ADC YAAHIDI KUWAFUTIA MADENI WALIOKOPA ELIMU YA JUU

 


NA FATMA  HAMAD, PEMBA

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tikati ya Chama cha Alliance for  Democratic  Change ADC  Hamad Rashid Moh’d amesema endapo atapata ridhaa ya wananchi na kuingia madarakani atawalipia deni la mkopo wa Bodi ya Mikopo Zanzibar wale wote waliokopeshwa kwa ajili ya kusomea, wafaidike na mishahara yao.

 Mgombea huyo aliyasema hayo kwakati akiwahutubia wananchi ikiwa ni muendelezo wa mikutano yake ya kampeni ulifanyika Mjimbini Mkoani mkoa wa Kusini Pemba.

Alisema waajiriwa wengi wamekua wakiishi maisha duni, kutokana na mishahara yao kukatwa na kulipa deni la mkopo hiyo.

Alisema sera ya chama chake ni kuepo kwa elimu bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu, hivyo akiingia madarakani atawalipia madeni kwa wote ambao wanadaiwa na Bodi ya mikopo, waondokane na halingumu za maisha.

‘’Mishahara yenyewe midogo haiwakidhii haja zao halafu unakatwa,  naahidi nikichaguliwa nawalipia wote wanaodaiwa,  wafurahie maisha yao,’’alisema.

Aidha kwa upande mwengine alisema atawapeleka kufanya kazi nje ya nchi wafanyakazi wa kada ya uuguzi, manesi na madaktari kwenda kupata ujuzi zaidi, ili kuja kuokoa maisha ya wananchi wa Zanzibar.

Mapema Katibu mkuu wa chama cha ADC Mwalim Hamad Aziz alisema endapo wataingia madarakani watajenga Chuo cha Uvuvi kisiwani Pemba, ili kuzalisha wataalamu kupitia sekta hiyo.

‘’Tutakapoingia madarakani tutaanzisha chuo cha uvuvi, vijana wa Pemba wasome na kupatikana kwa wataalamu wa uvuvi na kupatikana ajira kwa wingi,’’alisema.

Kwa upande wake Mratibu wa kampeni wa chama hicho Hafid Khamis Amour aliwataka wananchi wa Mjimbini hususani wanawake, kukichagua chama cha ADC, ili kiwaletee maendeleo.

‘’Wanawake ni kundi ambalo limekua likikumbana na vikwazo kadhaa vya udhalilishaji, hivyo nawaomba mkichague chama chetu, kije kuwa mkombozi wa shida zenu,’’alisema.

Aidha amewataka wananchi  hao kuwachagua viongozi ambao wanauchungu na chi yao ambao watawaletea mabadiliko majimbonimwao, na sio kuchagua kwa ajili ya chama Fulani.  

Nao baadhi ya wananchi wa Mjimbini walisema watahakikisha wanakiunga mkono chama hicho, kwani kimeonesha matumaini makubwa kwa wananchi wake.




Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO