Kiungoni walia na huduma ya Maji

NA FATMA HAMAD, PEMBA

WANACHI WA SHEHIA ya Kiuongoni wilaya ya Wete Kaskazini Pemba  wamelalamikia juu ya kadhiya inayowakabili, ya  ukosefu wa huduma za Maji safi na salama kijijini mwao.

Wananchi hao walisema tokea ulipoanza ujenzi wa barabara suala la Maji  ya Zawa  vijijini  mwao imekua ni kama ndoto, jambo linalopelekea usumbufu wa kutafuta huduma hiyo maeneo ya mbali.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi  huko kijijini kwao, kiungoni mwananchi Zainab Abdallah Hassan na Ngindo Kombo Faki  walisema  wanategemea huduma ya maji kupitia Kisima cha Msikitini, ambapo kupandishwa  kwake kwenye Tenki ni nadra, kwani hadi wananchi walipie pesa ndio yapandiswhe.

  ‘’ Hayo maji tunayotegemea hapo msikitini hayapatikani kama wananchi hawajachanga pesa, hivyo kupatikana kwake ni shida,’ walisema.

Walisema kuwa tatizo hilo limeshakua kubwa na linahitaji kuwangaliwa, kwani wakati mwengine wanashindwa kupata Maji hata ya kufanya usafi majumbani mwao sambamba na kufulia nguo za watoto wao.

‘’Kwakweli tunashida kubwa watu wa kiungoni mana inabidi tununue maji dumu shilingi miambili jee kweli hii ni hali tutaishi vipi sisi majumbani na watoto,’’walisema.

Kwa upande wao Time Salim Hamad  na Said Hamad Ali  walisema kukosekana kwa maji kumeathiri harakati za maendeleo ya wanakijiji wa Kiungoni, kwani wanashindwa kufanya shughuli za kilimo na kuzalisha mazao ambayo yangeweza kuinua uchumi wao.

‘’Suala la kukosa huduma ya maji kijijini kwetu limetuathiri, kwani tunashindwa kupanda hata mboga tukapata chakula kwani hazikubali zinakufa kutokana na kukosa maji,’’walisema

Walisema mbali ya hilo pia wanaathirika kukosa maji ya zawa kwani, wanawagonjwa pamoja na wenye ulemavu ambapo maji ya kununua ni tatizo, wanashindwa kupata maji ya kutosha majumbani mwao.

 ‘’Tunawaomba watendaji wa Mamlaka ya Maji itufanyie utaratibu juu ya suala hili, ukiangalia sasahivi ni kipindi cha Ramadhani bila kuepo kwa huduma ya maji kijijini mwao wanaathirika,’’walisema.

Sheha wa Kiuongoni Omar Khamis Othman alikiri kuepo kwa tatizo hilo la huduma ya Maji kijijini humo.

‘’Ni ukweli uliowazi kwamba baada ya tu ya kuanza kwa ujenzi wa barabara huduma ya Maji Safi ilikosekana kijijini hapo, na hii ni kutokana na kukatwa kwa miundombinu ya mabomba yanayosambaza Maji katika maeneo hayo,’’alisema.

Afisa mdhamini wizara ya Maji Nishati  na Madini Injinia Suleiman Hamad Omar alisema suala la kukosekana kwa huduma ya maji kijijini hapo limekuja baada ya utengenezaji wa barabara.

Alisema ni vyema wananchi kuendelea kuwa na subra, kwani ujenzi utakapomalizika na huduma itarejea kama awali bila ya shida yoyote.

MWISHO.

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’

UROHO WA MALI KWA WANAUME UNAVYONYIMA WANAWAKE ARDHI