
NA FATMA HAMAD,
PEMBA
Wandishi wa Habari
wametakiwa kuzitumia Tafiti wakati
wanapoandika habari zao, ili kuibua changamoto zinazoikabili jamii na
kupatikana kwa ufumbuzi wa jambo husika.
Ushauri huo umetolewa na commissiona wa ufuatiliaji na tathmini kutoka
Tume ya Mipango Zanzibar zuhura Mohd Abdallah kwa niaba ya katibu mtendaji
wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa
waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari, yaliyofanyika ZRA Gombani Chakechake mkoa wa Kusini pemba.
Alisema wandishi wa Habari wanasauti kubwa katika jamii, hivyo,
endapo watazitumia tafiti mbalimbali zinazofanywa wakati wakiandika habari zao,
wataibua matatizo yanayowakumba wanajamii na kufanyiwa kazi kusaidia kupatikana kwa
maendeleo Nchini
Aidha alisema Tume ya
mipango Zanziba imeona ipo haja kutoa
mafunzo hayo ya utafiti kwa Wandishi wa habari kwani kutawaongezea uwelewa wa
kufahamu mbinu za
uandishi wa habari za uchambuzi, zilizofanyiwa utafiti kwa
manufaa ya jamii na taifa
‘’Wandishi wa Habari ni
watu muhimu katika jamii, hivyo endapo mtazitumia na kuzichambua tafiti jamii
ikazielewa na kuzifazifanyia kazi watatatua
changamoto zinazo wakabili kwa asilimia kubwa,’’alisema.
Mapema Mhadhir kutoka
chuuo kikuu cha Dar- es - salaam Egbert
Mkoko na alisema kuwa habari za utafiti zina nafasi kubwa katika kuibua ukweli
na kufichua kero zilizojificha zilizojificha katika jamii.
‘’Wandishi wa Habari wasiogope kuzitumia tafiti kwani
wataisaidia jamii kuondokana na shida ambao zimewakabili vijijini
mwao,’’alishauri.
Kwa upande wake Mtaalamu wa masuala ya kihabari kutoka Zanziba Ali Sultan alisema bado
Wandishi wa habari hawajajikita zaidi kuandika habari za utafiti, hivyo ni budi
kwa mazingira ya sasa kuacha kuandika habari kimazoea, wazitumie tafiti ili
wawe mkombozi katika jamii.
Nao baadhi ya waandishi walioshiriki
katika mafunzo hayo walisema ni jambo lafaraja kuona tume hiyo imeona umuhimu
wakutoa mafunzo hayo ambayo
Yatawawezesha waandishi wa habari kufanya shughuli zao kwa
ufanisi Zaidi.
MWISHO
Comments
Post a Comment