Jitihada za vyama vya sisa wanazozifanya kwa wanaume, juu ya uongozi kwa mwanamke
Na Salim Hamad-Pemba
Suala la
uongozi ni haki
ya raia wote
na sio kwa wanaumme pekeo .
Kwani Haki ya uongozi imetajwa
katika Kifungu cha 21 (3) cha
Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kinasema kila Mzanzibari
anayohaki ya kushika nafasi yoyote ya kazi
na shughuli yoyote iliyoko
chini ya Mamlaka ya Zanzibar.
Sera na Sheria
mbalimbali za Zanzibar zimeelekeza kutambua haki ya mwanamke kushiriki katika
demokrasia na uongozi.
Historia inatuonesha kwamba uislamu
unaruhusu mwanamke kuwa kiongozi, kwani wapo wanawake kadhaa ambao walishiriki nafasi za mamuzi wakati wa Mtume Muhammad (S.A. W).
Ambapo miongoni mwa wanawake
walioshika uongozi ni Bi Khadija mke wa Mtume
(S.A.W), mtu wa mwanzo kuupokea Uislamu kutoka kwa Mtume Muhammad.
Pia Bi Asma binti Abu Bakar ndie alieongoza kitengo cha utoaji wa tarifa
na habari kwa Mtume ( S .A. W) wakati wa kuhamia Madina.
Hivyo ni wazi kwamba mwanamke anaruhusiwa kushika nyadhifa kwenye
uongozi, ingawa hadi leo tumekua tukishuhudia wanawake kadhaa ambao hupewa talaka
na waume zao, kwa sababu wameingia kwenye siasa.
Makala hii imewatafuta viongozi wa vyama vya siasa na kutaka kufahamu
wanachukua jitihada gani kuwaeilimisha wafuasi wa vyama vyao pamoja na
wananchi, kuona wanawashajiisha na kuwapafursa wanawake, waweze kujiingiza majimboni kwa wingi katika
uchaguzi
mkuu wa Zanzibar wa mwaka huu 2025.
VIONGOZI
WA VYAMA VYA SIASA
Katibu wa Chama cha ACT -WAZALENDO
Mmkoa wa Micheweni kichama Khatib Hamad
Shehe anasema wanachokifanya ni kuwapa
elimu jamii, ili wawape nafasi wanawake
waweze kushiriki kwenye kwenye masuala ya uongozi.
‘’Tunachokifanya kwa sasa tunawahamasisha wanajamii, wawaruhusu wanawake,
waweze kuingia kwa wingi majimboni katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2025 ili
kuepuka talaka hizo za ovyo ovyo,’
Maryam Saleh Juma ni Mwenyekiti wa Mkoa Chakechake Chama cha Ukombozi Chauma
anasema katika Chama chao wamekua wakiwaelimisha wanawake wanaotaka kugombea kwanza
kujielewa, kulinda utu wao na
pia kuheshimu maadili ya dini yao, ili
waweze kujijengea uwaminifu kwa waume zao,
katika kipindi chote
cha uchaguzi.
‘’Tumekua tukitoa elimu siku zote kwa wagombea
wanawake na waume zao, waweze kuaminiana
na kuheshiniana, ili kubakia katika ndoa zao mara baada ya kumalizika kwa
uchaguzi ,’’anaeleza.
Habib Ali Khamis katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kanda ya Pemba anasema
wanachokifanya wao ni
kuwapa mafunzo wanawake wanaotaka kugombea waweze
kujitambua, na kufahamu
wana nafasi gani katika dini yao,
ndoa zao na pia kwenye chama chao.
‘’Tunawaelimisha wanawake kwanza waweze kujitambua na vipi
anapata ruhusa kwa mume wake ya kujiingiza kwenye harakati za
uongozi,’’anaeleza.
Anasema ikitokea kuna mwanamke wamempa elimu na mume wake hakumpa ruhusa, wanawaita wote wawili na kuwaelimisha, na kuona
wanabakia kwenye ndoa yao endapo mwanamke
atagombea.
‘’Endapo kama itatokea kunamwanamke anataka kugombea mume wake hampi ruhusa, hatumuachi tu akapoteza
ndoto yake, bali tunahakikisha
tunamuelimisha mwanamme kufahamu umuhimu na faida
za wa uongozi kwa mwanamke,’’anafahamisha.
Anasema watahakikisha wanatumia njia za busara kuwaelimisha wanaume wa Chama chao
kuwaruhusu wanawake waweze kujitokeza
kwa wingi majimboni katika Uchaguzi wa mwaka
huu, ili kuona hakutokei vitendo hivyo vya
talaka kwasababu
ya mambo ya kisiasa, amemalizia Habib.
Fatma Khamis Rashid (sio jina lake halisi) mkaazi wa Kaskazini Pemba ni mmoja wa walioachwa, na mume wake kwa sababu tu aligombea ‘’Aliniacha mume wangu kisa niligombea,’’anasema.
Uchaguzi ni mchezo wa kidunia kusiwe na migogoro ya ndoa kama hiyo, hivyo ni wakati kwa wanaume
kubadilika na badalayake waweze kuwaruhusau wake zao waweze kugombea, ili waweze kuleta mabadiliko majimboni mwao.
Ni vyema kwa vyama
vya siasa pamoja na
mashirika kama Chama
cha Wandishi wa habari
wanawake Tanzania TAMWA
Zanzibar kuendelea kutoa elimu
kwa jamii juu
ya uongozi kwa
mwanamke, ili waweze kutoa
fursa kwa wanawake.
WANAHARAKATI
Tatu Abdulla Mselem ni mwanaharakati wa masuala ya Utetezi kwa
wanawake, watoto, mayatima na wanaoishi katika mazingira magumu Tujipe Pemba anasema sio jambo la busara katika
ulimwengu huu wa uwatandawazi kusikia
kama kuna mwanamme amemuacha mkewake
kwa sababu tu
ameingia kwenye kinyan’ganyiro cha
uongozi.
Mwanamke nayeye anaweza kuwakiongozi na akaweza kuleta
mabadiliko, hivyo ipo haja kwa viongozi wa vyama vya siasa kuwaelimisha
wanachama wao kufahamu madhara ya kukosekana kiongozi mwanamke, ili waweze
kuwapa ruhusa.
‘’Ili kuona wanawake wamekuwa na uthubutu wa kuingia kwa wingi majimboni
katika uchguzi mkuu ujao, ni lazima vyama vya siasa kufanya jitihada za makusudi kuwelimisha umma hususan
wanaume, ili wawpe fursa wenza wao waingie kwenye mchakato wa uongozi bila ya
vikwazo vyovyote,’’anasema .
Kaimu Mratibu wa
Chama cha wandishi
wa habari wanawake Tanzania
TAMWA - ZANZ Ofisi ya Pemba Amina Ahmed
Mohamed anasema moja ya mkakati walioufanya wameanzisha
wanaume mabadiliko, kwa ajili
ya kuwaelimisha wanaume
wenzao, wafahamu umuhimu wa uwongozi kwa mwanamke.
‘’Tumeanzisha timu ya wanaume mabadiliko , ambao watawahamasisha wanaume wenzao, waweze kuwaruhusu wake zao,
waweze kuingia kwenye majimbo na kugombania,’’naeleza.
Kombo Khatib Bakar (60) mkaazi wa
Kiuyu minungwini anasema ni vyema wanaume kuiga mfano wake, kwani yeye baada ya mke wake kumpa wazo la
kutaka kugombea hakumkatalia,
bali alimuunga mkono.
Anasema alijitoa kihali na mali na kumsaidia mke wake ambae aligombea udiwani jimbo la Wingwi kwa kipindi chote cha Uchaguzi, ili wweze kupata nafasi ya Udiwani ambayo
ndio aliyogombea.
‘’Simkumzui wala sikua na hisia mbaya nae, bali nilimuunga mkono kwa kipindichote, kwani
nilikua namini anaweza kupambana,’’anafahamisha.
Hivyo amewashauri wanaume wenzake kuwa
na uthubutu kama yeye, wawaruhusu
wenza wao kuingia kwenye fursa
mbalimbali za maendeleo ili walete mabadiliko kwenye jamii,’’anafahamisha.

Comments
Post a Comment