RUSHWA BADO NI JINAMIZI LINALOWAKUMBA WANAWAKE

 


 NA FATMA HAMAD, PEMBA

KUWEPO KWA rushwa ya pesa imetajwa kwamba ni moja ya sababu inayowakosesha wanawake wanaogombea nafasi za uongozi kushindwa kuyakamata majimbo.

Hayo yamesema na baadhi ya viongozi wa vyama  vya siasa na wanaharakati wa wanawake na watoto wakati wakiwa katika kikao cha tathmini juu ya Mradi wa SWIL, kilichofanyika Ofisi Tamwa  Chakechake Pemba.

Walisema licha ya mikakati mbalimbali inayochukuliwa na serikali na wadau wengine kuona wanawake wanashika nafasi za uongozi, bado  kunachangamoto ya rushwa ambayo inapelekea wanawake kushindwa na kupelekea wenye pesa zao kuyahodhi majimbo.

Walisema katika uchaguzi uliopita wa 2025 wanawake walionekana kujitokeza kwa wingi kugombea,lakini kwenye majimbo walirudi ni kidogo.

‘’Jamani tuseme ukweli uchaguzi sasahivi umekua kama ni biashara, kama huna pesa basi huwezi kufanikiwa , wanarudi majimboni walewale viongozi wa zamani ama wenye pesa zao,’’wanasema.

Mapema Salma Omar  kutoka chama cha Wanasheria wanawake Zanziba (Zafela) anasema ili kupunguza malalamiko hayo ipo haja kuwekwa sheria  itakayomlinda mtoa taarifa, sambamba na kuwekwa kwa dawati maalumu la upokeaji wa taarifa za vitendo vya rushwa wakati inapofika  kipindi cha chaguzi.

‘’Ifike wakati na sisi Zanzibar tuwe na sheria itakayo mlinda mtoa taarifa ya vitendo vya rushwa, kwani itasaidia kupunguza rushwa na wanawake wanyonge wapate nafasi,’alisema.

Kwa upande wake Afisa kutoka Ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali Hadid Rashid Hadid alisema kwa mujibu wa tafiti mbalimbali ambazo wamekua wakizifanya zimeonesha kwamba familia ambazo zinaongozwa na wanawake, ama wanawake wanashirikishwa juu ya mambo yao, zinakua ziko juu kimaendeleo.

‘’Niseme wanawake wakiondoshewa vikwazo na wakapata nafasi wanafanya viruzi, mfano tafiti tunazo zifanya tunagundua kwamba familia ambazo wanawake wanakua na maamuzi zinamaendeleo,’’alifahamisha.

Sabah Ali Mzee Mkurugenzi mtendaji wa Jumuia ya wanawake wenye ulemavu upande wa Unguja (JUWAUZ) alisema lengo la mradi wa Swil ni kuja kuwakomboa wanawake wote waondokane na vizigiti mbalimbali ambavyo vitawazuia kuingia katika maamuzi.

‘’Tunawasaidia vikundi vya wanawake hasa wenye ulemavu kuona wanafanya shughuli zinazowaingizia kipato kitakachowasaidia kuingia kwenye kinya’nganyiro cha uchaguzi,’’alisema.

Mkurugenzi wa Chama cha Wandishi wa Habari wanawake TAMWA Zanzibar Nairat Ali alisema katika Uchaguzi uliopita ilionekana idadi ya wanawake na hasa wenye ulemavu walijitokeza kwa wingi ukilinganisha na miaka ya nyuma.

‘’Tumeona Uchaguzi uliopita wanawake walijitokeza wengi, na ni mara ya kwanza kujitokeza mgombea Uraisi mwanamke, hivyo japo kuna changamo, bado tuendeleeni kutetea, ili kuona lile tunalolitaka la hamsini kwa hamsini katika uongozi limefikiwa,’’alishauri.

Nae Afisa Programu kutoka Tamwa Zanzibar Sabrina Yussuf Mwintanga alisema lengo la mradi wa SWIL ni kuwawezesha wanawake hata walioko vijijini kuhakikisha wanashirika katika harakati za uchaguzi, na kuingia kwenye maamuzi.

Alisema SWIL imeanza kuzaa kuleta mabadiliko kwani, katika serikali ya awamu ya nane, imeonekana idadi ya madiwani wanawake imeongezeka kwani ni 27 ukilinganisha na kipindi kilichopita, ilikua ni 25 kwa Zanzibar.

MWISHO.

 

 

 


Comments

Popular posts from this blog

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

HOFU YA UDHALILISHAJI MTANDAONI INAVYOWANYAMAZISHA WANAWAKE

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI