KIJANA OMAR ALI HAJI ATUPWA RUMANDE KWA KUTISHIA AMANI.
Mahakama ya
Mkoa C Chake chake imemsokomeza rumande kijana Omar Ali Haji mwenye umri wa miaka 18 mkaazi wa junda miti kiwani akidaiwa
kutishia amani, baada ya
kushindwa kutimiza masharti ya zamana aliyopewa na mahakama hiyo.
Hakimu wa
mahakama hiyo Rashid M Magendo amesema kijana huyo ataendlea kusota rumande hadi tarehe 30/ mwezi huu kwa ajili ya
kusikilizwa, huku akiwa na wadhamini wake wawili [2] na shilling laki tatu [30000],
kwa ajili ya kupewa dhamana yake.
Mtuhumiwa huyo wakati yupo kizimbani na kusubiri asomewe shitaka lake
mwendesha mashtaka wa Serikali kutoka
ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka DPP Mohd Said Mohd amesema sena pingamizi nimekubaliana
na uawamuzi huo.
Imedaiwa
kuwa siku ya tarehe 23/ 7/ mwaka huu majira ya sa moja na nusu asubuhi huko Junda miti Kiwani wilaya ya Mkoani Pemba ulimshambulia
kwa hatari Khamis Juma Ali kwa kumkata na Panga katika sehemu zake za mkononi
na kusababisha kupata maumivu makali katika sehemu hizo jambo ambalo ni kosa
kisheria kifungu cha 204 [a] sheria nambari 6/ 2018 sheria ya Zanzibar.
Comments
Post a Comment