SERIKALI YAAHIDI KUWEKA MAZINGIRA RAFIKI KWA MTOTO
NA FATMA HAMAD, PEMBA
Naibu
waziri huyo ameyasema hayo wakati
akifungua Kongamano la Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afirika
lililofanyika Viwanja vya kufurahishia watoto Tibirinzi Chkachake mkoa wa
Kusini Pemba.
Alisema
kila Mtoto anastahiki kupata haki muhimu kama vile kulindwa, kuishi, kushiriki
katika shughuli na kuwendelezwa, hivyo ni jukumu la kila mtu kuona haachwi
mtoto nyuma hasa katika fursa za maendeleo.
Aidha aliisisitiza
serikali kuhakikisha sera,Sheria, Bajeti
zinazingatia na kulinda masuala ya mtoto
na kudhibiti haki zao.
Mapema Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Hafidhi Ali
Mohamed alisema siku hii ya Mtoto wa Afrika inatoa fursa ya kujadili ni namna
gani watoto wataishi bila ya udhalilishaji, na kupata haki zao za msingi.
‘’Ndugu mgeni rasmi sikuhii inatufanya tujadili
ni kwa kiasi gani tunaweza kuwalinda watoto dhidi ya ukatili, na kuishi kwa
Amani,’’alisema.
Mkurugenzi wa wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia
Wazee na Watoto Siti Abass Ali alisema Serikali ya Mapinduzi itahakikisha inashirikiana
na watoto, na kwa mwaka huu wa 2026/2027 imetenga bajeti maalumu kwa ajili ya
masuala ya watoto.
Akitoa salamu kwa niaba ya Watoto wa Zanzibar
Mwenyekiti wa Baraza la Watoto Taifa Khamis Abdalah Mbarouk, aliipongeza
serikali pamoja na wadau wengine kuweka siku hii maalumu ya kuwaunganisha
watoto wote, na kupewa somo ni namna gani kufahamu udhalilishaji na kujua
wajibu wao pamoja na haki zao stahiki.
Kila
mwaka tarehe 16 Juni, nchi za Afrika huwa zinaadhimisha Siku ya Mtoto wa
Afrika, ambapo Siku hii ilianzishwa na Baraza la Wakuu wa Nchi na Serikali wa
Umoja wa Afrika mwaka 1991.


Comments
Post a Comment