ASHA MOH’D ALI MWANAMKE MWENYE NDOTO YA MABADILIKO

 


NA MOZA SHAABAN,PEMBA

NATAMANI moja niwe kiongozi nilete mabadiliko katika Jimbo langu.

Hayo si maneno ya mtu mwengine bali ni maneno ya Asha Mohamed Ali  ambae anagombea Ubunge Jimbo la Wawi kwa tiketi ya Chama cha  United Democratic Party (UDP.)

Mama huyo mwenye umri wa (45) mkaazi wa Wawi, wilaya ya Chakechake mkoa wa Kusini Pemba, ana watoto wanane (8),  wanawake watano na wanaume watatu, na  sasa yupo kwenye ndoa.

Asha alizaliwa mwaka 1977 katika kijiji cha Mvumoni Wawi wilaya ya Chakechake mkoa wa Kusini Pemba, na elimu yake ni elimu ya msingi aliyoipata katika Skuli ya Sekondari  Ziwani.

Asha  alianza safari yake ya kisiasa mwaka 2000, alivutwa na hamu ya kutetea haki za wananchi wa Pemba, hasa wanawake na vijana.

Anasema msukumo wake mkubwa wa kujingiza kwenye harakati za kisiasa ulitokana na ushauri wa mume wake.

Mume wake  aliemuoa mwanzo alikua kiongozi wa chama cha jahazi asilia, na yeye alimshauri na kujingiza kwenye harakati za kisiasa kupitia chama cha UDP.

‘’Kwa kusema kweli mimi hizi harakati nimerithi kwa marehemu mume wangu, mungu amuweke pahali pema sito msahau kwani yeye ndie alienifikisha hapa nilipo sasa,’’anaeleza.

USHIRIKI WAKE KWENYE CHAGUZI

Asha si mgeni kwenye siasa  za ushindani, alishawahi kugombea mara (3), na hii ni mara ya nne kugombea ubunge jimbo hilo hilo la Wawi.

‘’Nilishagombea mara tatu sijafanikiwa, sijakata tamaa na kwa uwezo wa Mungu marahii ninaimani kubwa nitafanikiwa kulikamata jimbo, ili niwaletee wanawawi maendeleo,’’anasema.

Anasema safari yake imekua na changamoto, lakini pia anamafanikio ya kujenga mtandao mpana kwa wafuasi wake.

Anaeleza kuwa alishawahi kushika nafasi ya Katibu wa akinama Taifa kwa muda wa mika mitano, na sasa ni mjumbe wa bodi ya wadhamini, katika chama chake.

Awali anaingia sasa kwenye mchakato huo wa  kinyanganyiro cha kugombea familia yake ilikua haimpi mashirikiano, ilikua wanahisi wakimchagua kama wanazitupa kura zao.

‘’Mwanzoni mwa mwaka 2000, wakati naanza sasa hata familia yangu ilikua haikopamoja na mimi kura zao walikua wazipeleka kwa Chama cha CUF ambapo kwa sasa ni ACT Wazalendo,’’anasema.

Ingawa kuanzia Uchaguzi uliopita wa 2020, walibadilika na walinipa kura zao na nilipata kuranyingi, na hadi sasa wakobega kwa bega na mimi kwa kila hatua ninayopitia.

SERA ZAKE KUU

Sera zake ambazo anazizungumzia katika kampeni zake ni kuwapatia wanavikundi miundombinu ya kisasa ya kilimo,  kuwatafutia mbegu bora pamoj na mitaji, wazalishe mazao ya biashara na ya chakula, kupatikane chakula cha kutosha na kuondokana na janga la njaa.

Sambamba na hayo anasema endapo atachaguliwa atahakikisha anawangalia walimu wa Madrasa za Qur an kwa kuwapa mshahara.

‘’Walimu wa Madrasa wengi ni masikini, naahidi nitakapokua mbunge nitahakikisha walimu wa madrasa nawapa mshahara walimu wa madras kama walimu wengine, ili waendeleze kitabu cha mwenyezi Mungu,’’anaeleza.

Mama huyo anasema ni wakati kwa jamii kuwachagua viongozi wanawake katika majimbo yao, wawaletee maendeleo.


MSAADA WA FAMILIA YAKE

Familia ya Asha imekua msaada mkubwa katika safari yake hiyo,kwani wamekua wakimsaidia kifedha, kimaombi na hata kushiriki katika mikutano yake ya kampeni anayoifanya, na ile ya kuenda nyumba kwa nyumba.

‘’Pesa ambazo nilikwenda kuchukulia fomu nilidundulikiza kwenye biashara zangu, na nyengine nilipewa na familia yangu” anasema.

Kutokana na mshikamano huo ambao amekua akiupata kupitia kwa  familia yake, umekua moja ya nguzo ya kuimarisha nafasi yake kisiasa, na inamfanya kuwa na matumaini makubwa ya kufikia ndoto zake za kuwa kiongozi.

MUME WAKE

Anasema alipomuoa alimkuta na harakati zake hizo za kisiasa hajawahi kumzuia hata siku moja kufanya shughuli zake hizo.

Anasema amekua akimsaidia kwa kila hatua iwe nikwa pesa ama kwa ushauri, ili aweze kufanikiwa katika harakati zake hizo.

‘’Sijafanya wivu wala sijamkataza nimekua nikimsaidia kwa kila hatua, afanikiwe naamini akipata ataisaidia familia yetu, na hata wanawake wenzakeambao wanamzunguka,’’anaeleza .

Anasema kwa vile mke wake huyo ni mtu anaependa maendeleo na amekua ni mwenye kujali, endapo atapata nafasi ataondosha kero zinazowakwaza wananchi, ili waishi kwa matumaini.

‘’Naamini ipo siku atafanikiwa kwani nimtu ambae hapendi kukata tama, na mtu mwenye kujiamini na mwenye kujitambua.

 MTOTO WAKE

Omar Saleh Khalfan  ni mtoto wa mama huyo anasema tokea alipofahamu mama yake yupo katika harakati za kisiasa, amekua akigombea nafasi ingawa hajawahi kushika jimbo.

Anasema suala la uongozi kwa mwanamke ni jambo zuri, hivyo kitendo anachokifanya mama yao sio kitendo kibaya kwani, kinaweza kuja kuleta mabadiliko katika familia yao na hata kwa wananchi wa jimbo lao.

‘’Nimekua nikimsaidia mamayangu kwa kila hatua, aweze kufanikiwa, na namini siku moja atakuja kuwa mtetezi wa wanyonge hasa wanawake na watoto,’’anasema.

Anasema mtoto hufuata kichogo cha mlezi wake kwani nayeye amekua ni mwanasiasa mkubwa katika Chama hicho cha UDP.

KIONGOZI WA CHAMA CHAKE

Juma Khamis Faki Naibu Ktibu mkuu wa Chama cha  UDP anasema Asha ni mwanamke jasiri, muaminifu na mwenye kupenda maendeleo ya wenzake.

Anaamini endapo atapata ridha ya kuwa Mbunge maendeleo ya wananjimbo la wawi yatapatikana na shida zinazowakabili atazisimamia  vyema na kuzitetea.

‘’Asha ni mwanamke mpambanaji anapenda mashirikiano na wenzake, endapo kama atapita naamini jimbo la Wawi litan’gara kwa maendeleo,’’anasema.

Anasema kutokana na mafunzo mbali mbali ya uongozi ambayo wamekuwa wakiwapatia wanawake wa Chama chao yameweza kumjenga na amekua na uthubutu na shauku ya kutaka kua kiongozi, alete mabadiliko ndani ya jimbo lake.

WANAHARAKATI

Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar kimekua kikiwaelimisha wanawake juu ya masuala ya uongozi, wajitokeze  kwa wingi kwenye mchakato wa Uchaguzi na kuwania nafasi majimboni, kwani ni haki yao kikatiba.

Amina Ahmed Mohamed Mratibu kutoka TAMWA Pemba anasema lengo la kuwaelimisha wanawake hao ni kuwa na uthubutu wa kugombea nafasiza uongozi, ili watatue kero za wanawake wenzao katika majimbo yao pindi wakipata nafasihizo.

‘’Shida za wanawake anazijua mwanamke, na ndio maana tunawahamasisha wagombee waende wakatatue hizo shida za wanawake wenzao,’’anasema.

Hii ni ishaza nzuri ya mabadiliko, huku Asha Mohammed Ali akiwa miongoni mwa wanawake wanaothubutu kushindana moja kwa moja kwenye majimbo badala ya kutegemea viti maalumu.

  TAKWIMU

Kwa mujibu wa Chama cha Wandishi wa Habari WAnawake Tanzania Tamwa Zanzibar kupitia ripoti iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanziba mwaka 2020, kupitia nafasi ya Uwakilishi kwenye majimbo 50 ya Zanzibar wanawake waliojitokeza ni 61 walioshinda ni 8 na wabunge wanawake waliowakilisha Zanziba ni wane.

Takwimu kutoka Tume huru ya Uchaguzi Tanzania kwa upande wa wabunge walikua 141 walioshinda wanawake ni wane tu.

Kwa Uchaguzi wa mwaka huu 2025, unaweka historia mpya, kwani ni mara ya kwanza wanawake kujitokeza kwa wingi

kuwania nafasi mbalimbali ikiwemo Urais, Ubunge, Uwakilishi na Udiwani.

Kwa vile suasa la uchaguzi ni haki ya kila mtu kama katiba Katiba yetu mama ya nchi ya mwaka 1984 inavyoeleza katika kifungu cha 21,(2) kinaeleza mzanzibari yoyote anahaki na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika kufikia maamuzijuu ya mambo yanayo muhusu yeye, maisha yake au yanayohusu Taifa lake.

Hata Mikataba ya kimataifa ya haki za kiraia na haki za kisiasa ya mwaka 1966 kifungu cha 25, kila raia ana haki ya kupiga kura na kuchaguliwa katika uchaguzi wa kweli, wa haki na wa mara kwa mara, uliofanywa kwa kura ya siri na kuhakikisha uhuru wa wapiga kura.


 

 


Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO