WAJASIRIAMALI WAOMBA KUPATIWA ELIMU YA UTENGENEZAJI BIDHAA



          NA FATMA HAMAD, PEMBA

WAJASIRIAMALI kisiwani Pemba wameomba kupatiwa elimu ya usarifu wa bidhaa,  ili waweze kutengeneza bidhaa zenye ubora na zenye viwango, ambazo zitauzika katika Soko la ndani na nje  ya Pemba.

Wajasiriamali hao walitoa ombi hilo katika mafunzo ya ujuzi wa kidijitali yaliyofanyika kituo cha Uwalimu TC Wingwi wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba.

Biamu Omar Mbrouk mwanakikundi cha Hapa kazi kutoka Wingwi, ambacho kinajishughulisha na utengenezaji wa sabuni, mafuta, na unga wa mwani, alisema wamekua wakitengeneza bidhaa nyingi lakini zinashindwa kuuzwa hata Unguja, na huishia kuuzwa mitaani tu kutokana na kukosa ubora.

Alisema Mwani umebainika kuwa ni moja ya dawa inayotibu  magonjwa mengi katika mwili wa mwanadamu, hivyo ni vyema kupatiwa  elimu, ili wawe wazalishaji bora.

‘’Tunatamani siku moja kuona kwamba, na sisi tunaziuza Tanzania bara na hadi Nchi za nje bidhaa zetu, kwani kutatuwezesha tuweze kutambulika na pia kuinua uchumi wetu,’’alisema.

Ali Khatib Ali mjasiriamali wa kikundi cha Tumuombe Mola cha Makangale kinachojishughulisha na ufugaji wa Majongoo ya baharini, alisema wanahitaji kupatiwa elimu juu ya usarifu wa mazao hayo, ili waweze kuzalisha kwa kuzingatia viwango na kiutaalamu.

Alisema kuna utaalamu wa kulima na kuchakata wakati wanapovuna, ingawa wao bado wanafanya tu, jambo linalopelekea kukosa bei wanayoihitaji.

 ‘’Mukisha kuwavua wanautaalamu wake wa kuwachakata lakini sisi hatujui, bali tunawachemsha tu na badae ndo tnawauza, kikukweli tunahitaji kupewa elimu,’’alisema.

 Alisema endapo watapatiwa elimu kutawasaidia kufuga kwa uwelewa, na kupata bei nzuri inayolingana kilimo hicho, ambacho kitawawezesha kujikimu kimaisha.

Nae Abdala Salim Masoud mwanakikundi cha Ipo sababu ambacho kinajishughulisha na ukulima wa mwanai alisema wanahitaji kupatiwa elimu ya utengenezaji wa pagi za plastiki kwa ajili ya kufungia mwani wao, ili waondokane na na changamoto ya upatikanaji wa pegi hizo.

‘’Tunapokata pegi za mikanda au mibura haturuhusiwi, kwani tunaharibu mazingira, hivyo tunahitaji kupatiwa elimu tutengeneze pegi za plastiki, ili tuondokane na usumbufu na tuzalishe mwani kwa wingi,’’alieleza,’’

Alisema Kampuni ya mwani ya Sewedi Coporation walishawahi kwenda na kufanya utafiti wa kutengeneza pegi hizo, ingawa hadi sasa hawakurudi tena kwa ajili ya kuwapatia elimu hiyo.

Akifungua mafunzo hayo kwa niaba ya Mratibu wa Fawe Winnifred Yatuma Manawi Mjumbe wa bodi ya Fawe Zanzibar Biubwa Mohamed Mselem aliwataka  wajasiriamali hao, kuyatumia mafunzo watakayopewa, ili waweze kuleta mabadiliko katika vikundi vyao.

‘’Nyinyi wajasiriamali ambao mmebahatika kushiriki kwenye mafunzo haya, naomba muyachukue na muyafanyie kazi, ili muendeleze vikundi vyemu na muweze kuzalisha kwa mazao kwa wingi na kujingizia kipato,’’alisema.

Alisema lengo la FAWE ni kuwakomboa wanawake na vijana kiuchumi, hivyo ni vyema kuhakikisha wanayafanyia kazi, ili wawe wazalishaji na watengenezaji wa zuri wa bidhaa.

Mafunzo hayo ya sikumbili kwa vikundi vya wajasiriamali yameandaliwa na Jumuia inayoshughulikia na kutoa masuala ya wanawake na watoto, vijana na watu wenye ulemavu (FAWE)chini ya ufadhili wa UN WOMEN.




 

Comments

Popular posts from this blog

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’