WAFANYA BIASHARA TIBIRINZI WAMKABIDHI CHANGAMO ZAO MGOMBEA URAISI WA UDP

 


NA FATMA HAMAD, PEMBA
WAFANYABIAshara wa soko la Tibirinzi Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba wamemtaka  Mgombea Urais  wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa tiketi ya chama cha United Demokratik Pati UDP, Saumu Hussein Rashid wakati atakapoingia madarakani kuwapunguzia Kodi.

Wakizungumza na mgombea huyo baadhi ya wafanyabiashara hao akiwemo Kassim Kishuka, baada ya kuwatembelea katika biashara zao, walisema bei za vyakula ziko juu kutokana na ushuru mkubwa wanaotozwa, hivyo wamemtaka kulipa kipaumbele suala la kodi, ili bidhaa ziweze kushuka bei.

‘’Kwakweli bidhaa zimepanda bei mno, na hili ni kutokana na ushurumkubwa wa kodi, wafanyabiashara wenzetu wanashindwa kufanya  biashara, hivyo tunaomba suala la kodi uliangalie kwa hali ya juu pindi ukipata ridhaa ya kushika nafasi  hiyo.

Walisema uchumi wa wananchi wa Pemba ni mdogo, hivyo endapo suala la kodi kama halitoangaliwa, bidhaa zitaendelea kupanda bei na kupatikana kwa mlo mmoja, jambo litalopelekea tatizo la udumavu kwa wakaazi wa kisiwa hicho.

Aidha kwa upande wao Mohammed Juma Rehan na Omar  Mgando wamemtaka mgombea huyo kuhakikisha anawajengea soko la kisasa na lenye hadhi, ili wapate sehemu salama ya kufanyia biashara zao.

Walisema wamekua wakilipa kodi, lakini eneyo ambalo wanakaa na kufanyia biashara zao sio rafiki, kwani hata inaponyesha mvuainabidi wahame na kutafuta pahala pengine pa kujificha.

‘’Bado hatujakua na soko, unaona hapa tupo uwanjani na samaki wetu, sio mazingira rafiki kwetu, jee ikitokezea mvua unafkiri tunahangaika kiasi gani, tunaambiwa tukaingia ndani ya soko juu jee samaki tutauzaje uko juu gorofani, walisema.

Sambamba na hilo walisema wanahitaji kujengewa soko kubwa na lenye hadhi, wafanyabiashara wa aina zote wauze bidhaa zao humo, ili kuona bidhaa zote zinapatikana.

‘’Tutakapopata soko kubwa na kila bidhaa ikawepo hapa, wananchi watanunua vitu vyote humu, na sio nazi anunue hapa, samaki akanunue machomane,’’hiyo ni shida.

Nae Katibu wa wafanyabiashara wa Tibirinzi alisema atahakikisha wanampa kura za ndio kwa kwani ameonesha mwelekeo mzuri wa kuja kuwatatulia kero zao.

‘’Toka kampeni zilipoanza hatujawahi kumuona mgombea yoyote kuja na kutusikiliza shida zetu, wewe ndo wa mwanzo hivyo tunahakikisha tunakunga mkono wewe mwanamke kwani ulishaonesha mwelekeo mzuri kwetu,’’alisema.

Nae Mgombea huyo wa Urais Saum Hussein Rashid alisema lengo la kuwatembelea wajasiriamali hao ni kusikiliza changamoto ambazo zimekua zimekuwa zikiwakabili, aweze kuzifahamu, ili aje kuzitatua pindi akipata ridhaa.

Alisema sera ya Chama chao ni kuwainua wanchi kiuchumi, hivyo watahakikisha wanazitatua kero zinazowakwaza, ikiwemo kodi, na kuwapatia mitaji, waendeleze biashara zao, waweze kukuza kipato chao.

‘’Sisi sera yetu ni kuinua kipato cha wananchi, hivyo tutahakikisha kodi imepungua, na tutawapa mitaji wafanyabiashara waendeleze biashara zao, na wajiinue kiuchumi na kuondokana na umaskini,’’alieleza.

Aidha alisema kipaumbele chengine ni kuweka kiwanda kikubwa cha usindikaji wa Samaki, kuona soko linaimarika ndani na nje ya nchi, sambamba na kupatikana kwa kitoeleo cha kutosha.

Mgombea huyo aliwasili kisiwani Pemba leo asubuhi, ambapo mbali ya kuwatembelea wajasiriamali hao alitembelea kaburi la aliekuwa Makamo wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Omar Ali Juma, na kuifariji familia yake.




Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO