ya kimataifa.

Utafiti wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wa mwaka 2022, unaonesha zaidi ya asilimia 73 ya watu wenye ulemavu nchini, wanafanya kazi katika sekta zisizo rasmi hususan kilimo, uvuvi na biashara ndogondogo.

 Maranyingi, wanawake wenye ulemavu wanabaki nyuma zaidi kwa sababu ya changamoto hiyo ya uchimi, mitajina ukosefu wa fursa za kifedha, hali hii huwafanya kushindwa kugharamia kampeni za kisiasa au kushiriki ipasavyo katika uongozi.

Katika uchaguzi wa mwaka 2025, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilisajili wagombea 1,735 wa ubunge, kati yao wanawake walikuwa 558 (sawa na 32%), hata hivyo, ni wagombea 27 tu waliokuwa na ulemavu wakiwemo wanawake, chini ya asilimia 2 ya jumla ya wagombea wote.

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar  (ZEC), ilithibitisha wapiga kura 717,557, ambapo wanawake walikuwa asilimia 53.

 Hata hivyo, uwiano huu haukuakisi kwenye orodha ya wagombea wenye ulemavu, ambapo wachache sana waliweza kufikia hatua za mwisho za uteuzi au ushindi.

Baadhi ya wanawake wenye ulemavu walijitokeza kugombea kupitia vyamavya siasa, ingawa walikosa rasilimali fedha na kupelekea wenye pesa zao kujichiukulia majimbo, kutokana na mfumo wa uchaguzi ulivyo.

Halima Suleiman Ali mkazi wa Mtambile mwenye ulemavu wa uoni hafifu, amejitosa kuwania udiwani Wadi ya Mtambile, ingawa hakufanikiwa, anasema suala la uchaguzilinahitaji gharama.

“Uchumi wetu ni dhaifu, na si rahisi kugombea bila fedha, wengi wetu tunabaki kuwa wafuasi badala ya viongozi,” anasema.

Anasema fomu moja pekee ya udiwani ni shilingi 50,000, ukipita kuna pesa za kampeni ambapo unatakiwa ufanye mkutano kila shehia, napo hapo fedha huhitajika.

Mwingine ni Katija Mbarouk Ali mwenye ulemavu wa viungo mkaazi wa Kiuyu Minungwini wilaya ya Wete, aliyegombea Uwakilishi jimbo la Kojani, anasema uchumi ni moja ya kikwazo kinachowakosesha kuingia kwenye maamuzi.

Anasema ameshagombea marambili na wala hawajawahi kufanikiwa, ingawa mwaka 2020 aligombea nafasi hiyo kupitia viti maalumu.

Anasema ambacho amekigundua kushindwa yeye kuingia kwenye maamuzi ni kukosa pesa, kama wanavyofanya wingine.

‘’Fomu tu ya uwakilishi ya kugombea ni shilingi 500,000 hujapata pesa za kuchapisha mabango, vipeperushi na hata kufanya mikutano ya kampeni, hicho ni kikwazo kinachorudisha nyuma,’’anasema.

Marahii aliamua kugombea jimboni, kwani alihisi angeweza kupata unafuu wa gharama, ila anasema mambo ni magumu kwake kwa pande zote, kutokana na uchumi wake.


Bi Amina Abdala Said mwenye ulemavu wa viungo mteule wa udiwani viti maalum, kupitia Chama cha ACT WAZALENDO wadi ya Changaaweni Mkoani, anasema kulingana na mifumo ya harakati za uchaguzi ilivyo, wanawake wenye ulemavu ni vigumu kupata nafasi.

‘’Kwakweli sasahivi uongozi ni biashara, hivyo kama huna pesa huwezi kulikamata jimbo, hivyo sisi wenye ulemavu ni vigumu, kushika nafasi, na badalayake huzichukua watu wenye pesa zao,’’anaeleza.

Tumu Mwalim Massoud wa Wingwi Micheweni, ambae amegombea uwakilishi Jimbo la Wingwi kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mkuu wa 2020, anahamu ya kuwa kiongozi, ingawa akikumbuka gharama zilizomtoka, hatamani tena kugombea.

Anasema mbali na gharama ya fomu ya Uwakilishi ya shilingi 500,000 pia unahitajika ufanye mikutano wastani mitano kwenye jimbo, usafiri, vipaza sauti na vyote hivyo vinahitaji uvigharamikie mwenyeo.

Baada ya kumalizika kwa uchaguzi na kushindwa, alianza kuuza gari yake ya kutembelea, N’gombe wa mamake ili apate fedha ya kulipa madeni.

‘’Kwa sasa najifikiria kugombea tena kwa sababu nakumbuka maumivu ya kulipa madeni, ingawa natamani niingie tena kwani ndoto yangu ya kuwa kiongozi haijakamilika,’’anasema.

Anasema kwa mujibu wa utaratibu ulivyo, anaetaka kugombea uwakilishi, anatakiwa alipie chamani shilingi 100,000 kwa kuchukua fomu.

Pia anatakiwa kulipa Tume ya uchaguzi shilingi 500,000, wakati huo huo ukitakiwa kuchukua fomu, kwa ajili ya kuendelea na harakati nyingine.

JAMII

Hadia Omar Ali mkaazi wa Sizini anasema, ikiwa serikali haitokipatia ufumbuzi kilio hicho, siku zote wanawake wenye ulemavu wataendelea kushika mkia tu kwenye chombo cha mamuzi.

Mohamed Hassan Ali mkaazi wa Wete, anasemawanawake wenye ulemavu hawawezi kumudu gharama za chaguzi, kwani uchumi wao uko chini.

JUMUIA ZA WATU WENYE ULEMAVU

Hidaya Mjaka Ali kutok Jumuia ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), anasema uchumi bado kikwazo kinachopelekea wanawake wenye ulemavu kushindwa, kuonekana kwenye maamuzi.

Anasema bila ya kuwepo uwezeshwaji kwa wanawake hao, wengi wao hawana kipato kikubwa ambacho kianawezesha kumudu shughuli za uchaguzi.

‘’Chaguzi za sikuhizi, zimekua ni biashara, kama huna pesa huwezi kufanikiwa, na ndiomaana sisi wenye ulemavu hatupati nafasi, kwani uchumi wetu ni wa kipato cha chini,’’anaeleza.

Mashavu Juma Mabrouk ni Mratibu wa Baraza la watu wenye Ulemavu kisiwani Pemba, anasema wanawake wenye ulemavu, wamepata hamasa ya kuingia kwenye harakati za maamuzi, ingawa bado wanashindwa kumudu gharama.

Anasema wingi wa wanawake wenye ulemavu ni masikini wa kipato, hawamiliki hata mahitaji ya nyumbani kwake, seuze ya uchaguzi.

WANAHARAKATI

Tatu Abdalla Mselem ni mwanaharakati wa masiuala ya utetezi kwa wanawake, watoto, mayatima na wanaoishi katika mazingira magumu(TUJIPE) nasema katika zama za sasa pesa ndio kigenzo kikubwa kinachosababisha watu kushika nafasi za uongozi.

Anasema Wanawake Wenye Ulemavu sio rahisi kufanikiwa kuyakamata majimbo, kwani uchumi wao ni mdogo, gharama za chaguzi zimekua kubwa hawawezi kuzimudu.

‘’Kutokana na gharama za Chaguzi zilivyopanda, napata kusema Wanawake Wenye Ulemavu ni vikugumu kuyakamata majimbo na kuingia kwenye maamuzi kwani hali zao wenyewe ni duni,’anasema.

Mkurugenzi wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar (TAMWA)Dk. Mzuri Issa Ali anasema wamekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu, ushawishi wa sera, na kuwajengea wanawake wenye ulemavu.

NINI ATHARI YAKE

Ikiwa vyama vya siasa pamoja na serikali havikukaa chini na kutafakari mifumo ya uchaguzi iliyopo sasa, basi Wanawake Wenye Ulemavu na hata wasio na ulemavu itakua ni nadra kushika uongozi,’’wanasema wananchi.

NINI KIFANYIKE?

Ili kuona Wanawake Wenye Ulemavu na wao wanashiriki kwenye harakati za uchaguzi na kuingia kwa wingi katika maamuzi, ipo haja kwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kuweka ruzuku maalum, mafunzo pamoja na mitaji ambayo itawasaidia wagombea hususan wanawake wenye ulemavu.

 MIKATABA

Tanzania imeridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD), wa mwaka 2006  kinahimiza serikali, kuhakikisha ushiriki sawa wa watu wenye ulemavu katika siasa na maamuzi.

Hata Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na haki za kisiasa ya mwaka 1966 ibara ya 25, kila raia ana haki ya kupiga kura na kuchaguliwa, katika uchaguzi wa kisiasa.

Katiba ya Zanzibar ya 1984,kifungu chake cha 21(1) nacho kinatambua haki ya kila raia, kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi bila ubaguzi.

Kifungu kidogo cha (3) kinaeleza kwamba, kila mzanzibari anayohaki ya kushika nafasi yoyote ya kazi na shughuli yoyote iliyoko chini ya mamlaka ya Zanzibar.

Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar ya mwaka 2018 inaweka mazingira ya upatikanaji wa haki sawa, kwa wagombea wote, wakiwemo wenye ulemavu, lakini utekelezaji wake bado unahitaji nguvu zaidi.

Sheria ya watu enye ulemavu namba 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 29 kinaeleza, umuhimu wa watu wenye ulemavu kufikia miundombinu pamoja na taarifa, mawasiliano na haki zote za kibinadamu.

Katika programu za uchumi nchini Tanzania, hata pale ambapo watu wenye ulemavu wanashirikishwa, mara nyingi katika harakati za kijamii, bado nafasi za uongozi ni chache.

China, takwimu zinaonyesha kwamba kipato cha wanawake wenye ulemavu ni sawa na asilimia 42.5 ya kipato cha wastani kwa mtu bila ulemavu.

Ripoti ya Women’s World Banking inaonyesha kampeni ya taasisi ya wanawake wenye ulemavu nchini Indonesia ambayo imetoa mafunzo ya ujuzi wa fedha za kidijitali, na hivyo kuongeza fursa zao za kiuchumi.



 

Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO