RAHMA HAMAD IDDI : MWANAMKE JASIRI WA WETE ALIEVAA NGAO YA SIASA
NA FATMA HAMAD, PEMBA
NI SAA KUMI
na moja za jioni kijua kikiwa kimetulia, kwambaali nikasikia mdundo wa beni
umeacha maji, nikanza kuufuatilia ili kujua kuna nini.
Nikanza
kusogea kidogo kidogo, nilipofika nikawakuta watu wameroa kijacho wakiserebuka
kwa beni, kumbe ilikua ni mkutano wa kampeni wa chama cha ADC.
Hapo
ndipo nikamuona mgombea ubunge wa jimbo la Wete kupitia chama cha ADC Bi Rahma
Hamad Iddi akiwa jukwaani akiwamwagia sera zake wananchi wa jimboni kwake.
Baada
ya kumaliza kuhutubia nilimsogelea nikanza kumsalmia habar za saivi, nzuri
hujambo, sjambo, nikamsifu nikamwambia ahongere kwa sera nzuri,nikanza
kujitambulisha kwake nikamuomba nifanye nae mahojiano, kwa vile ni mwanamke
mwenye kujiamini hakunikatalia.
Bi
Rahma Hamad ni mzaliwa wa Mtambwe nyali ana umri wa miaka (32)anasema huu ni
mwaka wa tatu tokea kuanza kujingiza harakati za kisiasa.
Anasema
tokea akiwa mwananfunzi ndote zake nikutaka kuwa kiongozi, ili aisaidie jamii
yake.
‘’Sijashawishiwa
na mtu kuingia kwenye harakati hizi bali, ni vile nikiona kero kama vile za
ukosefu wa maji vijijini, nilikua natamani kua kiongozi nije
kuziondosha,’’anasema.
Anasema
mwaka juzi 2023 akanza kujiingiza moja kwa moja katika harakati za kisiasa, na
mwaka huu 2025 akajitoa na kujiingiza kwenye kinyan’ganyiro cha kulisaka jimbo
la wete.
Anasema
jimbo ambalo amegombea ni jimbo lenye mchuano mkali, ila anaaamini kwa asilimia
90 anaweza kushinda, wanawake wenzake wamemuahidi kumuunga mkono.
CHANGAMOTO
AMBAZO AMEPAMBANA NAZO
Moja
ya changamoto ambazo amekumbana nazo ni jamii kumchukulia vibaya kwamba
ameshaingia katika dimbwi la uhuni.
‘’Naambiwa
natakakua muhuni kwa vile nishajihusisha na mambo ya kisiaa, ingawa sikuyasikia
ninaendelea na harakati zanguhadi ndoto zangu zikamilike,’’anasema.
Mbali
ya hilo anasema amekua akidharauliwa na kuambiwa hawezi kushinda yeye mwanamke,
kwani uongozi si fani ya mwanamke.
Asema
licha ya changamoto hizo hakukata tamaa aliendelea na harakati zake, na ameamua
kugombea, kwani anaamini kufanya hivyo ni haki yake ya kikatiba, na naamini
siku moja ndoto zake zitatimia.
VIPAUMBELE
VYAKE
Rahma
anasema endapo atachaguliwa na kuwa kiongozi wa jimbo la Wete, kuwa karibu na
wanawake na kuanzisha kamati maalu za kupambana na vitendo vya udhalilishaji
kwa wanawake na watoto.
‘’Wanawake
na watoto ni makundi ambayo yanakumbana zaidi na udhalilishaji wa kijinsia,
nikipata nafasi naahidi kuanzisha kamati maalumu, ambazo zitaepusha matendo
hayo ndani ya jimbo langu,’’analeza.
Mbali
ya hilo anasema ataanzisha miradi mbalimbali ambayo itawasaidia vijana na
wananchi wote kupata ajira, na kuendesha maisha yao.
Pia
anasema atawasaidia watoto mayatima na wanaoishi katika mazingira magumu waweze
kusoma elimu ya dunia na ya akhera, ili wajipambanue na hali ngumu za maisha
yao.
FAMILIA YAKE
INAVYOMUUNGA MKONO
Anasema
familia yake imekua bega kwa bega na yeye,na kila anapokwenda kufanya mkutano
wanakua wanamfuata, na humsaidi fedha wakati anapohitaji.
‘’Nashukuru
familia yangu tuko kitu kimoja, hapa unaponiona kwenye mkutano nipo na baangu,
mamaangu ndugu zangu na hata majirani zangu wananifuata,’’anasema.
Anasema
pia hatokua mwingi wa fadhila kutoa shukurani kwa mume wake kwani hata usafiri
anaotumia kwenda shughuli zake za kampeni ni wa mume wake.
MUME WAKE.
Muhine
Ahmed Kombo ni mume wa bi rahma anasema mke wake alipomshauri kutaka kujiunga
na harakati za siasa hakumzuia, bali alikua anampa mashirikiano, ili akamilishe
ndoto zake za kua kiongozi.
‘’Sijamzuia
mke wangu kujiungana harakati hizi za kisiasa, naamini jambo hilo analolifanya
ni jema kwani linaweza kuja kuleta maendeleo kwa familia yetu na hata wanajimbo
hili la Wete,’’anasema.
KIONGOZI WA
CHAMA CHAKE
Katibu
Mkuu wa chama cha Alliance for Democratic
Change ADC Mwalim Hamad Aziz anasema katika kuhakikisha
wanawake wanatimiza malengo yao ya kuwa viongozi, wanawawezesha kwa kuwapa
mafunzo mbalimbali wawe na uthubutu wa kuingia majimboni na kuwania uongozi.
Anasema
katika chama chao suala la ubaguzi halipo, bali kumekuepo na nafasi sawa kati
ya wanaume na wanawake.
Takwimu
Kwa
mujibu wa Chama cha Wandishi wa Habari WAnawake Tanzania Tamwa Zanzibar kupitia
ripoti iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanziba mwaka 2020, kupitia nafasi ya
Uwakilishi kwenye majimbo 50 ya Zanzibar wanawake waliojitokeza ni 61
walioshinda ni 8 na wabunge wanawake waliowakilisha Zanziba ni wane.
Takwimu
kutoka Tume huru ya Uchaguzi Tanzania kwa upande wa wabunge walikua 141
walioshinda wanawake ni wanne tu.
Kwa
Uchaguzi wa mwaka huu 2025, unaweka historia mpya, kwani ni mara ya kwanza
wanawake kujitokeza kwa wingi
kuwania
nafasi mbalimbali ikiwemo Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani.
Kwa
vile suasa la uchaguzi ni haki ya kila mtu kama katiba Katiba yetu mama ya nchi
ya mwaka 1984 inavyoeleza katika kifungu cha 21,(2) kinaeleza mzanzibari yoyote
anahaki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika kufikia maamuzijuu ya mambo
yanayo muhusu yeye, maisha yake au yanayohusu Taifa lake.
Hata
Mikataba ya kimataifa ya haki za kiraia na haki za kisiasa ya mwaka 1966
kifungu cha 25, kila raia ana haki ya kupiga kura na kuchaguliwa katika
uchaguzi wa kweli, wa haki na wa mara kwa mara, uliofanywa kwa kura ya siri na
kuhakikisha uhuru wa wapiga kura.
Ripoti za vyombo vya habari na mashirika ya jinsia
zinaripoti ongezeko la wanawake wanaogombea
mwaka 2025 ikilinganishwa na uchaguzi uliopita.
Zanzibar pia imeona
wanawake wakichukua nafasi kubwa katika kuingia kwenye nafasi za juu za
uongozi,ikiwa ni sehemu ya mwelekeo wa kitaifa wa kuhamasisha ushiriki wa
wanawake katika siasa.
Hata kwa upande wa Bunge, ziko taratibu za viti maalum za
wanawake na hii imekuwa moja ya njia za kuimarisha uwakilishi wa kijinsia,
ingawa juhudi za kuongezeka kwa wagombea wa kiti cha uwakilishi wa moja kwa
moja zinaendelea.
MWISHO
Comments
Post a Comment