Aendelea kusota Rumande kwa tuhuma za Ubakaji
Mtuhumiwa Bakar Mbwana
Juma mwenye umri wa miaka 32 mkaazi wa Jomvu Kengeja anaekabiliwa na shitaka la
Kumtorosha na Kumbaka msichana mwenye umri wa 17 ameiambia mahakama ya Mkoa
Chake Chake kuwa yeye hahusiki na tukio hilo kwani muda uliotajwa kutenda kosa
hilo alikua kwenye kibanda akinywa kahawa.
Aliambia mahakama hiyo
kuwa yeye ni mfanya kazi wa ujenzi wa nyumba hivyo anakawaida ya kurudi
kazini baina ya saa moja hadi saa moja
na nusu za usiku na mara zote hufikia kwenye mkahawa kabla ya kwenda anakoishi.
Alidai kuwa siku ambayo
alituhumiwa kufanya tukio hilo alirudi kazini majira ya moja za usiku na
kifikia mgahawani na kupata kahawa akiwa yeye na marafiki zake.
Alifahamisha kuwa baada
ya kunywa kahawa alirudi nyumbani na kuigia chooni kwa ajili kujiandaa na sala
ya Isha na kisha kwenda msikitini.
‘’Nashangaa sana wakati huo wa saa mbili
nitatorosha saa ngapi na nitabaka saa ngapi hilo haliwezekani’’ Alidai
mtuhumiwa huyo.
Alidai kuwa kabla ya
kutokea kwa tukio hilo walikuwa na ugomvi kati yake na kaka wa anaedaiwa
kumfanyia udhalilishaji.
Wakili wa mtuhumiwa huyo
Abeid Mussa ameiomba mahakama hiyo kulipangia
siku nyengine shauri hilo kwa vile bado yuko shahidi mwengine wa utetezi.
‘’Mheshimiwa naomba ighairishe na uipange siku
nyengine kwa ajili ua kusikiliza shahidi mwengine’’ Alidaiwakili .
Baada ya mtuhumiwa huyo
kupanda kizimbani akisubiri taratibu za Mahakama ndipo mwendesha mashtaka
kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka DPP Juma Ali Juma alidai kuwa shauri
hili lipo kwa ajili ya utetezi.
‘’Mheshimiwa hakimu
shauri hili lipo kwa ajili ya ushahidi na kwa upande wetu hatunashaka na
hilo’’, alidai mwendesha mashtaka huyo.
Hakimu wa mahkama hiyo
Lusiano Makoe Nyengo alikubaliana na upande wa mashtaka na kumtaka mtuhumiwa
huyo ajitetee.
Ilidaiwa mahakamani hapo
mtuhumiwa huyo kosa la kwanza alitenda tarehe 2/6/2020 bila ya halali na bila
ya ridhaa ya wazazi wake alimtorosha msichana wa miaka 17 kutoka nyumbani kwao
na kumpeleka nyumbani anakoishi .
Kufanya hivyo ni
kosa kinyume na kifungu cha 113[1] [a] cha sheria nambari 6 ya
mwaka 2018 sheria ya Zanzibar .
Kosa la pili
alitenda siku hiyo hiyo majira ya sa 2; 00 za usiku katika kijiji cha Kengeja
wilaya Mkoani Mkoa wa Kusini Pemba.
Ilidaiwa kuwa bila ya
halali na bila ya ridhaa ya wazazi wake alimbaka msichana huyo wa miaka 17
ambapo kufanya hivyo ni kosa kisheria kifungu cha 108[1] [2] [e] na 109 [1]
sheria ya adhabu sheria nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.
Shauri hilo
litasikilizwa tena mahakamani hapo tarehe 12/10/2020 kwa ajili ya kusikilizwa
shahidi mwengine.
.
Comments
Post a Comment