
NA FATMA
HAMAD, PEMBA
WANAWAKE
ambao ni wagombea kutoka vyama tofauti
vya siasa wametakiwa kuzisoma na
kuzifahamu Sera na Seria za vyama vyao, ili waweze kuzungumza mambo yenye maana
wakati watakaposimama katika majimbo na kunadi sera zao.
Alisema ili waweze kusimama na kuzungungumza sera nzuri, ni
vyema kurudi katika vyama vyao na kuzisoma sera zao ili waweze kuzitambua.
Akizungumza katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wanawake wagombea kwa nafasi mbali mbali Mkurugenzi wa mradi wa kuwawezesha
wanawake katika masuala ya uongozi na Demokrasi kutoka Jumuia ya utetezi
wa kimazingira na haki za wanawake (Pegao) Hafidh Abdi Said katika ukumbi wa Chama
cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Mkanjuni Chake chake mkoa wa Kusini Pemba.
Alisema ni vyema kila mwanamke ahakikishe anafuata
sera ya chama chake, wakati anapokwenda kusimama na kunadi sera zake katika
jamii yake.
Alifafanua kuwa kila mmoja arudi kwenye chama chake ili
kusoma sera na kuweza kuzitambua, kwani kutamfanya kuzungumzia mambo yenye
maana ambayo yanaweza kuleta mabadiliko katika majimbo yao.
"Niwatakewanawake nyote mnaotarajiwa kuwa viongozi
kwenda kuzungumza kero ambaozinawakwaza wanajamii, na sio kuzungumzia yasikua na faida yoyote kwa
wananchi,’’anafahamisha.
Anasema endapo watasimama vyema na kuwa na sera nzuri zenye
maslahi na umma, kutawafanya waweze kuchaguliwa na kusimama kwa wingi
majimboni.
Kwa upande wake Mratibu wa Program kutoka Chama cha
waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar Sabrina Yussuf
Mwintanga alisema ni wajibu kwagombea hao, kuhakikisha wanakwenda kutekeleza vyema na kwa kujiamini majukumu yao, na sio kuzungumza sera ambazo
zitapelekea kuchafuana.
"Nyinyi ni wanawake shida zilizomo za kwenyevijiji
vyenu mnazijua, simameni na muwe karibu zaidi na wananchi wapate hamu ya kuja
kuwachagua siku ya kutia
kura,’’aliwasisitiza.
Mapema Mratibu wa mradi huo wa kuwawezesha
wanawake katika masuala ya uongozi na Demokrasia kutoka Jumuia ya utetezi wa kimazingira na haki za
wanawake Pemba (Pegao) Dina Juma Makota alisema ni wakati kwa wagombea hao, kuweka tageti na malengo waliyoyakusudia katika uongozi wao pindi wakichaguliwa.
" Wanawake wenzangu niwatake kwenda kusimamia vyema
majukumu yenu hakika nyinyi ni viongozi watarajiwa", alifafanua.
Mkufunzi wa mafunzo hayo
Sabahi Mussa Said alisema ni wajibu kwa watia nia hao, kufuata sheria,
Sera na maadili ya uchaguzi kwa wakati
wote wanapokua wakinadi sera zao, ili kudumisha Amani na utulivu kabla na baada
ya uchaguzi.
Alisema suala la uchaguzi ni kipindi cha mpito, hivyo ni
vyema kuwa wastaarabu, ili kulinda hadhi na heshima ya utu wao na Taifa lao.
Kaimu Mratibu wa
Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar
Ofisi ya Pemba Amina Ahmed Mohamed alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwajenga
vyema wagombea wanawake wawe na uthubu
kusimama na kuzungumza sera ambazo zitasaidia kupatikana kwa maendele, kwenye
jamii zao.
Baadhi ya wagombea hao ambao walisema mafunzo hayo yamewajenga vyema, na
kuhakikisha wanafuata yote ambayo wameelekezwa.
Mafunzo hayo ya
kuwajengea uwezo wagombea hao yameandaliwa na Chama cha waandishi wa habari Wanawake
Tanzania Tamwa Zanzibar kwa ushirikiano wa Pegao, Zafela
na Juwauza.
Comments
Post a Comment