CHAMA CHA MAPINDUZI KUJA NA NEEMA KWA VIJANA NA FATMA HAMAD, PEMBA
NA FATMA HAMAD, PEMBA
CHAMA CHA Mapinduzi CCM Taifa kimesema moja ya vipaumbele vyake ni
kutatua changamoto ya ajira kwa vijana, pindi wananchi watakapokichagua kushika
madaraka na kuiongoza nchi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
Mjumbe
wa Halmashuari Kuu ya CCM Taifa Masoud Ali Mohamed alitoa kauli hiyo wakati
akizungmza na wananchi na wanaccm katika Uzinduzi wa Kampeni za Jimbo la Tumbe pamoja
na kuwanadi wagombea wa Ubunge, Uwakilishi na Udiwani, huko Viwanja Vya Gonga
Mfupa Tumbe Mkoa wa Kaskazini Pemba .
Alisema
Chama Cha Mapinduzi kinafahamu Changamoto ya ajira Kwa Vijana, hivyo
watakapokichagua tena kitaondosha Shida hiyo.
‘’Niwahakikishie
vijana mtakapokichagua chama cha CCM naahidi nyote mtapata ajira, ambapo ndio
shida yenu kubwa inayowaumiza,’’alisema.
Alisema
chamapekee ambacho kinaweza kuleta mabadiliko ni chama cha Mapinduzi, hivyo ni
vyema mkakichagua tena, ili kije kiwe mkombozi wa shida
zenu.
Aidha
alisema kipaumbele Changine ni kudhibiti
Mfumuko wa Bei za Bidhaa za Vyakula, kuona kila mwananchi anauwezo wa kula mlo
uliotimia, ili kuwa na jamii yenye afya bora.
Alisema
moja ya eneo ambalo serikali ya Mapinduzi imeweka kipaumbele ni kupunguza kodi
za vyakula, ili wananchi waondokane na njaa, na wajasiriamali wamudu kufanya
biashara.
Sambamba
na hilo alisema wataweka ghala la kuhifadhia bidhaa, kuona vyakula vinapatikana
kwa muda wote na bila kupanda kwa bei, hatakama duniani kimepungua.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumujiya ya
Wazazi Mkoa wa Kaskazini Pemba Ramadhan Issa Kipaya na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya
Micheweni Ali Masod Kombo wamewataka wananchi wa Jimbo la Tumbe kutofanya
makosa kwa kuwachagua Viongizi makini, ambao wanaweza kusimama na kutetea kero
zao.
Walisema
wakati umepita wa kuchagua kiongozi kwa sababu ya chama Fulani ama kwa kipato
chake, wachague watu ambao wanauzalendo nan chi yao na wananchiwao.
Naye
Mgombea wa Uwakilishi Jimbo la Tumbe Salma Khamis Tumu alisema atakapochagualiwa
na wananchi na kuwa mwakilishi wa Jimbo hilo ataelekeza nguvu zake katika
kuinua Vikundi Vya Ushirika kwa kuvipatia usajili na Mitaji.
‘’Naamini
katika jimbo langu kuna vikundi vingi vya ujasiriamali lakini havifikii malengo
yao kutoana na kukosa mitaji, hivyo mkinipa kura za ndio nitahakikisha
naviimarisha kwa kuvipatia mitaji viweze kuzalisha bidhaa kwa wingi na zenye
ubora,’’alisema.
Aidha
kwa upande mwengine alisema atahakikisha anapigania maslahi ya watu
wenyeulemavu, ili kuona nawao hawaachwi nyuma katika fursa mbali mbali za
kimaendeleo ambazo zinakuja katika jimbo lake.
‘’Nitakapokua
muwakilishi sitokubali kuona mtu mwenye ulemavu amefungiwa ndani, nitapambana
kila mtoto mwenye ulemavu anapata haki zake stahiki iwe ya elimu, afya sambamba
na kushiriki katika miradi yote ya maendeleo ambayo imekua ikitokezea shehiani
mwao,’’alisema.
Maryam Hemed na kutoka Jimbo la Tumbe waliahidi kumuunga mkono mwakilishi wa jimbo hilo, kwa vile ni mwanamke mwenzao, ili aje asimame na kutetea shida za wanawake wenzake.
Walisema
shida za wanawake anazijua mwanamke vile vile, hivyo walisema watahakikisha wanampa kura za ndio, jami ya wanawake ije iwe
rahisi kumfika na kumuelekezea matatizo yao.
Walisema mgombea huyo alishakamata nafasi ya
udiwani miaka iliyopita na kuna mengi mazuri aliyowafanyia, hivyo wataendelea
tena kumrudisha kwenye maamuzi, akasimame ni kuzisemea kadhia za watu wa Tumbe.

Comments
Post a Comment