Suhaila Omar: ni mwanamke anaepambana kuiheshimisha wadi ya Mtambwe baharini

 

Jee ni vipi Suhaila anapambana kuingia kwenye maamuzi

NA FATMA HAMAD, PEMBA

Nilipabana na wanaume saba nashukuru nimewaangusha, licha ya kuwa walinibeza kwa sababu ya uwanawake wangu.

Hiyo ni kauli ya Bi Suhaila Omar  Hamad mgombea wa Udiwani wadi ya Mtambwe Baharini kwa chama cha ACT Wazalendo, mwenye tunu ya kutaka kuingia kwenye maamuzi.

Bi suhaila ni mama wa watoto 5 ana umri wa (34), ni mzali wa mtambwe, anaishi kijiji cha Uondo, ambacho kinawakaazi wapatao 4220 ameanza harakati za kisiasa tangu mwaka 2017.

Suhaila anaonekana kuwa miongoni mwa wanawake waliojitokeza  kuingia kwa kishindo  kwenye siasa za ngazi ya chini mwaka huu, kipindi ambacho wananchi wengi na wadau wa jinsia wametoa msukumo kwa uwezeshaji wa wanawake.

Kutokana na hilo ndipo akanza kujitoa, ambapo uchguzi wa mwaka huu 2025, ni mara yake ya kwanza kuingia kwenye kinyan’ganyiro cha kuwania uongozi katika wadi ya mtambwe baharini.

Hata Takwimu na ripoti zinaonyesha ongezeko la ushiriki wa wanawake kwenye uchaguzi wa 2025 nchini Tanzania, ikijumuisha Zanzibar.

Suhaila ameanza kujihusisha na harakati za siasa tokea mdogo, ameanza kushika nafasi ndogo ndogo za kwenye tawi, jimbo, mkoa na hadi amefikia hatua mara hii kujiingiza katika kinyan’ganyiro cha kugombea nafasi hiyo ya Udiani wadi ya Mtambwe Bsharini.

Anasema baada ya wenzake na viongozi wake kumuona anauwezo mzuri wa kuongoza ndipo walipomshawishi aingie kwenye nafasi kubwa, aweze kusimama na kutetea shida za wanamtambwe akiwa kwenye maamuzi.

Hivyo mwaka huu 2025 ndipo aliposimama rasmi na kuchukua fomu ya kugombea Udiwani wa Wadi ya Mtambwe baharini kupitia tiketi ya chama cha ACT Wazalendo,ili

kuboresha huduma za msingi ikiwemo maji, afya, elimu na kutetea maslahi ya kina mama na vijana wa Mtambwe Baharini. 

Suhaila anatokea  ACT Wazalendo, chama kinachojivunia msimamo wa demokrasia, uwajibikaji na uwazi.

Anasema ACT ni chama kilichopewa usajili wa kudumu na kinaonekana kuwa mchezaji mkubwa wa upinzani na siasa za mrengo wa vyama pinzani, na kinachojali wanawake.

 Mipango ya chama kuhusu uwakilishi wa wanawake katika maamuzi  imekuwa ikisaidiwa na ngome za wanawake na mashirika ya kiraia.

Vikwazo anavyokutana navyo

Suhaila anasema moja ya changamoto anayokumbana nayo ni maneno ya baadhi ya watu wasiomtakia ambao wamekua wakimuwambia hawaezi kushinda kwa vile amegombea na wanaume na tena wenye uwezo wao  kifedha.

Anasema amepata pesa kidogo na amefanikiwa kufanya mikutano kidogo ya kampeni, ingawa maranyingi anafanya   za nyumba kwa nyumba.

 Anasema changamoto nyengine inayomkabili ni kukosa pesa za kuchapishia  mabango pamoja na vipeperushi kwa ajili ya kuvisambaza na kuweza kufahamika na wananchi.

‘’Suala la kukosa rasilimali pesa bado ni tatizo kwangu,nashindwa kufanya mikutano ya hadhara, na kuchapisha vipeperushi ambavyo vingeniwezesha kujitangaza kwa wananchi,’’anasema.

Anasema hata mabadiliko ya sheria za uchaguzi ya mwaka 2024 yanayoweka masharti mapya, usajili wa vyama na taratibu za kusajili wagombea pia umekuwa changamoto kwa baadhi ya vyama na wanawake wagombea.

VIPAUMBELE VYAKE

Mwanamama huyo anasema vipaumbele vyake ni kuwakaribu na wanawake wenzake na kuwasaidia kero zao ambazo zimekuwa zinawatokezea katika vjiji vyao.

Anasema kipaumbele chengine ni kuvisaidia vikundi vya wajasiriamali wanawake kwa kuvipa mikopo vianzishe biashara ambazo zitawazesha kuinua kipato chao,

Kipaumbele chake chengine pia anasema ni kusimamia nifuko ya Wabunge na Wawakilishi inayotolewa kwa ajili ya wananchi, na kuona inawanufaisha kweli wahusika wenyewe.

   


  FAMILIA YAKE

Anasema familia yake ikiwa ni pamoja na ndugu zake  watoto, na majirani zake wamekuwa wakimuunga mkono tokea mwanzo wa kutia nia ya kwenda kuchukua fomu yakuingia kwenye kinyan’ganyiro hicho.

‘’Nashukuru familia yangu inaniunga mkono, iko bega kwa bega na mimi, na wamekua wakiwahamasisha wapiga kura waweze kunichagua,’’anaeleza.

Anasema kwa upande wa mume wake ambae anafhamika kwa jina la Omar Hamad, amekua msaada mkubwa kwake, kampeni zake za nyumba kwa nyumba amekua akimpeleka na kumsadia kuwaomba wananchi wamuunge mkono mwanamke mwenzao huyo.

KIONGOZI WA CHAMA CHAKE

Juma Khamis Ali mwenyekiti wa ACT Wazalendo Mkoa wa Wete kichama anasema chama chao kinasera maalumu ya kuwasaidia wanawake washiriki harakati za uchaguzi na kuingia kwenye maamuzi.

Anasema Suhaila amekuepo chamani kwa muda mrefu, amekua akijitolea kukisaidia chama kuhakikisha kinapiga hatu, hivyo hata akipata nafasi katika wadi yake mabadiliko yatapatikana.

‘’Suhaila ni mmoja wa wanawake mwenye kujituma na mpambanaji, naamini akichaguliwa na kiongoza wadi ya mtambwe naamini anaweza kuleta mapinduzi makubwa ndani ya wadi na hata katika chama,’’anaeleza.

Takwimu

Kwa mujibu wa Chama cha Wandishi wa Habari WAnawake Tanzania Tamwa Zanzibar kupitia ripoti iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanziba mwaka 2020, kupitia nafasi ya Uwakilishi kwenye majimbo 50 ya Zanzibar wanawake waliojitokeza ni 61 walioshinda ni 8 na wabunge wanawake waliowakilisha Zanziba ni wane.

Takwimu kutoka Tume huru ya Uchaguzi Tanzania kwa upande wa wabunge walikua 141 walioshinda wanawake ni wane tu.

Kwa Uchaguzi wa mwaka huu 2025, unaweka historia mpya, kwani ni mara ya kwanza wanawake kujitokeza kwa wingi

kuwania nafasi mbalimbali ikiwemo Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani.

Kwa vile suasa la uchaguzi ni haki ya kila mtu kama katiba Katiba yetu mama ya nchi ya mwaka 1984 inavyoeleza katika kifungu cha 21,(2) kinaeleza mzanzibari yoyote anahaki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika kufikia maamuzijuu ya mambo yanayo muhusu yeye, maisha yake au yanayohusu Taifa lake.

Hata Mikataba ya kimataifa ya haki za kiraia na haki za kisiasa ya mwaka 1966 kifungu cha 25, kila raia ana haki ya kupiga kura na kuchaguliwa katika uchaguzi wa kweli, wa haki na wa mara kwa mara, uliofanywa kwa kura ya siri na kuhakikisha uhuru wa wapiga kura.

Ripoti za vyombo vya habari na mashirika ya jinsia zinaripoti ongezeko la wanawake wanaogombea mwaka 2025 ikilinganishwa na uchaguzi uliopita.

 Zanzibar pia imeona wanawake wakichukua nafasi kubwa katika kuingia kwenye nafasi za juu za uongozi,ikiwa ni sehemu ya mwelekeo wa kitaifa wa kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika siasa.

Hata kwa upande wa Bunge, ziko taratibu za viti maalum za wanawake na hii imekuwa moja ya njia za kuimarisha uwakilishi wa kijinsia, ingawa juhudi za kuongezeka kwa wagombea wa kiti cha uwakilishi wa moja kwa moja zinaendelea.





Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO