ZSSF yawataka Masheha kuwaripoti wanachama waliofariki
NA FATMA HAMAD – PEMBA
MASHEHA WA MKOA WA KUSINI Pemba
wametakiwa kutoa taarifa katika Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) endapo
kutatokea kifo cha mwanachama wa mfuko
huo katika shehia zao, ili kupunguza udanganyifu hasa katika malipo ya fedha za
Serikali.
Hayo
yamesemwa na Mkuu wa Mafao kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF Zanzibar Mussa
Yussuf wakati akiwasilisha mada ya dhima ya Masheha katika utoaji wa huduma za
ZSSF katika kikao kazi kilichofanyika Tibirinzi Chakechake Pemba.
Alisema
kumekuwepo na baadhi ya watu wamekua wakipeleka taairifa za vifo vya jamaa
zao katika mfuko huo ambazo si za
ukweli, hivyo endapo watapeleka taarifa wataepusha kutokea kwa udanganyifu huo, sambamba na kuokoa fedha za Serikali.
‘’Wamekua
wakitujia watu na taarifa za jamaa zao kufariki na kudai mafao yao, lakini
tukifanya uchunguzi tunagundua kwamba sio ukweli ni uzushi,’’alisema.
Aliendelea kusema kuwa endapo Masheha watatoa taarifa na
kupeleka vielelezo sahihi vya marehemu
watasaidia warithi wake kupata mafao yao kwa haraka na kwa wakati.
Akifungua
kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Hamad Omar Bakar kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa
wa Kusini Pemba Rashid Hadid Rashid aliwataka
Masheha hao kuwa na mashirikiano
ya hali ya juu na mfuko wa Hifadhi ya Jamii, ili kufanikisha azma na
malengo ya mfuko huo.
‘’Ndugu
masheha nyinyi mnadhima kubwa katika Jamii, hivyo ni vyema mkaweka mashirikiano
na ZSSF ili kuona kila mwanachama
anapata mafao yake,’’alisisitiza.
Nao baadhi ya masheha walioshiriki mkutano huo walisema watahakikisha wanalifanyia kazi agizo hilo la kuripoti matukio ya vifo yanapotokezea shehiani mwao, ili kuepusha malalamiko kati ya wananchi na ZSSF.
‘’Tunalichkua
na Tutahakikisha mabuku tuliopewa kwa
ajili ya kuripoti matukio ya vifo
tunayatumia na tunaripoti Kwanu nyinyi
ZSSF, kwani kutamfanya kila
mwanachama aweze kupata stahiki zake,’’alieleza.
Aidha kwa
upande mwengine masheha hao waliutaka Mfuko huo wa Hifadhi ya Jamii ZSSF
kuwaingiza katika mfuko wa Pencheni ya
wazee ili nawao waweze kufaidika na matunda ya Serikali yao.
Comments
Post a Comment