‘’Wandishi wa Habari msiandike habari, zenye kuleta migongano’’
Mkuu wa Mkoa
wa Kusini Pemba Rashid Hadid Rashid amewataka wandishi wa habari kuandika
habari zenye ukweli na zenye kuzingatia maadili, ambazo hazitosababisha uvunjifu wa amani Nchini.
Mkuu huyo
ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano la wadau wa Habari, lililoandaliwa na Ofisi ya Rais Ikulu huko
ukumbi wa ZRA Chakechake Pemba.
Alisema
vyombo vya Habari ndivyo ambavyo vinaweza vikaiweka Nchi katika hali ya Amani,
ama kwenye migogoro, hivyo ni vyema wandishi mkatumia maadili yenu na kuandika
habari zenye ukweli na zenye kuleta maendeleo,ili kuibakisha Nchi katika hali Utulivu.
Alisema
Serikali ya awamu ya nane imefanikiwa kuweka mambo mbalimbali ya maendeleo
mjini na vijijini, hivyo ni jukumu lenu wandishi wa habari kuyandikia maendeleo
hayo.
‘’Yapo mambo
mengi ya maendeleo ambayo yamefanywa na Serikali yetu, hivyo yaandikeni hayo,
ili yapate kufahamika, msiandike mambo ambayo yataleta uchochezi,’alieleza.
Kwa upande
wake Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja aliwasisitiza wandishi wa
habari kuzingatia takwimu wakati wanapoandika habari zao.
‘’Ili uwe
mwandishi mzuri na kazi zako ziwe zinavutia na zinasomwa na watu wengi, ni
lazima uwe unatumia takwimu katika Makala yako ama kipindi chako,’’alisisitiza.
Mapema Afisamdhamini kutoka Tume ya Mipango Pemba
Khamis Issa alisema wandishi wa Habari wananafasi kubwa, hivyo ipo haja kuibua
kero na changamoto zilizoko, zieze kufahamika Ili Serikali iweze kuzitatua.
‘’Juzi
wakati mheshimiwa Rais akiwa kule uwekezaji Micheweni alisema sasa ni zamu ya
Pemba, jee kama wandishi wa habari mnafanyanini, kuona mnayaibua hayo maeneo
ambayo bado kuna changamoto ili
mkaisaidia Serikali,’’alisema.
Nao wandishi wa Habari walioshiriki Kongamano hilo wamesema ni vyema kufanyiwa marekebisho baadhi ya Sheria ambazo zinakwaza uhuru wa utekelezaji wa majukumu yao.
Comments
Post a Comment