Posts

Showing posts from March, 2025

TIMU ZA WANAWAKE ZA PEMBA ZAOMBA KUSHIRIKISHWA KWENYE MASHINDANO YA KITAIFA

Image
                         NA FATMA HAMAD-PEMBA Kukosekana kwa uwanzishwaji wa ligi maalumu kwa wachezaji wanawake,  imekua ni kikwazo kikubwa kinachokwamisha Timu ya Mpira wa pete iliyopo Mchangamdogo  Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Hayo yamesemwa na Amina Kudra Ali Mchezaji wa timu ya mpira wa Pete ya Wete wakati wakizungumza na wandishi wa habari ikiwa ni ufuatiliaji wa tathmini ya mafanikio wa mradi wa michezo kwa maendeleo uliokua ukitekelezwa na Chama cha wandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar (TAMWA), Chama cha wanasheria wanawake (ZAFELA)   na CYD. Anasema anahamu ya kua mchezaji mkubwa duniani, lakini anarudinyuma kwasababu tangu walipoanzisha timu hiyo hawajashirikishwapo mashindano  ya ligi za aina yoyote na kuweza kukuza vipaji vyao. ‘’Huu ni mwaka wa tano tokea kuanzisha timu yetu hii ya mpira wa pete pamoja na Netball, lakini tunakata tama hatujashirikiswapo hata siku mo...

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

Image
                        NA  FATMA HAMAD- PEMBA WANANCHI WA KIJIJI cha Gombeume Shehia ya Mchangamdogo   Wilaya  ya  Wete  Mkoa wa Kaskazini  Pemba,  wamelalamikia  juu  ya  ukosefu  wa  huduma  ya  Maji  safi  na  salama   kijijini hapo. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi huko kijijini kwao Gombeume mwananchi Bishamba Suleiman Ali na  Fatma Said Haji wamesema huu ni zaidi ya mwaka wa tatu hawapati huduma ya maji katika kijiji chao. Walisema wamechoka na kadhiya hiyo ambayo inawafanya waende  mabondeni  kufuata huduma ya maji,  kwa  ajili  ya  matumizi  ya  majumbani  mwao. ‘’Kwakweli tuna shida kubwa wananchi wa gombeume, tunakwenda mabondeni kwenye visima vya zamani kuchota maji,  tunaumia na tumechoshwa na shida hiyo,’’walisema. Walisema wanahofu ya kujakupata  m...

JAMII YAOMBWA KUWASHIRIKISHA WANAWAKE KWENYE MICHEZO

Image
                                     NA FATMA HAMAD, PEMBA Katika zama za sasa suala la michezo limekuwa ni moja ya njia ambayo hupelekea baadhi ya watu kujipatia fursa mbali mbali za maendeleo, ikiwemo ajira. Tumekuwa tukishuhudia kuwa vijana wakiajiriwa katika taasisi za Serikali ikiwemo kwenye vikosi vya Polisi, kuajiriwa kwenye timu za ndani na nje ya nchi. Lakini fursa hizo mara nyingi huzipata vijana wa kiume, kwani jamii bado haijakuwa na mwamko wakutosha kufahamu kwamba, mwanamke na yeye anahitaji kuzipata fursa hizo. Hadi leo hii bado jamii imekuwa na mawazo kwamba mwanamke akishiriki michezo atakua hana maadili mazuri, hali inayopelekea siku zote kuishia kuwa watazamaji na washangiliaji katika suala la michezo. Kwa mujibu wa dini, mwanamke ameruhusiwa kushiriki michezo, kwani michezo ni moja ya njia ya kuufanya mwili kuwa imara na kuweza kupambana kwa kila magonjwa kwa sababu ni mazo...

WANAWAKE WAMUOMBA DOKTA SAMIA KUWAUNGA MKONO KENYE UONGOZI

Image
NA FATMA HAMAD- PEMBA WANAWAKE WA CHAMA CHA Wananchi CUF wamemuomba Raiswa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kulinda haki za wanawake wa vyama vya upinzani watakaojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi wa Oktaba mwakahuu,  ili nafasi za wanawake ziwenyingi zaidi. Ombi hilo limetolewa na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Wanawake ya CUF Taifa Anna Rioba Paul katika maadhimisho ya siku ya siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika huko Vikunguni, Wilaya ya ChakeChake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema wanawake wengi wa vyama vya upinzani kikiwemo CUF wamekua na shauku ya kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, lakini wamekuwa wakienguliwa kwa kisingizio cha kuwepo makosa katika fomu za maombi za uteuzi, jambo ambalo ni tofauti na upande wa Chama Tawala CCM, Alisema kuepo na changamoto hiyo imekua ikikatisha ndoto za  wanawake  wanaotaka kugombea, na kupelekea kubakia nyuma katika nafasi za uongozi.   ‘’   Tunakuomba Rais...

Yafahamu mavazi ambayo anatakiwa kuvaaa mwanamke akiwa kwenye michezo

Image
                          NA FATMA HAMAD, PEMBA MAUMBILE ya mwanamke kikawaida mwili wote hautakikani kuonekana isipokuwa viganja vya mikono na uso tu. Na ndio maana wanatakiwa kujisitiri mwili mzima popote watakapokuwepo, ili kulinda zaidi heshima zao. Kama Qur-an tukufu ilivyoeleza katika suratul Nour aya ya 31… ‘Na waambie waumini wanawake wainamishe macho yao na wazilinde tupu zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika (viganja vya mikono na uso)’. ‘…Na waangushe shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa waume zao au kaka zao au wana wa kaka zao, au wana wa dada zao au wanawake wenzao au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, au wafwasi wanaume wasio na matamanio au watoto ambao hawajajua mambo yaliyohusu uke’ ‘…Wala wasipige chini miguu yao ili yajulikane mapambo waliyoyaficha. Na tubuni nyote kwa Allah (Subhanah...

ZSSF yawataka Masheha kuwaripoti wanachama waliofariki

Image
                               NA FATMA HAMAD – PEMBA MASHEHA WA MKOA WA KUSINI Pemba wametakiwa kutoa taarifa    katika  Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) endapo kutatokea  kifo cha mwanachama wa mfuko huo katika shehia zao, ili kupunguza udanganyifu hasa katika malipo ya fedha za Serikali. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mafao kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ZSSF Zanzibar Mussa Yussuf wakati akiwasilisha mada ya dhima ya Masheha katika utoaji wa huduma za ZSSF katika kikao kazi kilichofanyika Tibirinzi Chakechake Pemba. Alisema kumekuwepo na baadhi ya watu wamekua wakipeleka taairifa za vifo vya jamaa zao  katika mfuko huo ambazo si za ukweli, hivyo endapo watapeleka taarifa wataepusha kutokea kwa udanganyifu  huo, sambamba na kuokoa fedha za Serikali. ‘’Wamekua wakitujia watu na taarifa za jamaa zao kufariki na kudai mafao yao, lakini tukifanya uchunguzi tunagundua kwamba sio ...

Wastaafu anzisheni miradi ili iwasaidie baada ya kustaafu

Image
  NA FATMA HAMAD- PEMBA Afisa Mdhamini Ofisi ya Raisi Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala bora Halima Ali Khamis amewataka wastaafu watarajiwa kuyatumia mafao yao ya kustafu kwa kuanzisha miradi ya maendeleo ambayo itawapatia kipato ili waweze kuendesha maisha yao. Mdhamini huyo ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya mandalizi ya kustaafu kwa wastaafu watarajiwa huko Tibirinzi Chakechake Mkoa wa Kusini Pemba. Alisema kustaafu sio mwisho wa maisha bali ni vyema wakajiwekea akiba pamoja na miradi mbalimbali, ili waweze kuishi maisha yao ya kawaida kama walivyokua wakiwa kazini. ‘’ Niwaombe wazazi wangu,tusishtuke, bali tijiekeze, tusizitumie pesa zetu kwa kuzifanyia mambo ambayo hayatatuletea faida kwetu,’’alisema. Aidha  aliwapongeza watumishi hao kwa kuwa na moyo wa imani na kuutumikia vyema utumishi wao hadi kufikia muda wao  wa kustaafu, huku akiwataka waache khofu wakati watakapopaew barua zao za kuustaafu, kwani ni jambo la kawaida kwa kila mtumishi wa umma....