SALIM HAMAD,PEMBA
BAADA ya kufanikiwa kutinga katika fainali ya Michuano ya
Mawizara (Wizara Cup) Nahodha wa timu ya Wizara ya Afya Abdul Karim Abdi
Heri ameapa kuwa watabeba ubingwa katika michuano hiyo.
Akizungumza na Mwanaspoti mara baada ya kufanikiwa kutinga
kwenye hatua hiyo kwa kuichapa timu ya Shirika la Umeme ‘’Zeco’’ mabao
2-0 katika mchezo wa Nusu Fainali uliopigwa Uwanja wa Gombani, Nahodha
huyo alisema ushindi huo umewapa asilimia kubwa ya kufanya vizuri kwenye
Fainali ya mashindano hayo.
Alisema haikuwa kazi rahisi kuweza kuwafunga wapinzani wao
kutokana na wao kutafuta nafasi ya kuwania kucheza fainali ya Mashindano hayo
ili waweze kubeba ubigwa kwamara ya kwanza tokea kuanzishwa kwa mashindano
hayo.
Alisema katika mchezo huo walipambana na kuonesha umahiri
mkubwa kwa kushinda mchezo huo uliokuwa mgumu kwenye hatua hiyo iliyo kuwa
inawaniwa na wapinzani wao.
‘’Sisi tumejipanga sana katika mashindano hayo licha kuwa ni
magumu lakini tunaahidi washabiki wetu kwamba tutabeba taji la mashindano hayo
kwa mara ya kwanza’’alisema .
Hata hivyo alisema kutokana na uwezo mkubwa walionesha
kwenye mchezo huo anaamini kwa kiasi kikubwa wateweza kufanya
Vyema ili kutwaa kombe la michuano hiyo.
Akizungumzia muendelelezo wa Michuano hiyo Msemaji wa timu hiyo
Hassan Said alisema michuano hiyo imekuwa na msisimko kama michuano ya ligi
daraja la kwanza taifa iliyomalizika hivi karibuni.
Comments
Post a Comment