WAJAWAZITO WATAKIWA KUTUMIA LISHE BORA



NA FATMA HAMAD, PEMBA

AKINAMAMA wajawazito wamehimizwa kula vyakula vyenyelishe bora, ambavyo vinapelekea kuongezeka kwa uzito miilini mwao, ili kulinda afya ya mama, kumfanya mtoto azaliwe akiwa salama.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Chakechake Kaimu Mratibu wa Kitengo cha Lishe kisiwani Pemba Said Abdi Said alisema  lishe hupelekea kuongezeka kwa uzito kwa mama mjamzito, na pia kunasababisha ukuaji  kwa mtoto alie tumboni.

Alisema  mjamzito anatakiwa kuongezeka  uzito wastani wa kilo nane hadi 12, kwa kipindi chote cha ujauzito wake, hivyo ni vyema kutumia lishe bora, ili kulinda afya na usalama kwa mama na mtoto.

‘’Kuongezeka kwa uzito kwa mjamzito ni muhimu, hivyo jitahidini kutumia lishebora ili kuboresha afya ya mama na mtoto aliemo tumboni,’’alisema.

Alisema  mjamzito anatakiwa kula mlo kamili wenyemchanganyiko wa vyakula kutoka katika mchanganyiko wa makundi sita kama vile Mboga, Matunda, Samaki kila siku ili kuongeza uzito katika kipindi hicho cha ujauzito.

Akitaja athari ya kutokuongezeka uzito kwa mama mjamzito alisema ni kujifungua kwa mtoto mwenye uzito mdogo, ambapo huwa wako hatarini kupata utapia mlo.

Kwa upande wake Mtaalamu wa Sayansi ya Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Tanzania Davis Gisuka anasema mtoto anapokua tumboni anategemea zaidi chakula kutoka kwa mamayake, hivyo ni vyema mama mjamzito kula vyakula vyenye lishe bora,  ili kujenga afya ya mama na mtoto.

 ‘’Tufahamu kwamba mtoto akiwa tumbona anategemea chakula kutoka kwa mama yake tu, hivyo ni vizuri wajawazito kupendelea kula mlo uliokamilika,’’alisema.

 Mapema mwananchi Saida Ali Hamad mkaazi wa Chakechake anasema upo umuhimu mkubwa kwa mjamzito kutumia lishe bora, kwani humsaidia kufikia kiwango cha damu  anachotakiwa kuwanacho mjamzito,ambacho kitamuwezesha kujifungua salama.

 ‘’ Mama mjamzito anatakiwa awe na kiwango cha damu kisichopungua uzito 12, hivyo endapo kama hatokula vyakula vya lishebora kutapelekea kutoakea kwa athari hususani wakati anapojifungua,’’alieleza.

 Hadia Kombo Ali ambae anaujauzito wa miezi sita mkaazi wa Micheweni alisema kula vyakula vya lishe bora kwa mjamzito ni muhimu, kwani hujenga afya ya mama na mtoto.

 Alisema yeye mumewake amekua akimtafutia lishe bora, na kwa mara ya mwisho alipokwenda Cliniki aliambiwa afya pamoja na uzito wake uko vizuri na kwenye kiwango kinachotakiwa.

 Mwananchi Sheha Ali Said aliwakumbusha wanaume wenzake kuhakikisha wanawashughulikia wenza wao ipasavyo na kuwapa huduma muhimu ikiwemo lishe bora, ili kuonesha upendo kwa mama na mtoto alie tumboni.

 Nae Afisa Mdhamini wizara ya Afya Khamis Bilali Ali alisema ili mtoto azaliwe akiwa salama ni vizuri kujengewa mazingira bora na salama tokea akiwa tumboni kwa mama yake.

 Alisema ni vyema wazazi wa kiume kuhakikisha wanakua karibu na wenza wao na kuwapatia lishe bora hususani wakati wanapokua na ujauzito, ili kumlinda mtoto na maradhi ya utapiamlo wakati atakapo zaliwa.

 ‘’Niwaombe wanaume wenzangu wakati wake zetu watakapokua na ujauzito tupunguze pirika tuwe karibu nao, tuoneshe upendo kutamsaidia ajifungue akiwa na hali nzuri,’’alishauri.

 Alisema kwa mujibu wa kitaalamu ya Sayansi ya Makuzi, Malezi na Maendeleo ya awali ya mtoto, mtoto anapokua tumboni anasikia kila kitu kinachofanyika ulimwenguni, hivyo endapo kama wazazi watakua wanaishi kwa  upendo na furaha, kunamjenga mtoto na kujihisi yuko kwenye familia bora.

 Kwa mujibu wa ripoti ya UNICEF ya mwaka 2021, ambayo ilifanyika katika Mkoa wa Pwani, ilibaini kuwa ni asilimia 28 tu ya wanawake wajawazito waliokula vyakula kutoka katika  makundi matano ya  au zaidi.

 Pia ulibaini kuwa kuna asilimia 18 tu wanawake wajawazito waliokua na uwelewa wa kutosha kuhusu lishe bora, ambapo hali hiyo inachangia ulaji usiofaa na hatimae husababisha matatizo kwa mama mjamzito.  


  

 


    

 


Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’