UMGOMBEA URAIS WA MUUNGANO WA UDP AAHIDI NEEMA LUKUKI KWA WAPEMBA
NA FATMA
HAMAD, PEMBA
MGOMBEA
URAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Tiketi ya Chama cha United
Demokratik Pati UDP Saum Hussein Rashid amesema endapo atachaguliwa na kupata
ridhaa ya kuongoza atahakikisha anaboresha miundombinu ya afya, ili kuona
huduma zote zinapatikana bure, ikiwemo huduma za mama na mtoto.
Mgombea
huyo aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi na wanachama wa chama hicho,
katika mkutano uliofanyika Shamiani Chake chake Mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema
endapo atapata ridhaa na kuwa Rais wanchi atahakikisha huduma zote za afya
Hospitalini zinapatikana bure, hususani za mama na mto, ili kuepusha vifo
vitokanavyo na uzazi.
‘’Nikiwa
Rais nitahakikisha vifaavyote ambavyo vya kujifungulia vinapatikana bure, mama awe amejifungua kwa uperashini ama kwa njia ya kawaida,
zote tutazigharamikia sisi,’’alieleza.
Aidha
akitaja kipaumbele chengine atakuja na kilimo cha umwagiliaji, ambacho kitasaidia
wananchi kupata chakula sambamba na kuzuia atahari za mabadiiko tabianchi.
Alisema
suala la mabadiliko ya tabia ni tatizo ambalo limekua likiathiri kwa kiasi
kikubwa jamii, hivyo pindi akichaguliwa, ataanzisha kilimo cha umwagiliaji,
wananchi wazalishe mazao na kupatikana chakula cha kutosha, sambamba na
kujiepusha na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabianchi.
Kwa
upande wake Mjumbe wa kamati kuu Taifa UDP Erasto Nyaga Suzan alisema endapo
Chama chao kitapata ridhaa ya kuongoza nchi atahakikisha analipa kipaombele suala
la ajira, kuona vijana wote wanaajiriwa.
‘’Tutakapoingia
madarakani tutahakikisha tunaweka miradi mbalimbali ambayo itawawezesha vijana
kupata ajira kwa wingi,’’alisema.
Mapema
Mjumbe wa Mkutani Mkuu wa Chama hicho Abass Mohamed Khatib aliwataka wananchi
wa Chake chake kukiunga mkono chama chao, ili kije kiwaletee mabadiliko.
Nae
mgombea Ubunge wa jimbo la Wawi, wa chama hicho Asha Mohamed Ali aliwataka
wananchi kuendeleza mshikamano na umoja walio nao, na sio kubaguana kwa ajili ya
siasa.
Alisema
suala la siasa sio ugomvi wala chuki, hivyo ipo haja wananchi kushikamana kwa
pamoja katika shughuli zote za kimaisha na wasibaguane kwa sababu ya vyama
vyao.

Comments
Post a Comment