SARATANI YA SHINGO YA KIZAZAI ADUI MWINGINE MPYA KWA WANAWAKE, HUATHIRI MFUMO WA UZAZI
Kumbe kukosa mtoto, na magonjwa nyemelezi ni sehemu yake
NA FATMA
HAMAD, PEMBA
SARATANI ya
shingo ya kizazi ni ile ambayo, hutokana na mabadiliko ya mfumo wa chembe
chembe au seli zilizomo katika shingo ya kizazi na wingine wakiita mlango wa
kizazi.
Saratani hii huathiri shingo ya kizazi, ambayo ni sehemu ya
chini ya mfuko wa kizazi, ambapo kwa kawaida huonekana pale tu mwanamke,
anapolala chali na inaweza kuonekana kupitia uke wake.
Kwa
mujibu wa Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ inathibitisha kuwa, saratani
hii, ni ya nne kwa kuathiri wanawake, ikiwa na wagonjwa wapya 604,000 mnamo
mwaka 2020.
Takriban
asilimia 90 ya vifo 342,000 vilivyosababishwa na saratani ya shingo ya kizazi,
vilitokea katika nchi za kipato cha chini na cha kati.
Viwango
vya juu zaidi vya saratani hiyo na vifo ni kutoka Afrika, kusini mwa Jangwa la
Sahara, Amerika ya Kati na kusini Mashariki mwa Asia.
Takwimu
za WHO, zinaonesha kuwa kila mwaka Tanzania ina wagonjwa wapya wa saratani
42,000 ambapo wagonjwa hao wapya wanaofika kwenye vituo vya afya, ni takribani
15,900 tu.
Ripoti
za utafiti wa kisayansi zimeafiki kuwa saratani za shingo ya kizazi, hutokana
na maambukizi ya virusi vya 'Human Papillomavirus' au ‘HPV’
vilivyoko katika jamii ya papiloma.
VIRUSI
VYA PAPILOMA
Virusi
aina ya Human Papiloma (HPV) ni maambukizi ya kawaida ya zinaa, ambayo yanaweza
kuathiri ngozi, sehemu za siri na koo, takriban watu wote wanaofanya ngono
wataambukizwa wakati fulani wa maisha yao, kwa kawaida bila dalili.
Daktari
bingwa wa magonjwa ya wanawake na mkufunzi wa kitaifa wa saratani ya shingo ya
kizazi, Amina Jumanne Yusuph, anasema, virusi hivi huambukizwa kwa njia ya kujamiiana.
Akaeleza kuwa, kwa hivyo hawa vigumu mno
kujua uliyejamiiana naye ana maambukizi au hana, ingawa suluhu ya hilo na
kuchunguuza afya kila wakati.
“Mtu
yeyote ambaye amewahi kujamiiana, karibu asilimia 80 ya watu wote, wamewahi
kuambukizwa mara moja au mara mbili, kwasababu kinaambukizwa kutoka kwa mtu
mwenye maambukizi kwenda kwa mtu asiye na maambukizi”, anasema.
Kwamba
mwanaume anaweza akakichukua kirusi hicho kutoka kwa mwanamke mwenye nacho,
ingawa mwanaume hawezi kuugua saratani kwasababu wao hawana mlango wa kizazi.
“Mwanaume anaweza kuwa amejamiiana na
wanawake wengi, miongoni mwao, mwanamke mmoja akiwa na kirusi kuna uwezekano wa
kuwaambukiza wingine, ingawa siyo lazima wote waugue,’’anafafanua.
Hayo, aliyatanabahisha, wakati
wa mazungumzo na UN News yaliyofanyika katika hospital ya Kanda ya Bugando,
mkoani Mwanza kaskazini magharibi mwa Tanzania.
DALILI ZAKE NI ZIPI?
Sababu
za hatari zinazoweza kusababisha saratani ni pamoja na kiwango cha aina ya
‘HPV’ iitwayo ‘oncogenicity’ ya hali ya kinga mwilini, uwepo wa
magonjwa mengine ya zinaa, idadi ya kuzaa watoto, ujauzito wa kwanza katika
umri mdogo.
Anafafanua
kuwa, sababu kubwa ni kirusi aina ya ‘HPV’ ambacho iwapo ukiambukizwa na kukaa
mwilini kwa muda mrefu, kinaweza kuleta shida ya saratani, ambapo huanza
kuonesha dalili kwa muda wa miaka 10 hadi 20.
Inachukua
muda mrefu mfano, binti akianza kujamiiana akiwa na umri wa miaka 15, maana
yake mpaka kuanza kutengeneza mabadiliko ya awali.
Hii ni
kwenye mlango wake itachukua miaka 10 hadi 20, kwa hiyo binti huyu ataanza
kuonesha mabadiliko ya awali akiwa na miaka 30.
WALIOKO WENYE
HATARI
Kwa mujibu wa Dk. Amina ni watu wanaoishi na
maambukizi ya VVU, wanawake waliobeba mimba na kuzaa watoto wengi kuanzia
watano, wanawake wenye mahusiano na zaidi ya mtu mmoja, anakuwa katika hatari
ya kupata maradhi.
“Mabinti
wanaoanza kujamiiana mapema, inawaweka katika hatari kwasababu wanakuwa na muda
mrefu wa kujamiiana, lakini pia hata wale wanaoishi na maambukizi ya magonjwa
ya zinaa, nao ni hatari kubwa ya kupata ugonjwa huu,”anafafanua.
SHUHUDA
‘’Nilipata tatizo la saratani ya mlango wa
kizazi mwaka 2013, nilikua natoka maji kama mfano wa chai ya rangi, na
nikifanya tendo landoa na mwenza wangu
ilikua,’’anahadithia.
‘’Napata maumivu makali, nikakaa hali
ikaendelea kuwa mbaya nikaenda Hospitali ya Chake chake wakanipima ule uchafu
ila wakaniambia hawajajua ni kitu gani,’’anasema Sikuzani Omar ambae sio jina
lake halisi.
Aliamua kurudi tena hospitalini, ingawa
mara hiyo sasa alitakiwa kwenda hospital ya Oceacn road Tanzani bara, na kutii
agizo hilo, na kisha alikakatwa kinyama kwa uchunguuzi.
‘’Hapo nikambiwa nirudi nyumbani hadi miezi
miwili baadae, na ilipofika nilirudi na kuanza matibabu ya miozi,’’anasimulia
Sikuzani.
‘’Tokea
mwaka huo nilikua narudi Hospitali kila baada ya miezi mitatu, na nimekua
nikiendelea na dawa hadi sasa nipo vizuri, naishi na familia yangu pamoja na
mume wangu na nafanya kila ninachojiskia,’’anasema.
Mgonjwa
mwingine ambae pia hakutaka kufahamika jina lake ni kutoka Kaskazini Pemba,
alijikuta akitokwa na damu saa 24, kwa muda wa miezi sita bila ya kujua sababu.
Ingawa
baadae anasema, alikimbilia hospital ya Bugando Mwanza kwa matibabu, na sasa
anasema yuko vyema baada ya kuelezwa kuwa ilikuwa ni dalili ya saratani.
WATAALAMU WA AFYA
Daktari
bobezi wa saratani ya mlango wa kizazi kutoka Hospitali ya Lumumba Zanzibar,
Hellen Robart Makwani anasema, ugonjwa huo unaathiri kizazi, kwani mwanamke
anaweza asibebe ujauzito kabisa.
Hata
akibeba, inaweza kutoka, kutokana na mlango wake wa kizazi, kuwa hauko salama
na uimara kama ya wingine.
‘’Mama
anapopata saratani ya kizazi, hawezi kubabe mimba na ikitokea amebeba, basi
hawezi kujifungua ni lazima afanyiwe upasuaji,’’anaeleza.
Mapema
dokta Rahila Salum Omar wa Chake chake, anaeshughulikia huduma za watu wanaishi
na VVU, anasema saratani ya shingo ya kizazi, yaweza kutibika iwapo
itagundulika mapema.
Anasema,
Pap Test, Pap-smear ni kipimo, ambacho hutumika kuchunguza mabadiliko ya
chembe, zilizoko katika mlango wa kizazi wa mwanamke.
Lengo ni
kugundua mabadiliko yanayotokea katika chembe hizo, na hivyo kuwahi kuyakabili
mapema, iwezekanavyo.
‘’Kuna chanjo, kinga pekee kabla haujaanza
kujamiiana apewe, tunawataka watu waelewe chanjo, kwa hivyo mpeleke binti
akapate chanjo,”anasisitiza.
WHO,
lilitangaza kuwa kila mwezi Januari ni mwezi wa kuhamasisha jamii kuhusu
satarani ya shingo ya kizazi.
Wataalam
wa afya, katika mataifa mbalimbali ikiwemo Tanzania, wamekuwa wakitoa elimu ya
ugonjwa huo, katika jamii na kuhamasisha wanawake kujitokeza katika vituo vya
afya vinavyotoa huduma hiyo.
Ili
kupima afya zao kujua iwapo wana mabadiliko ya awali, au kudhaniwa kuwa na
saratani ya mlango wa kizazi.
Mkakati
wa WHO, ni kupunguza idadi ya wagonjwa wapya kila mwaka hadi wanne au pungufu
zaidi, kwa kila wanawake 100,000 na kuweka malengo matatu yatakayofikiwa
ifikapo mwaka 2030.



Comments
Post a Comment