TAMWA YAWAFUMBUA MACHO WANAWAKE, WANAWAKE VIJANA NA WANAWAKE WENYE ULEMAVU

 

NA FATMA HAMAD, PEMBA

CHAMA CHA Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania, Zanzibar (TAMWA ZANZIBAR ), kimezindua mradi wa Wanawake Viongozi kwa ajili Usawa, Uwajibikaji na  Demokrasia( W-LEAD) unaolenga kuimarisha nafasi za uongozi na ushiriki wa wanawake, hususan wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu, katika mifumo ya kidemokrasia na kushika nafasi mbalimbali za maamuzi.

Akizungumza katika uzinduzi huo kwa wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu  katika ukumbi wa Ofisi za Tamwa Mkanjuni Chakechake Pemba,  Afisa Tathmini na ufatiliaji Mohammed Khatib Mohammed alisema mradi huo utaimarisha uongozi wa wanawake , wanawake wenye ulemavu na wanawake  vijana Zanzibar.

Alisema kwa  mujibu wa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 wanawake wako  asilimia 51 ambao ni wengi ulkilinganisha na wanaume,  lakini katika nafasi za uongozi wanawake  ni asilimia 38 tu  idadi ambayo bado haijaridhisha ipasavyo.

Alisema kwa sasa Zanzibar idadi ya wanawake viongozi ni ndogo kwani ni  asilimia 38 tu ukilinganisha na wanaume.

‘’ Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 inaonesha wanawake wako wengi ni asilimia 51, hivyo Tamwa tumekuja , na mradi huo kuona wanawake, wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu wanahamasika kushiriki na kushika nafasi mbalimbali za uongozi,’’alisema.

Alisema kwamba miaka ya zamani Zanzibar ilikua imetawaliwa na mfume dume, hivyo kufuatia mradi huo utahakikisha  inaondoa mawazo  mgando kwa wanawake na wanajamii  juu ya mfumo huo.

Aliendelea kusema kuwa  Tanzania na Zanzibar zimeridhia kuendeleza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake, hivyo  mradi utasaidia kufikiwa kwa lengo la asilimia ya 50 kwa 50 katika maamuzi.

‘Baada ya mafunzo hayo wanawake vijana 60 wataunganishwa na taasisi mbalimbali za umma, sekta binafsi na asasi za kiraia kwa ajili ya kujifunza kwa vitendo masuala ya uongozi, wajiamini na kujiandaa kuchukua nafasi za uongozi, ili kufikiwa kwa lengo hilo la 50 kwa 50 katika uongozi,’alisema.

Kwa upande wa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kutoka TAMWA Zanzibar  Sofia Ngalapi alisema  lengo hasa  ni kuwawezesha wanawake,  wanawake vijana na wanawake wenye ulemavu, kwa kuwajengea uwezo ili waweze  wajiamini  na  kushiriki kikamilifu katika mifumo ya kidemokrasia na nafasi za maamuzi  huku wakiongeza   ajira kwa vijana.

Alisema Zaidi ya wananchi 100,000 wanatarajiwa kunufaika na mradi huo, huku watetezi wa haki za wanawake 60 wakijengewa uwezo wa kufuatilia,kuripoti na kushughulikia vitendo vya ukatili kwa wanawake.

Nae Afisa kutoka kituo cha Utafiti na Uchambuzi wa sera za kijamii Zanzibar Mohamed Salum Ali amewataka wanawake kuhakikisha wanajitokeza kugombania nafasi mbalimbali za uongozi, ili kuleta mabadiliko katika jamii zao.

Mradi huo wa kuimarisha uongozi wa wanawake Vijana Zanzibar ( W-LEAD ) unatekelezwa na TAMWA Zanzibar kwa ushirikiano na Jumuia ya wasiona (ZANAB), chuo kikuu cha  Taifa cha  Zanzibar (suza) na Zanzibar Univesity (ZU)  chini ya ufadhili wa   Umoja wa Ulaya kupitia mpango wa Ushiriki wa wanawake na Vijana katika Demokrasia na kuanza  utatekelezwa wake  kuanzia mwaka huu  2026 hadi 2027.

Kauli mbiu ya mradi huo  ni  Kujenga Zanzibar ambayo wanawake na wanaume wanashiriki kwa usawa katika kuunda na kuendeleza jamii zenye demokrasia na ujumuishi kwa wote.

MWISHO.


Comments

Popular posts from this blog

WANDISHI WA HABARI ANDIKENI HABARI ZA UCHAMBUZI

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI