Wandishi ibueni kero zinazowakwaza wanawake, kushindwa kutimiza ndoto zao za kua viongozi
CHAMA
cha waandishi wa habari wanawake Tanzania Tamwa Zanzibar kimewataka waandishi kisiwani
Pemba kushirikiana pamoja na wahamasishaji jamii ( CBEES ) juu ya maswala
ya wanawake na uongozi ili kuongeza
nguvu na kusaidia kupatikana kwa ufumbuzi wa changamoto mbali mbali
zinazowakabili wanawake na kuongeza ushiriki wao katika nafasi za
uongozi.
Wandishi
wa Habari wametakiwa kujikita Vijijini, ili waweze kuibua kero zinazowakwaza
wanawake, ambazo zinawafanya washindwe kugombea nafasi mbalimbali katika
uongozi.
Akizungumza
na waandishi hao kutoka vyombo mbali mbali kisiwani Pemba Afisa ufuatiliaji na
tathmini kutoka (TAMWA) Mohamed Khatib
Mohamed waliofika katika mkutano maalum
uliowakutanisha wahamasishaji jamii pamoja na waandishi hao uliofanyika katika
ukumbi wa PEGAO Msingini Chake chake Amesema katika miaka ya nyuma wanawake walikua wako nyuma kushika nafasi za uongozi,
kutokana changamoto mbalimbali ambazo zinakua zinawakabili, hivyo ni wakati kwa
wandishi wa habari kuziibua kero hizo na kuzisemea, ziweze kusikika katika
Mamlaka husika na kuweza kufanyiwa kazi, ili waweze kupata fursa za kushiriki kwenye uongozi.
‘’Wanawake
wamekua wakikumbana na keronyingi ambazo zinawafanya wasiyape kipaombele
masuala ya uongozi,mfano kukosekana huduma za mama na mtoto, Maji safi na
salama, barabra,’amesema Afisa ufuatiliaji na tathmini
Anasema
lengo la mradi wa Swili kuhakikisha
wandishi wa habari wanaielimisha jamii waweze
kubadilika, ili kuona wanawake wanashiriki nafasi mbalimbali za uongozi kuanzia
ngazi ya Shehia hadi ngazi za juu.
‘’Tunatamani
kuona wanawake wanashika nafasi za
masheha, ubunge, uwakilishi pamoja na ngazi tofauti tofauti,’’amesema.
Mapema
Omar Mjaka Omar ambae ni miongoni mwa wahamasishaji jamii kutoka wilaya ya
Micheweni anasema wandishi wa habari ndio sauti ya wanyonge, hivyo ipi haja
kufanya majukumu yao kwa uwadilifu ya
hali ya juu, ili waweze kuwasaidia wananchi juu ya kero zinazowakwaza vijijini
mwao.
‘’Nyinyi
wandishi wa habari ni watu humimu katika jamii, hivyo msiweke mbele maslahi
bali fanyeni kazi kwa ajili ya kuwasaidia wananchi pamoja na Taifa kiujumla,’amesema.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa mradi wa Swil kisiwani Pemba Hafidh Abdi Said amesema
endapo wandishi wa habari watafanya kazi
ipasavyo ya kuwahamasisha wanajamii juu ya masuala ya uongozi, wanawake
wataweza kushawika na kuhakikisha wanaingia kwa wingi majimboni, ili lile lengo
la hamsini kwa hamsini kwenye uongzi liweze kufikiwa.
Nao wandishi wa habari walioshiri kikao hicho wamesema ili kuona wananchi wamefikiwa na kupaza sauti zao, ipo haja ya kuepo na mashirikiano ya hali yaa juu kati yao na timu hiyo ya wahamasishaji jamii (CBEES.
Katika mradi huo wa kuwawezesha wanawake waweze kushiriki nafasi mbalimbali za uongozi, umefadhiliwa NORWE ambao unatekelezwa na TAMWA, PEGAO, ZAFELA NA JUWAUZA.
Comments
Post a Comment