Jeshi la Polisi lawataka wahisani kuisaidia familia ya wototo wenye ulemavu
NA FATMA
HAMAD – PEMBA
Jeshi
la Polisi Mkoa wa Kusini Pemba limewataka Wadau
pamoja na wahisani mbali mbali
kujitokeza kuisaidia familia ya Mohamed
Mussa yenye watoto wawili wenye ulemavu
wa viungo, iliyopo Matele wilaya ya Mkoani
Pemba mahitaji muhimu ikiwemo makaazi
pamoja na viti mwendo.
Wito huo umetolewa na Mratibu wa
Polisi jamii wa mkoa wa Kusini
Pemba Makame Nasibu Silima kwa niaba ya Kamanda wa Polisi wa
Mkoa huo, Abdla Hussein Mussa, mara baada
ya kukabidhi msaaada wa vyakula na godoro,
ikiwa ni shamra shamra ya kuelekea madhimisho ya siku 16
za kupinga ukatili
wa kijinsia.
Alisema mazingira
ya familia hiyo ni duni, hivyo ni vyema wadau pamoja na wahisani kujitokeza
kuisaidia familia hiyo ili iweze kuishi katika hali ya furaha kama binadamu
wengine.
‘’Kutokana
na halingumu ya kimaisha inayoikumba familia hiyo, tumeamua kuwapa msaada wa vyakula pamoja na magodoro ili vieze
kuwasaidia,’’alisema
Mapema mkuu wa mtandao wa Polisi wanawake mkoa wa Kusini Pemba (TPF NET ) Habiba Ali Said amesema baada ya kuona tarifa ya familia hiyo ambayo inakukumbwa na ugumu wa maisha kupitia kwenye mitandao ya kijamii, wameamua kuja kuifariji familia hiyo.
‘’Baada ya
kuona tarifa hiyo imetugusa na tumeamua kujakuifariji familia hiyo kwa kidogo
chetu mungu alichotujaalia,’’alisema.
Alisema
katika kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia wamekua wakitoa
misaada mbali mbali kwa familia zinazoishi katika mazingira magumu, waliopatwa
na maafa pamoja waliopatwa na udhalilishaji.
Kwa upande wake baba mzazi wa watoto hao wenye ulemavu Muhammed Mussa, alisema wanashindwa kusoma Skuli kutokana na kukosa Vigari vya maringimawili kwa ajili ya kutembelea.
‘’Hawasomi
Skuli wala Mdrasa, kwani ni mbali hawana
vigari, na mimi sina uwezo wa kununua,’’alisema baba mzazi.
Wakitoa
shukrani zao mara baada ya kupokea msaadahuo wanafamilia hao, wamelipongeza Jeshi la Polisi kwa kuwapatia
msaada, huku wakiwataka na wengine wenye nia ya kutoa kuekeza sadaka yao kwa familia hiyo, ili waweze kupata mahitaji
muhimu ambayo yatawasaidia watoto hao.
Comments
Post a Comment