KUKOSEKANA KWA MTANDAO KWA SABABISHA HASARA KWA WAFANYA BIASHARA
|
NA NIHIFADHI ABDULLAH UNGUJA Kukosekana kwa mtandao kumesababisha hasara ya kutoingiza kipato kwa watu ambao shughuli zao zinategemea huduma hiyo kwa kiasi kikubwa Wakizungumza na kati fm kwa nyakati tofauti wafanyakazi wanaotoa huduma ya intanet na waandishi wa habari wa mitandao wamesema hali hiyo imewarejesha nyuma kwani walishindwa kufanya kazi. Waandishi wa habari Hassan Mselem na Amina Masoud wamesema kutokana na dunia ilipo kuzimwa au kukosekana huduma ya inteneti inapelekea hasara sio tu kwao bali hata kwa wananchi kutopata habari kwa wakati muafaka Nae Juma Marijani amesema ameamua kujiajiri kwa kuekeza kutoa huduma za intanet hivyo inapokesakana kunarejesha nyuma nguvu za kujikwamua kiuchumi Sambamba na hayo ametoa wito kwa serikali kutatua vikwazo katika masuala ya mtandao ili kwenda sambamba na ulimwengu ulipo |

Comments
Post a Comment