Posts

Showing posts from October, 2025

BARAZA LA HABARI TANZANIA (MCT ) LATOA SOMO KWA WANDISHI WA HABARI PEMBA KUELEKEA UCHAGUZI

Image
   NA FATMA HAMAD, PEMBA   BARAZA  la   Habari  Tanzania  (MCT) Ofisi ya Zanzibar , limewataka  Waandishi wa Habari kuzingatia miiko, kanuni na maadili yao wakati wanapoandika habari zao hasa  katika  kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu, ili kuepusha nchi kuingia kwenye migogoro.   Ametoa nasaha hizo kwa Viongozi wa klabu ya Wandishi wa Habari kisiwani Pemba (PPC), pamoja na baadhi ya wanachama wao Mratibu mstaafu wa Baraza la habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar,Bishifaa Said Hassan katika kikao maalumu cha kuwatembelea wanachama wake.   Alisema kuwa Baraza la habari linajukumu kubwa la kuzungumza na Waandishi wa habari sambamba na kuwakumbusha wajibu wao kwani sauti na kalamu zao zikitumika vibaya vinaweza kupelekea machafuko yasio ya kutegemewa hasa katika kipindi hichi cha kuelekea Uchaguzi mkuu.   Alieleza kuwa Baraza la habari Tanzania (MCT) Ofisi ya Zanzibar imeamuwa kuwatembelea wanachama wake ikiwem...

RAHMA HAMAD IDDI : MWANAMKE JASIRI WA WETE ALIEVAA NGAO YA SIASA

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA NI SAA KUMI na moja  za jioni kijua kikiwa kimetulia, kwambaali nikasikia mdundo wa beni umeacha maji, nikanza kuufuatilia ili kujua kuna nini. Nikanza kusogea kidogo kidogo, nilipofika nikawakuta watu wameroa kijacho wakiserebuka kwa beni, kumbe ilikua ni mkutano wa kampeni wa chama cha ADC. Hapo ndipo nikamuona mgombea ubunge wa jimbo la Wete kupitia chama cha ADC Bi Rahma Hamad Iddi akiwa jukwaani akiwamwagia sera zake wananchi wa jimboni kwake. Baada ya kumaliza kuhutubia nilimsogelea nikanza kumsalmia habar za saivi, nzuri hujambo, sjambo, nikamsifu nikamwambia ahongere kwa sera nzuri,nikanza kujitambulisha kwake nikamuomba nifanye nae mahojiano, kwa vile ni mwanamke mwenye kujiamini hakunikatalia. Bi Rahma Hamad ni mzaliwa wa Mtambwe nyali ana umri wa miaka (32)anasema huu ni mwaka wa tatu tokea kuanza kujingiza harakati za kisiasa. Anasema tokea akiwa mwananfunzi ndote zake nikutaka kuwa kiongozi, ili aisaidie jamii yake. ‘’Sijashaw...

Suhaila Omar: ni mwanamke anaepambana kuiheshimisha wadi ya Mtambwe baharini

Image
  Jee ni vipi Suhaila anapambana kuingia kwenye maamuzi NA FATMA HAMAD, PEMBA Nilipabana na wanaume saba nashukuru nimewaangusha, licha ya kuwa walinibeza kwa sababu ya uwanawake wangu. Hiyo ni kauli ya Bi Suhaila Omar   Hamad mgombea wa Udiwani wadi ya Mtambwe Baharini kwa chama cha ACT Wazalendo, mwenye tunu ya kutaka kuingia kwenye maamuzi. Bi suhaila ni mama wa watoto 5 ana umri wa (34), ni mzali wa mtambwe, anaishi kijiji cha Uondo, ambacho kinawakaazi wapatao 4220 ameanza harakati za kisiasa tangu mwaka 2017. Suhaila anaonekana kuwa miongoni mwa wanawake waliojitokeza   kuingia kwa kishindo   kwenye siasa za ngazi ya chini mwaka huu, kipindi ambacho wananchi wengi na wadau wa jinsia wametoa msukumo kwa uwezeshaji wa wanawake. Kutokana na hilo ndipo akanza kujitoa, ambapo uchguzi wa mwaka huu 2025, ni mara yake ya kwanza kuingia kwenye kinyan’ganyiro cha kuwania uongozi katika wadi ya mtambwe baharini. Hata Takwimu na ripoti zinaonyesha ongezeko la...

BISHAMBA ALI ALAWI: MWANAMKE MWENYE UTHUBUTU PEMBA

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA ‘’Mwanamke akipewa nafasi ya kumiliki ardhi na akajishughulisha na kilimo, basi haachi nyayo pekee ardhini, bali huacha alama ya mafanikio,’’ Hayo si maneno ya mtu mwengine bali ni mwanamke mpambanaji mkaazi wa shehia Kambini Wilaya ya Wete Pemba, Bishamba Ali Alawi. Katika mazingira ya kawaida ya vijijini, mwanamke huyo sasa ni kielelezo tosha jinsi kilimo msitu (Agro forest) kinavyombadilisha maisha yake. Anasema, alipitia ugumu kwenye maisha yake kutokana na kukosa kazi ya maana ya kujikwamua kiuchumi ingawa hakukata tama. Lakini tangu mwaka 2023 aliposhiriki mafunzo ya kilimo msitu, alianza kuona mabadiliko ya maisha kuwa mazuri kwa upande wake. Kupitia mafunzo yaliotolewa na Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kwaupande wa Zanzibar na Jumuia ya Uhifadhi wa Misitu Pemba (CFP), Bishamba alijifunza kuchanganya aina ya miti mbali mbali kwenye shamba lake. Walifunzwa kwamba, uchanganyaji wa miti kwenye shamba moja unasaidia k...

ADC YAAHIDI KUWAFUTIA MADENI WALIOKOPA ELIMU YA JUU

Image
  NA FATMA  HAMAD, PEMBA Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tikati ya Chama cha Alliance for  Democratic  Change ADC  Hamad Rashid Moh’d amesema endapo atapata ridhaa ya wananchi na kuingia madarakani atawalipia deni la mkopo wa Bodi ya Mikopo Zanzibar wale wote waliokopeshwa kwa ajili ya kusomea, wafaidike na mishahara yao.   Mgombea huyo aliyasema hayo kwakati akiwahutubia wananchi ikiwa ni muendelezo wa mikutano yake ya kampeni ulifanyika Mjimbini Mkoani mkoa wa Kusini Pemba. Alisema waajiriwa wengi wamekua wakiishi maisha duni, kutokana na mishahara yao kukatwa na kulipa deni la mkopo hiyo. Alisema sera ya chama chake ni kuepo kwa elimu bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu, hivyo akiingia madarakani atawalipia madeni kwa wote ambao wanadaiwa na Bodi ya mikopo, waondokane na halingumu za maisha. ‘’Mishahara yenyewe midogo haiwakidhii haja zao halafu unakatwa,  naahidi nikichaguliwa nawalipia wote wanaodaiwa,  wafurahie maisha yao,’’alisema...

AFUNGWA JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA BINTI WA MIAKA 7

Image
                              NA FATMA HAMAD, PEMBA   MAHAKAMA ya Mkoa chake chake imemuhukumu kutumikia chuo cha mafunzo  kwa muda wa miaka 30,pamoja na kulipa fidia shilingi Milioni tatu Hakim  Said Hakim mwenye umri wa miaka 36 Mshirazi  wa Jondeni wilaya ya Mkoani , baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la kubaka  mtoto mwenye umri wa miaka 7.   Hukumu ya kijana huyo  kutumikia chuo cha mafunzo kwa kosa hilo la kubaka ambalo ni kinyume na  vifungu vya 108,(1)(2) n 109 (2) Vya sharia namba 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar ,imetolewa October 21 2025  chini ya Hakimu dhamana  Taki Abdalla Habibu  mbele ya mwendesha Mashataka  wa serikali Kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Juma Ali Juma .   Juma Ali Juma  mwendesha wa mashtaka wa serikali   kutoka ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka  alisema kuwa hukumu hiy...

KAMPENI ZA UCHAGUZI 2025, FURSA MPYA KWA WANAWAKE PEMBA

Image
                 NA FATMA HAMAD, PEMBA WAKATI kampeni za uchaguzi mkuu wa 2025 zikiendelea kupamba moto kila kona kisiwani Pemba, wananchi wanamiminika kwa wingi kusikiliza sera za viongozi wao, huku wakiwa na biashara zao ndogo ndogo. Hiyo inaonesha wazi kwamba siasa siyo tu mjadala wa kura na wagombea, bali pia ni chanzo kipya cha ajira na kipato kwa wanawake. Fursa mbali mbali za kibiashara zinapatikana katika mikutano ya kampeni kwa wauzaji wa chakula, mafundi vyarahani, hata kwa wanawake wanaofanya kazi kwenye sekta za utalii na huduma. Kwani, wengi wanasema kampeni zimewafungulia milango ya biashara na kuleta matumaini katika mifuko yao. Kipindi cha kampeni kila mkutano ni fursa ya kipato kwani watu hupata kusikiliza sera za wagombea, huku wakiwa na biashara zao mikobani. Katika mkutano wa kampeni wa chama cha Alliance for   Democratic Change ADC uliofanyika Mchangamdogo, mwandishi alikutana na muuza juisi na malai Asha...