Tunahitaji kupatiwa maji, tuzalishe mazao kwa wingi ili tujikomboe na umaskini

 


                                           NA FATMA HAMAD –PEMBA

KUKOSEKANA KWA HUDUMA za Maji safi na salama imekua ni kero kubwa kwa wakulima  wanaolima  kilimo msitu katika Shehia za Mjini kiuyu,   Kambini kichokochwe, Mchanga mdogo na Chwale wilaya ya Wete  Mkoa wa Kaskazini Pemba.

 Akizungmza na mwandishi wa habari mara baada ya kuwatembelea katika mashamba yao mkulima Fatma Sheha Juma kutoka Kiuyu minungwini anasema wanahitaji kupatiwa maji katika mashamba yao, ili waweze kukuza vilimo vyao.

Alisema wanapata shida kubeba maji majumbani kwao na kupeleka katika mashamba yao, hivyo wanahitaji kupatiwa msaada wa kuchimbiwa visima karibu na maeneo yao wanayolima, ili waweze kuzalisha mazao kwa wingi.

‘’Kwakweli kubeba maji kwa vichwa  kutoka majumbani hadi mashambani  kwetu tunakolima ni shida  tunaathirika, hivyo tunaomba tuangaliwe,’’alisema Fatma.

Alisema ili waweze  kulima na kuzalisha mazao kwa wingi kunahitajika kupatikana kwa maji ya kutosha  kwa ajili ya kumwagilia mbegu zao.

Kwa upande wake mkulima Fatma Mohamed Shaib alisema wameshaanza kuotesha miche, lakini inakufa kutokana na kukosa maji.

‘’Tulitegemea tuvune mazao mengi ili tuweze kuuza na kupata chakula cha kutosha, lakini mazao yetu yanakufa tunachoka kubeba maji sehemu za mbali,’’alieleza.

Alisema wanahamu ya kulima kilimo msitu lakini wanarudinyuma kutokana na kukosekana kwa maji ya kumwagilia vipando vyao.

Mkulima Kombo Bakari kutoka shehia ya Minugwini  amaeitaka Serikali pamoja na wadau wengine kuwafanyia msada wa kuwatilia umeme ili waweze kujenga visima karibu na mashamba yao.

‘’Tunategemea maji ya mvua, kwa kipindi hiki cha  kiangazi tunakosa maji ya kumwagilia, hivyo tunahitaji tuwekewe umeme, ili tuweze kuchimba  tusitegemee maji ya mvua tu,’’anasema.

Afisa uhusiano wa Mamlaka ya Maji Zanzibar Zawa Ofisi ya Pemba Suleimana Anass Masoud  alisema Mamlaka ya Maji inangalia matumizi ya nyumbani kwanza na sio kwa shughuli za umwagiliaji.

Alisema Wakulima wanaouwezo wa kuchimba visima vyao  wenyewe, isipokua wafuate masharti  kutoka kwa Mamlaka husika ya  Maji safi na salama.

‘’Walio na jukumu la kusaidia maji kwa ajili ya umwagiliaji kwa wakulima wadogo wadogo ni wizara ya kilimo, sisi tunaangali kwanza mahitajio ya wananchi,’’alieleza.

Aidha aliwasisitiza wakulima kutumia  maji kwa uwangalifu ili kuepuka kutokea kwa uharibifu wa miundombinu ya maji, jambo litalosbabisha kukosekana kwa maji kwa wananchi.

Afisa mdhamini wizara ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi, Idirisa Abdulla Hassan alisema katika wizara yake wameweka mkakati maalumu wa kuwasaidia wakulima hususan wadogo wadogo,  ili kuona wanaondokana na changamoto zinazorudisha nyuma vilimo vyao.

‘’Tunahakikisha tunawasaidia wakulima wa vikundi mbalimbali, ili kuona  wanaondokana na changamoto na kuhakikisha wanazalisha mazao kwa wingi.

Nae Mkurugenzi wa Tasisi ya upandaji wa misitu  Pemba  CFP Mbarouk Mussa Omar alisema tayari wameshaomba ufadhili kutoka kwa Serikali ya Kanada CFI wa kuchimbiwa visima wakulima hao ili waweze kuondokana na kero hiyo.

‘’Tayari tumeshaomba ufadhili kutoka kwa wenzetu kutoka Kanada, kuchimbiwa visima ili kuona wakulima hao waweze kupata maji, na kuzalisha mazao ya kutosha.



 

 


Comments

Popular posts from this blog

KERO YA MAJI, TATIZO KWA WANAKIJIJI CHA GOMBEUME

HIVI NDIVYO UTELEKEZWAJI WA WATOTO UNAVYOATHIRI MALEZI, MAKUZI YAO

DNA YA THIBITISHA, MTUHUMIWA NDIE BABA MZAZA WA MTOTO