Wasaidizi wa sheria wapewa mbinu
NA FATMA HAMAD- PEMBA
Wasaidizi wa Sheria wametakiwa kuendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya masuala ya
udhalilishaji, ili kuona inaondokana na vitendo hivyo viovu ambavyo vimekua
vikijitokeza siku hadi siku.
Akizungumza
katika mafunzo ya kuwajengea uwezo wasaidizi wa sheria wa wilaya ya Micheweni Muhasibu wa Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria
Wilaya hiyo Riziki Ali Hamad juu ya
masuala ya udhalilishaji, huko Tumbe wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini
Pemba.
Alisema
katika wilaya ya Micheweni bado kumekua
kukijitokeza masuala ya ubakaji na ulawiti
kwa watoto, hivyo ipohaja kwa wasaidizi wa sheria kuisaidia jamii kwa
kuwaelimisha madhara yatokanayo na masuala hayo, ili kuona yameondoka.
Akitaja sababu inayopelekea kujitokeza kwa masuala
hayo ya ubakaji na ulawiti katika wilaya
hiyo ni utelekezwaji uliokithiri wa wanawake na watoto.
Alisema wapo
baadhi ya wazazi wa Micheweni huondoka vijijini mwao na kwenda kufanya shughuli zao za uvuvi katika
maeneo mengine kama vile Tanga, Mombasa, Mafia, ambapo mwisho wa siku huziacha familia zao na
kuzitelekeza.
‘’Mababa
wengi wanapondoka na kwenda kufanya shughuli zao za uvuvi maeneo mengine,
huzitelekeza familia zao, na badalayake
hutafuta wanawake wengine na kuanza nao
maisha,’ alisema.
Alisema
kutokana na hilo ipo haja kwa wasaidizi
wa Sheria kukaza kamba kuwaelimisha
wanajamii, ili kuona kila mzazi analea na kutunza familia yake, jambo litalopelekea kuwa muarubaini wa
masula hayo ambayo imeonekana ni kero kubwa kwa wanawake na watoto, hususani
wanaoishi katika maeneo ya bahari.
Alisema kwa
sasa wanatekeleza mradi wa sauti ya mwanamke ambao unalengo la kuwasaidia
wanawake na wasichana na jamii kwa ujumla juu ya masuala ya udhalilishaji, ili
kuona wanaondokana na tatizohilo.
Mapema mkufunzi wa mafunzo hayo Suleiman Hemed
alisema lengo hasa la kutoa mafunzo kwa wasaidizi wa sheria ni kuhakikisha
wanafika kila shehia na kutoa msaada wa
kisheria kwa jamii, ili kuona wanakua na
uwelewa juu ya masuala hayo na kuripoti katika vyombo vinavyo husika wakati
vinapotokea vitendo hivyo na kupata haki zao.
Nao wasaidizi hao wa Sheria akiwemo Othman Juma Nahoda na Ziada Ali Hamad walisema watahakikisha wanatekeleza majukumu yao ipasavyo na kwa mujibu wa Sheria ilivoelekeza, ili kuona jamii imeilimika na kuwa mstari wa mbele kutokomeza udhalilishaji.
Katika Mradi
huo wa Sauti ya mwanamke ambao unatekelezwa na Jumuia ya wasaidizi wa Sheria
Wilaya ya Micheweni ni ufadhili wa Shirika
la Msaada wa kisheria LSF na Umoja wa Ulaya (ENABLE)
.jpg)
Comments
Post a Comment