Wazazi watakiwa kuvunja ukimya kwa watoto wao

 


                  NA FATMA HAMAD, PEMBA

WASAIDIZI WA SHERIA wametakiwa kuielimisha jamii kuwa na utaratibu wa kukaa na watoto wao na kuzungumza nao, waweze kujitambua, ili wajiepushe na vitendo vya udhalilishaji.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mradi wa sauti ya mwanamke Hamisa Bakari Hamad wakati akizungumza na wasaidizi wa Sheria wa wilaya ya Micheweni katika mafunzo ya Usawa wa kijinsia yaliofanyika kituo cha Uwalimu Wingwi mkoa wa Kaskazini Pemba.

Alisema katika ulimwengu wa leo wazazi waliowengi wamekosa utamaduni wa kukaa na watoto wao na kuwafundisha umuhimu wa kujitunza,na kuwa na khofu ya kujiepusha na vitendo vya udhalilishaji.

‘’Kuna watoto wamekuwa wakifanyiwa udhalilishaji lakini wanashindwa kutoa taarifa majumbani kwao, na wazazi wanashindwa kuwagudua kutokana na kukosa usubutu wa kukaa nao kjenga nao ukaribu,’’alisems.

Alisema ili kuwalinda watoto na vitendo vya udhalilishaji, ipo haja kwa wasaidizi wa Sheria kuendelea kuielimisha jamii kuvunja ukimya na kukaa na watoto wao na kuzungumza nao, ili wawe na uthubutu wa kuripoti kwa wazazi wao watakapoona viashiria vya vitendo hivyo.

Aidha kwa upande mwengine mkuu huyo aliwasisitiza wasaidizi hao wa Sheria kuzidisha bidii ya kuisaidia jamii juu ya masuala ya kisheria,ili kuona wanaondokana na kero zinazowakwaza.

Mwanaharakati wa masuala ya wanawake na watoto wilaya ya Micheweni Semeni Ali Khamis alisema sasahvi  Dunia yote ipo kiganjani kutoka na mabadiliko ya kiutandawazi,  hivyo ni wakati kwa wazazi kukaa na watoto wao na kuwafundisha jinsi ya kujitambua, kujiheshimu na kujitunza.

‘’Ulimwengu sasahivi umekua ni tofauti na zamani, hivyo ni wambie wazazi wenzangu tuvunje ukimya wala tusione aibu tuwafundishe watoto mbinu za kujiepusha na udhalilishaji,’’ alisema.

Nao wasaidizi hao wa Sheria walisema watahakikisha elimu hiyo wanaifikisha katika jamii, ili kuona matendo ya udhalilishaji yanapungua.




Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’