NA FATMA HAMAD, PEMBA
MAHAKAMA ya Mkoa chake chake imemuhukumu
kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 30,pamoja na kulipa fidia
shilingi Milioni tatu Hakim Said Hakim mwenye umri wa miaka 36
Mshirazi wa Jondeni wilaya ya Mkoani , baada ya kutiwa hatiani kwa kosa
la kubaka mtoto mwenye umri wa miaka 7.
Hukumu ya kijana
huyo kutumikia chuo cha mafunzo kwa kosa hilo la kubaka ambalo ni kinyume
na vifungu vya 108,(1)(2) n 109 (2) Vya sharia namba 6 ya mwaka 2018 sheria
ya Zanzibar ,imetolewa October 21 2025 chini ya Hakimu
dhamana Taki Abdalla Habibu mbele ya mwendesha Mashataka wa
serikali Kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Juma Ali Juma .
Juma Ali Juma
mwendesha wa mashtaka wa serikali kutoka ofisi ya mkurugenzi wa
mashtaka alisema kuwa hukumu hiyo iwe fundisho kwa wengine walioko
katika jamii ambao wanaendelea na vitendo vya udhalilishaji kwa
watoto ,na kuonesha utendaji wa haki na msaada wa serikali katika
kupambana na vitendo vya udhalilishaji .
Ilidaiwa mahakamani
hapo kuwa mnamo siku ya tarehe 14 july 2024 majira ya saa 4.00 usiku huko mkoani
mkoa wa kusini pemba kwa kutumia nguvu na bila ya ridhaa yake, alimbaka
mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 7 Jambo ambalo ni kosa kisheria.
Ikumbukwe kuwa kesi
hiyo kwa mara ya kwanza ilifunguliwa Mahakamani hapo tarehe 3\12\2024 na jumla
ya mashahidi 7 walitoa ushahidi ulioiwezesha Mahakama kumtia hatiani mshtakiwa
huyo.
Hakimu huyo alimuamuru kijana huyo kutumikia
Chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka 30 sambamba na kulipa fidia ya shilingi 3 ili iwe fundisho
kwake na wengine wenye tabia kama hizo.
Comments
Post a Comment