Posts

Showing posts from August, 2025

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZAI ADUI MWINGINE MPYA KWA WANAWAKE, HUATHIRI MFUMO WA UZAZI

Image
  Kumbe kukosa mtoto, na magonjwa nyemelezi ni sehemu yake               NA FATMA HAMAD, PEMBA SARATANI ya shingo ya kizazi ni ile ambayo, hutokana na mabadiliko ya mfumo wa chembe chembe au seli zilizomo katika shingo ya kizazi na wingine wakiita mlango wa kizazi. Saratani hii huathiri shingo ya kizazi, ambayo ni sehemu ya chini ya mfuko wa kizazi, ambapo kwa kawaida huonekana pale tu mwanamke, anapolala chali na inaweza kuonekana kupitia uke wake.   Kwa mujibu wa Shirika la Afya Ulimwenguni ‘WHO’ inathibitisha kuwa, saratani hii, ni ya nne kwa kuathiri wanawake, ikiwa na wagonjwa wapya 604,000 mnamo mwaka 2020.   Takriban asilimia 90 ya vifo 342,000 vilivyosababishwa na saratani ya shingo ya kizazi, vilitokea katika nchi za kipato cha chini na cha kati.   Viwango vya juu zaidi vya saratani hiyo na vifo ni kutoka Afrika, kusini mwa Jangwa la Sahara, Amerika ya Kati na kusini Mashariki mwa Asia.   Tak...

WAJAWAZITO WATAKIWA KUTUMIA LISHE BORA

Image
NA FATMA HAMAD, PEMBA AKINAMAMA wajawazito wamehimizwa kula vyakula vyenyelishe bora, ambavyo vinapelekea kuongezeka kwa uzito miilini mwao, ili kulinda afya ya mama, kumfanya mtoto azaliwe akiwa salama. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko Chakechake Kaimu Mratibu wa Kitengo cha Lishe kisiwani Pemba Said Abdi Said alisema   lishe hupelekea kuongezeka kwa uzito kwa mama mjamzito, na pia kunasababisha ukuaji   kwa mtoto alie tumboni. Alisema   mjamzito anatakiwa kuongezeka   uzito wastani wa kilo nane hadi 12, kwa kipindi chote cha ujauzito wake, hivyo ni vyema kutumia lishe bora, ili kulinda afya na usalama kwa mama na mtoto. ‘’Kuongezeka kwa uzito kwa mjamzito ni muhimu, hivyo jitahidini kutumia lishebora ili kuboresha afya ya mama na mtoto aliemo tumboni,’’alisema. Alisema   mjamzito anatakiwa kula mlo kamili wenyemchanganyiko wa vyakula kutoka katika mchanganyiko wa makundi sita kama vile Mboga, Matunda, Samaki kila siku ili kuongeza uzito kat...

Wazazi watakiwa kuvunja ukimya kwa watoto wao

Image
                    NA FATMA HAMAD, PEMBA WASAIDIZI WA SHERIA wametakiwa kuielimisha jamii kuwa na utaratibu wa kukaa na watoto wao na kuzungumza nao, waweze kujitambua, ili wajiepushe na vitendo vya udhalilishaji. Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mradi wa sauti ya mwanamke Hamisa Bakari Hamad wakati akizungumza na wasaidizi wa Sheria wa wilaya ya Micheweni katika mafunzo ya Usawa wa kijinsia yaliofanyika kituo cha Uwalimu Wingwi mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema katika ulimwengu wa leo wazazi waliowengi wamekosa utamaduni wa kukaa na watoto wao na kuwafundisha umuhimu wa kujitunza,na kuwa na khofu ya kujiepusha na vitendo vya udhalilishaji. ‘’Kuna watoto wamekuwa wakifanyiwa udhalilishaji lakini wanashindwa kutoa taarifa majumbani kwao, na wazazi wanashindwa kuwagudua kutokana na kukosa usubutu wa kukaa nao kjenga nao ukaribu,’’alisems. Alisema ili kuwalinda watoto na vitendo vya udhalilishaji, ipo haja kwa wasaidizi wa Sheria k...

WAJASIRIAMALI WAOMBA KUPATIWA ELIMU YA UTENGENEZAJI BIDHAA

Image
          NA FATMA HAMAD, PEMBA WAJASIRIAMALI kisiwani Pemba wameomba kupatiwa elimu ya usarifu wa bidhaa,  ili waweze kutengeneza bidhaa zenye ubora na zenye viwango, ambazo zitauzika katika Soko la ndani na nje  ya Pemba. Wajasiriamali hao walitoa ombi hilo katika mafunzo ya ujuzi wa kidijitali yaliyofanyika kituo cha Uwalimu TC Wingwi wilaya ya Micheweni mkoa wa Kaskazini Pemba. Biamu Omar Mbrouk mwanakikundi cha Hapa kazi kutoka Wingwi, ambacho kinajishughulisha na utengenezaji wa sabuni, mafuta, na unga wa mwani, alisema wamekua wakitengeneza bidhaa nyingi lakini zinashindwa kuuzwa hata Unguja, na huishia kuuzwa mitaani tu kutokana na kukosa ubora. Alisema Mwani umebainika kuwa ni moja ya dawa inayotibu  magonjwa mengi katika mwili wa mwanadamu, hivyo ni vyema kupatiwa  elimu, ili wawe wazalishaji bora. ‘’Tunatamani siku moja kuona kwamba, na sisi tunaziuza Tanzania bara na hadi Nchi za nje bidhaa zetu, kwani kutatuwezesha tuweze kutambu...

‘’KATIBU MKUU ELIMU ‘’TOENI ELIMU YA MALEZI BORA’’

Image
  NA FATMA HAMAD, PEMBA Katibu mkuu wizara ya   Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdala Said amewataka wandishi wa habari kuielimisha jamii kufahamu umuhimu wa malezi na makuzi ya awali ya mtoto, ili kufahamu utaratibu wa kuwalea katika kipindi hicho,   na kupatikana kizazi chenye afya njema. Alisema katika visiwa vya Zanzibar bado kuna tatizo la udumavu kwa watoto   kutokana na kukosa huduma muhimu kama vile Afya, Chakula bora, ulinzi pamoja na ushirikishwaji, hasa   katika kipindi cha awali   cha   malezi,   makuzi na maendeleo ya mtoto. Katibu Mkuu huyo aliyasema hayo wakati akifunga mafunzo ya siku nne Waandishi Vinara wa ECD Zanzibar, yaliofanyika Mjini Dar esalam. Alisema wandishi wa habari wanajukumu kubwa katika jamii, hivyo ipo haja kuwaelimisha kufahamu umuhimu wa malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto, ili kupata kizazi chenye madili na afya bora. ‘’Ndugu zangu wandishi wa habari nyinyi   mnadhima kubwa ka...

WAZAZI KUWENI KARIBU NA WATOTO WENU

Image
          NA  FATMA HAMAD, Dar-Es-Salaam   ELIMU ya malezi na makuzi bora ya watoto inahitajika katika jamii ili kuhakikisha wazazi wanalea watoto wao katika malezi yaliyobora.   Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa wa hoteli ya Jamirex jijini Dar-Es-Salaam, Mtaalamu wa Sayansi ya Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto nchini Tanzania David Gisuka alisema, kuna baadhi ya wazazi wana tabia ya kushughulikia zaidi kazi zao na kuwaacha watoto wao wapweke, hali ambayo inawasababishia udumavu wa akili na kimwili.   Alisema kuwa, watoto wanahitaji ukaribu wa wazazi wao ili kujifunza mambo mbali mbali ambayo yatawajenga kiakili, hivyo ni vyema wakatenga muda maalumu kwa ajili ya watoto wao.   "Mtoto anaanza kujifunza akiwa tumboni mwa mama yake, hivyo tunatakiwa kuwa karibu nao zaidi na tuwape malezi bora ili wakue vizuri, hii itamfanya awe imara na mwenye uwelewa wa hali ya juu," alisema Mtaalamu huyo.   Kwa upand...

WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUJIUNGA NA MAJUKWAA YA WANAWAKE

Image
  NA, FATMA HAMAD-PEMBA Mkurugenzi  Idara ya Maendeleo  ya Jamii Jinsia wazee na Watoto Zanzibar Siti Abasi Ali amewataka Viongozi wa Majukwaa ya Wajasiriamli Wanawake Kisiwani Pemba kuhakikisha wanavishajihisha Vikundi Vya Ujasiriamali kujiunga na Majukwaa hayo  ili viweze kuwezeshwa kwa  kupatiwa mikopo ya kujiendeleza kiuchumi. Mkurugenzi  huyo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Wenyeviti wa Majukwaa wa wilaya Nne za Pemba katika hafla ya ufunguzi wa Mafunzo ya kuwajengea uwezo wajasiria mali hao. Alisema Vikundi vitakapo jiunga na majukwaa hayo itakuwa rahisi kupatiwa mikopo ya kujiendeleza katika harakati zao . Alisema Serikali imeaanzisha majukwaa ya Wajasiriamali wanawake kwa ajili ya kuwaunganisha Pamoja na kuwa na sauti moja ili waweze kujadili shida walizonazo . Alisema hatua hiyo itakuwa rahisi kuweza kuwafikia kwa wepesi katika kuwasidia kwa kuwapatia mitaji ya kujiendeleza kiuchumi, ili  waondokane na utegemezi na unyanyasi wanaoupata...