WAKULIMA BADO WALIA NA BEI NDOGO YA MWANI
NA FATMA HAMAD, PEMBA
WANAKIKUNDI CHA TUMAINI kilichopo shehia ya Michenzani Mkoani Pemba ambacho kinajishughulisha na ukulima wa kilimo cha Mwani, wametupa kilio chao kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwangalia tena kwa jicho la huruma, kwa kuongeza bei ya mwani.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mwanakikundi Biwanu Ngwali Faki alisema bei ya mwani ya kilo shilingi miasaba (700) ni ndogo, ukilinganisha na gharama wanazozitoa wakati wa kulima.
Alisema lengo la Serikali ya Mapinduzi ya awamu ya Nane ni kuwaimarisha wakulima wa Mwani kichumi, hivyo ni wakati kuongeza bei hadi shilingi 2000.
‘’Kwaweli bei ya shilingi miasaba inatuumiza kazi ni ngumu, ukiangalia Tunanunua Kamba pamoja na taitai kwa gharama kubwa,hivyo tunaiomba Serikali ituengezee bei, ifike angalau elfu 2000,’’ alisema.
Kwa upande wake mwanakikundi Kazija Ali Bakar alisema bado wakulima wa mwani hawajanufadika na zao hilo, kwani kilimo hicho kina changamoto nyingi.
‘’Kiukweli hasa tusifichane wanaonufaika na zao la mwani ni makampuni yanayo nunua mwani na sio wakulima, wakulima tunaishia kunyanyasika na kuumia tu,’’ alieleza.
Katibu wa kikundi hicho Zakia Omar Ngwali alisema asilimia 80 ya wakaazi wa Shehia hiyo wanategemea kilimo cha mwani kuendesha maisha yao, hivyo ipo haja kwa Serikali kufikiria kuongeza bei.
Aidha alisema wanakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa vitendea kazi ikiwemo Boti za kuchukulia mwani.
‘’Tunasikia tu kama kuna boti za mkopo ila sisi hatujazipa, hivyo tunawaomba wahusika watufanyie msada na sisi watupatie tunateseka,’’alieleza.
Alisema wanatarajia katika mwaka huu wa 2025 kiwanda hicho kitanza uzalishaji wa bidhaa zinazotokana na mwani, hivyo wakulima watapata fursa ya kuuza bidhaa hiyo kwa bei nzuri.
Alisema kiwanda hicho kitakua na uwezo wa kuchakata tani zaidi 30,000 za mwani kwa mwaka, hivyo waendelea kuvumilia.

Comments
Post a Comment