
NA FATMA HAMAD - PEMBA
Wanawake wametakiwa
kuacha tabia ya kuweka vitu kwenye sehemu za siri, kwani wanaweza kuathiri
mfumo mzima wa viungo vya uzazi.
Hayo yamesemwa na Mratibu
wa Tume ya Ukimwi Pemba (ZAC) Ali Mbarouk Omar wakati Akizungumza na waandishi wa habari
katika Ukumbi wa chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania (TAMWA)
ZANZIBAR Ofisi Pemba, alisema, wapo
baadhi ya wanawake huweka vitu katika sehemu zao za siri, jambo ambalo ni
hatari kwa afya ya uzazi.
Alisema kuwa, ni vyema
wakaenda hospitalini na vituo vya afya
kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa mara kwa mara, endapo wamepata matatizo
waweze ili waweze kupatiwa matibabu na
sio kuweka vitu ambavyo vinaweza kuwapatia madhara zaidi.
"Kuna baadhi yao
huweka vitu kama wanajitibu baada ya kupata magonjwa ya kujamiiana na kuna
wengine wanaweka vitu hivyo kwa urembo, haya yote hayafai kwa sababu wanaweza
kuathirika katika mfumo wa kizazi," alisema Katibu huyo.
Aidha, akielezea
kuhusu maambukizi ya magonjwa ya kujamiiana alisema, pia yanasababisha kuathiri
kizazi cha mama na kupeleka mtoto anaezaliwa kupata madhara mbali mbali.
"Maradhi ya
kuambukiza ikiwemo ukimwi, saratani ya shingo ya kizazi, gonoria, pangusa,
kisonono cha usaha ni hatari katika kuharibu mfumo mzima wa uzazi kwa mwanamke,
hivyo waache tabia ya kufanya ngono zembe kuepuka magonjwa hayo,"
alieleza.
Akifungua
mkutano huo Afisa Mawasiliano kutoka TAMWA Zanzibar Khairat Haji Ali alisema
kuwa, elimu ya afya ya Uzazi ni muhimu na
inahitajika iwafikie wanajamii, hivyo ipo haja kwa waandishi wa habari kutumia
kalamu zao katika kuielimisha jamii.
Alisema kuwa, wameamua
kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili kusudi waelewe masuali ya afya ya
uzazi, jambo ambalo litawasaidia kutoa elimu kwa jamii wakiwa na ujuzi wa hali
ya juu.
"Wanawake
wanapata shida kubwa kwenye mfumo wa uzazi bila kujijua, hivyo iwapo waandishi
tutaweza kutoa elimu, jamii itaelewa na watakuwa ni wenye kupima afya zao na
kuacha Yale ambayo yatawasababishia matatizo," alisema.
Akitaja baadhi ya
dalili za maradhi ya kujamiiana Mratibu
wa kituo cha Tiba na Kinga Rahila Salim
Omar, ni maumivu chini ya kitovu,
majeraha sehemu za siri, kuharibika kwa mimba, kutokwa na maji maji mazito
sehemu za siri yenye rangi na harufu.
"Kuweka vitu
sehemu za siri pia kunasababisha saratani ya shingo ya kizazi, hivyo waandishi
nijitahidi kuielimisha jamii yetu," alifahamisha.
Kwa upande wao
washiriki wa mkutano huo walisema kuwa, watahalikisha wanaibadilisha jamii kwa
kuwapa elimu ya afya ya uzazi, ili kuondosha madhara yanayowapata wanawake na
watoto.
"Tumejifunza
mambo mengi ya afya ya uzazi, hivyo kupitia elimu hii, itatusaidia kuielewesha
jamii ili wajitunze na kuepuka madhara mbali mbali," anaeleza.
Mafunzo hayo ya siku
mbili waandishi wa vyombo vya habari mbali mbali kisiwani Pemba yameandaliwa na Chama cha Wandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar.
Comments
Post a Comment