Wanawake wenye ulemavu ambao waligombea na kukosa waomba kuangaliwa
NA FATMA
HAMAD, PEMBA
WANAWAKE Wenye
Ulemavu kisiwani Pemba ambao waliingia kwenye kinyan’ganyiro kugombea, katika Uchaguzi mkuu 2025, wamemtaka Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hussein Ali Mwinyi kuwangalia kwa jichola
huruma kwa kuwapa nafasi mbalimbali, ili walete mabadiliko kwa Taifa na kwa wenzao
wenye Ulemavu.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi huko
nyumbani kwao Katija Mbarouk Ali mwenye Ulemavu wa Viungo ambae aligombea
Uwakilishi Jimbo la Kojani ingawa hakufanikiwa, alisema wamekua wakiingia
kwenye kinyan’ganyiro ili kuona nawao wanaingia kwenye maamuzi.
Alisema
wakati kunapokuepo na nafasi za uteuzi kuwapa kipaombele wale ambao
walijitokeza kugombea, ili kuwatia hamasa na moyo wa kuingia kwenye
kinyan’ganyiro kwa wanawake hao wenye Ulemavu.
‘’Tumejitoa
tumedharauliwa kwa sababbu tunapambana na watu wenye pesa na vyeo vyao, hivyo
ipo haja Rais utuone, ili kufuta nguvu zetu ambazo tumezipoteza,’’alisema.
Alisema
watuWenye Ulemavu maranyingi wamekua wakisahauliwa katika fursa mabalimbali
ambazo zimekua zikitokezea, hivyo ipo haja serikali kuwaona ili wafaidike na
fursa hizo ambazo zimo katika serikali yao.
Halima Suleiman Ali mkazi wa
Mtambile aliejitosa kuania udiwani Wadi ya Mtambile alisema wakati wa wanawake
wenye ulemavu kuwekwa nyuma katika fursa za maamuzi umepitwa na muda, hivyo ni wakati kupewa
nafasi, hivyo ni vyema kupewa nafasi ili kuonesha uthubutu na uwezo walionao wa
kutumikia taifa lao.
‘’Wanawake wenyeulemavu
hatutaki tena kuekwa nyuma, tunaomba tuangaliwe hususani wale ambao tumeonesha
uthubutu wetu tokea kwenye Uchaguzi Mkuu,’’alisema.
Nasra Fakih Hassan mwenye ulemavu
wa viungo mzaliwa wa Kangagani Wete
Pemba , ambaye alijitosa kugombea nafasi ya uwakilishi viti maalumu kupitia
Chama cha Mapinduzi (CCM) alisema katika
nafasi za wanawake za Wilaya na za mkoa kuhakikisha watu wenyeulemavu
wanazipata nafasi hizo.
‘’Makundi yote ikiwemo Vijana, Wanawake kila mkoa na
wilaya zinakua ni mbili mbli, iweje kundi la watu wenye ulemavu iwe ni nafasi
moja mkoa mzima ama Pemba mzima, tunaomba tuangaliwe tuwemo kila
sehemu,’alisema.
Mratib wa Jumuia
ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA) Pemba Juma Kombo Hija, aliema
katika Uchaguzi wa 2025, Wanawake Wenye Ulemavu walihamasika kuingia kwa wingi
majimboni kuania uongozi ikiwa walikua ni 12, kwa Pemba pee ambapo haijawahi
kutokea kwa chaguzi zilizopita.
Alisema ni vyema serikali kuwatupia jichowanawake hao
ambao walionesha uthubutu wao kwa kuwapatia nafasi waweze kufikisha mchango wao
katika serikali yao, sambamba na kutoa hamasa kwa wanawake wenzao wenyeulemavu
wa kushiriki harakati za kimaendele, zilizomo katika Taifa lao.
Kaimu Mratibu wa Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake
Tanzania TAMWA Zanziba Ofisi ya Pemba
Amina Ahmed Mohamed alisema wamekua wakifanya jitihada mbali mbali, kuona wanawake wenyeulemavu wanaingia
katika nafasi za maamuzi.
‘’Huu ni mwaka wa mabadiliko tumechoka kuona wanawake
wenye ulemavu wakitazamwa kama wakulima, tunatamani kuona wanaigia kila
sehemu,’’alisema.
Nao baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa akiwemo Hamad
Rashid Mohamed wa chama cha Alliance for Democratic
Change (ADC) Maryam Saleh
Juma kutoka chama cha Ukombozi wa Umma (Chauma)
walisema wanawake wenye ulemavu wanamchango mkubw, hivyo ipo haja kupewa
kipaombele na kuona wanashiriki kwa wingi katika nafasi mbali mbali za maamuzi.
Sheria ya watu enye ulemavu namba 8 ya mwaka 2022, kifungu cha
29 kinaeleza, umuhimu wa watu wenye ulemavu kufikia miundombinu pamoja na
taarifa, mawasiliano na haki zote za kibinadamu.
Katika programu za uchumi nchini Tanzania, hata pale ambapo watu
wenye ulemavu wanashirikishwa, mara nyingi katika harakati za kijamii, bado
nafasi za uongozi ni chache.
Comments
Post a Comment