MARYAM ALI: MGOMBEA UWAKILISHI ANAEPANIA KUMALIZA KERO ZA JIMBO LA MTAMBWE
Maryam Ali Rashid ni mgombea wa Chama cha Mapinduzi CCM, anaewania
uwakilishi jimbo la Mtambwe.
Binti huyu anaweka historia ni mfano tosha kwa
wanawake, kwani amekua na uthubu wa kuingia kwenye kinyan’ganyiro cha kusaka Jimbo
akiwa bado ana umri mdogo, ana miaka 34.
Ameanza
kushiriki katika shughuli za kijamii kupitia vikundi vya wanawake na miradi ya
maendeleo kijijini kwao, maji elimu ya watoto na uwezeshaji wanawake hapo ndipo
alipoanza kuingizwa zaidi kwenye siasa za chama kwa sababu kazi zake zinaonekana.
‘’Nimeanza
kwa kutetea shida ya maji kijijini kwangu, ambayo imekua inawakwaza wananchi kwa muda mrefu, na nimefanikiwa na sasa shida
imeondoka,’’anasema.
Baada ya kuona matokeo hayo watu wakanza kumuomba
aingie kwenye uongozi, afike kwenye ngazi za juu, aendelee kuwatetea.
NAFASI
AMBAZO AMEWAHI KUSHIKA KABLA YA KUGOMBEA
Kabla
ya kugombea uwakilishi Maryam alishika nafasi mbalimbali za kijamii na ndani ya
chama katika ngazi ya shehia na wilaya.
Miongoni
mwa nafasi ambazo ameshazishika ni kuwa msimamizi wa miradi ya wanawake, Katibu wa Baraza la Vijana Tanzania.
Ya
muhimu zaidi ni kazi zake kama mwenyekiti wa kikundi cha Ujima Cooparative ambacho
kinashughulikia ufadhili wa biashara ndogo ndogo na elimu ya kila raia, jukumu
lililoijenga sifa yake kwa wanajamii.
KILICHO
MSHAWISHI NA KILICHOMSAIDIA KUPATA NAFASI YA KUGOMBEA
Maryam
anasema kuwa msukumo mkubwa ulitokana na wanajamii waliomuona akifanya kazi za
kujitolea.
Alipata
ushawishi kwa Wakulima, walimu wa Skuli za msingi, viongozi wa kijiji na
wanawake, pia alipata ushawishi kutoka kwa viongozi wa chama jimboni ambao walimtambua kwa uwezo wake wa
kutatua matatizo ya wanakiji
chao.
‘’Kiongozi
wa chama change ananiona nashughulikia malalamiko ya maji kijijini kwetu,
akaanza kuniamini na akaona naweza kuleta mabadiliko katika baraza la
uwakilishi,’’ anasema.
Kipengele
chengine ambacho kimemsaidia ni mtandao wa wanawake na mashirika ya kijamii
anayoshirikiana nayo, pamoja na ujuzi wa
usimamizi wa miradi na uwezo wa kuzungumza hadharani.
CHANGAMOTO
ANAZOKUMBANA NAZO
Moja
ya changamoto ambazo anakumbana nazo ni mtazamo potofu kwa baadhi ya wanaume
kumtisha kwamba hawezi kupita kwani mwanamke si kiongozi.
SERA NA
MATARAJIO YAKE
Miongoni
mwa vipaumbele vyake ambavyo ameviweka Maryam ni kuendeleza ajira za vijana na
wanawake kupitia ufadhili wa biashara ndogo ndogo, na uwajibikaji wa serikali
katika utoaji wa huduma.
Pia
ataziendeleza sheria zinazowezesha ushiriki wa wanawake katika ngazi zote za
uongozi na kuimarisha utekelezaji wa sera za ardhi, ambapo ni kikwazo kwa
wanawake wakulima.
Matarajio
yake ni kuona Mtambwe inabadilika ndani ya muhula mmoja kwa kuongezeka upatikanaji
wa maji safi, upanuzi wa huduma za afya za msingi, na elimu bora kwa wasichana.
‘’Nataka
kila mtoto wa Mtambwe asome bila kikwazo, kila kijiji kipate maji na kila
kijana awe na ajira’’.
Maryam
anaishukuru familia yake kwa kumsaidia kila hatua anayopitia, ili atimize ndoto
zake.
‘’Kiukweli
siku nikipata ridhaa na kuwa muakilishi mama yangu ndie mtu wa mwanzo anaesababisha
mimi kuwa kiongozi, kwani ile pesa ya niliyokwenda kuchukulia fomu ya kugombea amenipa
yeye, ni pesa yake ya kila mwisho wa mwezi anayoipata kwenye pesa za wazee,’’anasema.
FAMILIA YAKE
Mama
yake anasema wakati mtoto wake huyo alipomshauri anataka kujiunga na harakati
za kisiasa hajamzuia, bali anamuunga mkono na kumsaidia kila hatu.
‘’Sijamzuia
mtoto wangu kuingia kwenye siasa kwani
naamini endapo atafanikiwa kulikamata jimbo, ambapo ndo kiyu yake, ataifanyia
vyema dhamana atakayopewa na wananchi
wake,’’anafahamisha mama yake.
Hamad
Ali Rashid (sio jina halisi) ni ndugu wa Maryam, anasema kutokana na mambo ambayo anayafanya kusaidia wanawake,
pamoja na wanafunzi wa Skuli, wanamatumaini makubwa dada yao huo anaweza
kulikamata jimbo la Mtambwe na akalibadilisha kkwa maendeleo.
‘’Dadaetu tunamuamini na endapo wananchi
watamchagua, jimbo la Mtambwe litan’gara kwa maendeleo, kwavile kiongozi
mwenyewe ameonyesha uthubutu wake wa kuwatatatulia shida zao tokea mapema’’.
KIONGOZI
WAKE WA CHAMA
Katibu
wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Wete anamsifu Maryam kwa kuendelea kufanya
kazi za kujitolea ndani ya chama na
kuwaonesha matokeo mazuri.
Mwalimu
mkuu Skuli ya Msingi Kijumbani iliyopo Kisiwani kwa Bintiabedi Hamad Khamis
Hamad anasema Maryam ni mwanamke anaefaa kupewa dhamana.
Anasema mgombea huyo anaonesha matumaini kabla
hajaingia kwenye maamuzi, kwani kupitia Ushirika wake wa Ujima Coperative amekua akisaidia vifaa mbali mbali kama vile sare za Skuli za
wanafunzi pamoja na karatasi kwa matumizi ya Ofisi.
‘’Tulikua tuna wanafunzi ambao sare zao
zimechanika miguuni na magotini, hali zao zinatilisha imani kwekweli, ingawa
Maryam amewasaidia na sasa wako hali nzuri wanaendelea na masomo,’’.anaeleza.
JAMII
Wazee
na vijana wa kijiji cha Mtambwe, wanasema wanafurahi kuona mwanamke wa kwanza
kusimama jimboni akiwa na shauku ya kwenda, kutetea matatizo yao kwenye maamuzi
bila woga.
WANAHARAKATI
Wanaharakati
masuala ya wanawake mfano Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA
Zanzibar wanamuona Maryam kama mfano wa kuigwa, anauwezo mkubwa wa kuleta
nafasi za ajira, kwa wanawake na kukuza elimu ya wasichana.
Kaimu
Mratibu wa Chama hicho Ofisi ya Pemba Amina Ahmed Mohamed anasema, moja ya
mkakati wao ni kutoa elimu kwa jamii, kuona wanawake wanahamasika kuingia
kwenye maamuzi, watetee shida za wanawake wenzao.
VIONGOZI WA
DINI
Viongozi
mbalimbali wa dini wamekua wakisisitiza kwamba wanawake wapewe nafasi, kwani wana uwezo mkubwa wa
kufanya kazi na kuleta mabadiliko.
Wanaendelea
kusema kuwa Hakuna dini hata moja inayomzuia fursa mwanamke, ambayo itakuepo
kwenye maeneo yao.
Safri
ya Maryam ni mfano wa mabadiliko ya kijamii, ni kielelezo cha ndoto za wanawake
kuingia kwenye uongozi bila kuogopa changamoto.
‘’Hii
si safari yangu pekeyangu, ni safari ya wanawake wote wa Zanzibar”
Ilani
ya Uchaguzi na serikali za mitaa ya
mwaka 2019 na Uchaguzi Mkuu 2020 inalenga
serikali kuu iliyoko madarakani na ile itakayoshika madaraka na taasisi
zake, ina wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa uwanja wa ushindani wa kisiasa ni
huru na wa salama kwa makundi yote hususani wanawake.
Hata
Mkataba wa kimataifa wa haki za kiraia na haki za kisiasa ya mwaka 1966 kifungu
cha 25, kila raia ana haki ya kupiga kura na kuchaguliwa katika uchaguzi wa
kweli, wa haki na wa mara kwa mara, uliofanywa kwa kura ya siri na kuhakikisha
uhuru wa wapiga kura.
Hata Katiba ya Zanzibar
ya 1984, ambayo ndo sharia mama, kupitia kifungu chake cha 21(1) nacho kinatambua haki ya kila raia
kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi bila ubaguzi.
.jpg)
.jpg)
Comments
Post a Comment